Kwa Waebrania 8:1-13

  • Maskani iliwakilisha vitu vya mbinguni (1-6)

  • Tofauti kati ya agano la kale na agano jipya (7-13)

8  Sasa jambo kuu tunalosema ni hili: Sisi tuna kuhani mkuu wa namna hii,+ naye ameketi kwenye mkono wa kuume wa kiti cha ufalme cha Ukuu mbinguni,+  mhudumu* wa mahali patakatifu+ na wa hema la kweli, ambalo limesimamishwa na Yehova,* na si mwanadamu.  Kwa maana kila kuhani mkuu huwekwa rasmi ili kutoa zawadi na dhabihu; basi ilikuwa lazima huyu pia awe na kitu cha kutoa.+  Ikiwa angekuwa duniani, hangekuwa kuhani,+ kwa sababu tayari kuna watu wanaotoa zawadi kulingana na Sheria.  Watu hao hufanya utumishi mtakatifu kwa mfano wa uhalisi na kivuli+ cha vitu vya mbinguni;+ kama vile Musa, alipokuwa karibu kujenga hema, alipewa amri na Mungu: Kwa kuwa Mungu anasema: “Hakikisha kwamba unatengeneza vitu vyote kwa kufuata kielelezo ulichoonyeshwa mlimani.”+  Lakini sasa Yesu amepata huduma iliyo bora* zaidi kwa sababu yeye pia ni mpatanishi+ wa agano lililo bora+ kwa kulinganishwa, ambalo limefanywa imara kisheria juu ya ahadi zilizo bora.+  Ikiwa agano la kwanza halingekuwa na kosa, hakungekuwa na haja ya agano la pili.+  Kwa maana anaona hatia ya watu anaposema: “‘Tazama! Siku zinakuja,’ asema Yehova,* ‘nitakapofanya agano jipya pamoja na nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda.  Halitakuwa kama agano nililofanya pamoja na mababu zao siku niliyowashika mkono na kuwaongoza kutoka nchini Misri,+ kwa sababu hawakuendelea kulishika agano langu, basi nikaacha kuwajali,’ asema Yehova.* 10  “‘Kwa maana hili ndilo agano nitakalofanya pamoja na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo,’ asema Yehova.* ‘Nitazitia sheria zangu katika akili yao, nami nitaziandika katika mioyo yao.+ Nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.+ 11  “‘Nao hawatafundishana tena kila mtu na raia mwenzake na kila mtu na ndugu yake, wakisema: “Mjue Yehova!”* Kwa maana wote watanijua, kuanzia mdogo zaidi mpaka aliye mkubwa zaidi miongoni mwao. 12  Kwa maana nitaonyesha rehema kwa matendo yao yasiyo ya uadilifu, nami sitazikumbuka tena dhambi zao.’”+ 13  Anaposema “agano jipya,” amelifanya lile la zamani lichakae.+ Basi kile kilichochakaa na kuzeeka kiko karibu kutoweka.+

Maelezo ya Chini

Au “mtumishi wa watu wote.”
Au “utumishi wa watu wote ulio bora.”