Nehemia 8:1-18
8 Kisha watu wote wakakusanyika kwa kusudi moja katika kiwanja cha watu wote chenye kilikuwa mbele ya Mulango Mukubwa wa Maji,+ wakamuambia Ezra+ mwandikaji* alete kitabu cha Sheria ya Musa,+ yenye Yehova alikuwa ameamuru Israeli wafuate.+
2 Basi Ezra kuhani akaleta Sheria mbele ya kutaniko+ la wanaume, wanamuke, na wote wenye wangeweza kusikiliza na kuelewa, katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba (7).+
3 Na akawasomea kwa sauti kubwa+ Sheria hiyo wanaume, wanamuke, na wote wenye wangeweza kuelewa, katika kiwanja cha watu wote chenye kilikuwa mbele ya Mulango Mukubwa wa Maji, kuanzia asubui sana mupaka katikati ya muchana; na watu wakasikiliza kwa uangalifu+ kitabu cha Sheria.
4 Na Ezra mwandikaji* alikuwa amesimama juu ya jukwaa la mbao lenye lilitengenezwa kwa ajili ya tukio hilo; na Matitia, Shema, Anaya, Uria, Hilkia, na Maaseya walisimama pembeni yake kwenye upande wake wa kuume; na Pedaya, Mishaeli, Malkiya,+ Hashumu, Hash-badana, Zekaria, na Meshulamu kwenye upande wake wa kushoto.
5 Ezra akafungua kitabu mbele ya macho ya watu wote, kwa maana alikuwa mwenye kusimama juu kuliko watu wote. Wakati alifungua kitabu hicho, watu wote wakasimama.
6 Kisha Ezra akamusifu Yehova Mungu wa kweli, mwenye ni Mukubwa, kisha watu wote wakajibu, “Amina!* Amina!”+ nao wakainua mikono yao juu. Kisha wakainama na kushusha nyuso chini mbele ya Yehova.
7 Na Yeshua, Bani, Sherebia,+ Yamini, Akubu, Shabetai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi,+ Hanani, na Pelaya, wenye walikuwa Walawi, walikuwa wanafasiria watu Sheria,+ wakati watu walikuwa wamesimama.
8 Na wakaendelea kusoma kwa sauti kubwa katika kile kitabu, katika Sheria ya Mungu wa kweli, wakaifasiria waziwazi na kueleza maana yake; kwa hiyo wakasaidia watu kuelewa mambo yenye yalikuwa yanasomwa.*+
9 Na Nehemia, mwenye alikuwa gavana* wakati huo, Ezra+ kuhani na mwandikaji,* na Walawi wenye walikuwa wanafundisha watu wakaambia watu wote: “Siku hii ni takatifu kwa Yehova Mungu wenu.+ Musiomboleze wala kulia.” Kwa maana watu wote walikuwa wanalia wakati walikuwa wanasikia maneno ya Sheria.
10 Akawaambia: “Muende, mukule vitu vya muzuri* na kunywa vitu vitamu, na mutume mafungu ya chakula+ kwa wale wenye hawana kitu; kwa kuwa siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu, musihuzunike, kwa maana shangwe ya Yehova ni ngome yenu.”*
11 Na Walawi walikuwa wanatuliza watu wote, kwa kusema: “Munyamaze! kwa maana siku hii ni siku takatifu; wala musihuzunike.”
12 Kwa hiyo watu wote wakaenda kula na kunywa na kutumia wengine mafungu ya chakula na kushangilia sana,+ kwa maana walielewa maneno yenye walikuwa wamejulishwa.+
13 Na siku ya pili, vichwa vya jamaa za upande wa baba za watu wote, makuhani, na Walawi wakakusanyika kumuzunguka Ezra mwandikaji* ili wapate kuelewa zaidi maneno ya Sheria.
14 Kisha wakavumbua kwamba ilikuwa imeandikwa katika Sheria kwamba Yehova alikuwa ameamuru kupitia Musa kwamba Waisraeli walipaswa kukaa katika vibanda* wakati wa sikukuu katika mwezi wa saba (7),+
15 na kwamba walipaswa kutangaza+ na kujulisha katika miji yao yote na Yerusalemu yote, na kusema: “Muende katika eneo lenye milima na mulete matawi ya mizeituni, ya miti ya misonobari, ya miti ya mihadasi na ya miti ya mitende, na matawi ya miti ingine ili kujenga vibanda, kama vile imeandikwa.”
16 Kwa hiyo watu wakaenda na kuleta matawi ili kujijengea vibanda, kila mutu kwenye sehemu ya juu ya nyumba yake, na pia katika viwanja vyao, na katika viwanja vya nyumba ya Mungu wa kweli,+ na katika kiwanja cha watu wote cha Mulango Mukubwa wa Maji,+ na katika kiwanja cha watu wote cha Mulango Mukubwa wa Efraimu.+
17 Basi kutaniko lote la wale wenye walikuwa wamerudia kutoka katika utekwa wakajenga vibanda na kukaa katika vibanda hivyo; kwa maana Waisraeli walikuwa hawajafanya vile tangu siku za Yoshua+ mwana wa Nuni mupaka siku hiyo, kwa hiyo kukakuwa furaha kubwa sana.+
18 Na kitabu cha Sheria ya Mungu wa kweli kikasomwa kila siku,+ tangu siku ya kwanza mupaka siku ya mwisho. Na wakafanya sikukuu hiyo kwa siku saba (7), na kukakuwa mukusanyiko mukubwa siku ya munane (8), kama vile iliombwa.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “mwandishi.”
^ Ao “mwandishi.”
^ Ao “Ikuwe vile!”
^ Ao “wakaeleza maana ya usomaji huo.”
^ Ao “mwandishi.”
^ Ao “Tirshata,” jina la cheo cha Kiajemi cha gavana wa jimbo.
^ Tnn., “vitu vinono.”
^ Ao “nguvu yenu.”
^ Ao “mwandishi.”
^ Ao “makao ya muda.”