Kwa Waebrania 4:1-16

  • Hatari ya kutoingia katika pumziko la Mungu (1-10)

  • Himizo la kuingia katika pumziko la Mungu (11-13)

    • Neno la Mungu liko hai (12)

  • Yesu, kuhani mkuu aliye bora (14-16)

4  Kwa hiyo, kwa kuwa ahadi ya kuingia katika pumziko lake bado ipo, acheni tuwe macho* ili yeyote kati yenu asionekane amepungukiwa.+  Kwa maana sisi pia tumetangaziwa habari njema,+ kama walivyotangaziwa; lakini neno walilosikia halikuwaletea faida, kwa sababu hawakuunganishwa kwa imani pamoja na wale waliosikia.  Kwa maana sisi ambao tumeonyesha imani tunaingia katika pumziko, kama alivyosema: “Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu, ‘Hawataingia katika pumziko langu,’”+ ingawa kazi zake zilimalizika tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.+  Kwa maana mahali fulani amesema hivi kuhusu siku ya saba: “Na Mungu akapumzika siku ya saba kutoka katika kazi zake zote,”+  na hapa tena anasema: “Hawataingia katika pumziko langu.”+  Basi, kwa kuwa bado imebaki watu fulani waingie katika pumziko hilo, na wale ambao walitangaziwa kwanza habari njema hawakuingia kwa sababu ya kutotii,+  yeye tena anaweka siku fulani kwa kusema baadaye katika zaburi ya Daudi, “Leo”; kama ilivyosemwa hapo juu, “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu.”+  Kwa maana ikiwa Yoshua+ aliwaingiza katika mahali pa pumziko, Mungu hangesema baadaye kuhusu siku nyingine.  Kwa hiyo bado limebaki pumziko la sabato kwa ajili ya watu wa Mungu.+ 10  Kwa maana mtu ambaye ameingia katika pumziko la Mungu, amepumzika pia kutoka kwenye kazi zake mwenyewe, kama Mungu alivyopumzika kutoka kwenye kazi zake.+ 11  Kwa hiyo acheni tufanye yote tunayoweza ili kuingia katika pumziko hilo, ili yeyote asije akaanguka katika kielelezo kilekile cha kutotii.+ 12  Kwa maana neno la Mungu liko hai nalo ni lenye nguvu+ na lina makali kuliko upanga wowote wenye makali pande mbili+ nalo huchoma hata kufikia kugawanya nafsi* na roho,* na viungo kutoka katika urojorojo, nalo linaweza kutambua fikira na makusudio ya moyo. 13  Na hakuna kiumbe kilichofichwa machoni pake,+ bali vitu vyote viko uchi navyo vimefunuliwa wazi machoni pa yule ambaye tunapaswa kutoa hesabu kwake.+ 14  Basi, kwa kuwa tuna kuhani mkuu sana ambaye ameingia katika mbingu, Yesu Mwana wa Mungu,+ acheni tuendelee kumtangaza hadharani.+ 15  Kwa maana hatuna kuhani mkuu ambaye hawezi kuusikitikia udhaifu wetu,+ bali tuna yule ambaye amejaribiwa katika mambo yote kama tulivyojaribiwa, lakini hakutenda dhambi.+ 16  Basi na tukikaribie kiti cha ufalme cha fadhili zisizostahiliwa tukiwa na uhuru wa kusema,+ ili tupokee rehema na kupata fadhili zisizostahiliwa tunapohitaji msaada.*

Maelezo ya Chini

Tnn., “tuwe na woga.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “zitusaidie wakati unaofaa.”