Nehemia 10:1-39
10 Wale wenye walishuhudia kwa kutia muhuri juu ya mapatano hayo+ walikuwa:
Nehemia gavana,* mwana wa Hakalia,
Na Sedekia,
2 Seraya, Azaria, Yeremia,
3 Pashuri, Amaria, Malkiya,
4 Hatushi, Shebania, Maluku,
5 Harimu,+ Meremoti, Obadia,
6 Danieli,+ Ginetoni, Baruku,
7 Meshulamu, Abiya, Miyamini,
8 Maazia, Bilgai, na Shemaya; hao walikuwa makuhani.
9 Pia Walawi: Yeshua mwana wa Azania, Binui wa wana wa Henadadi, Kadmieli,+
10 na ndugu zao Shebania, Hodia, Kelita, Pelaya, Hanani,
11 Mika, Rehobu, Hashabia,
12 Zakuri, Sherebia,+ Shebania,
13 Hodia, Bani, na Beninu.
14 Vichwa vya watu: Paroshi, Pahat-moabu,+ Elamu, Zatu, Bani,
15 Buni, Azgadi, Bebai,
16 Adoniya, Bigvai, Adini,
17 Ateri, Hezekia, Azuri,
18 Hodia, Hashumu, Besai,
19 Harifu, Anatoti, Nebai,
20 Magpiashi, Meshulamu, Heziri,
21 Meshezabeli, Sadoki, Yadua,
22 Pelatia, Hanani, Anaya,
23 Hoshea, Hanania, Hashubu,
24 Haloheshi, Pilha, Shobeki,
25 Rehumu, Hashabna, Maaseya,
26 Ahiya, Hanani, Anani,
27 Maluku, Harimu, na Baana.
28 Watu wengine—makuhani, Walawi, walinzi wa milango mikubwa, waimbaji, watumishi wa hekalu,* na watu wote wenye walijitenga na watu wa inchi hizo ili wafuate Sheria ya Mungu wa kweli,+ pamoja na bibi zao, watoto wao wanaume, na watoto wao wanamuke, wale wote wenye ujuzi na uelewaji*—
29 wakajiunga na ndugu zao, watu wao wa maana, wakajifunga kwa laana na kiapo, ili kutembea katika Sheria ya Mungu wa kweli, yenye ilikuwa imetolewa kupitia Musa mutumishi wa Mungu wa kweli, na kufuata kwa uangalifu amri zote za Yehova Bwana wetu, hukumu zake, na masharti yake.
30 Hatutapatia watu wa inchi watoto wetu wanamuke, na hatutachukua watoto wao wanamuke kwa ajili ya watoto wetu wanaume.+
31 Kama watu wa inchi wanaleta vitu vyao na kila namna ya nafaka ili kuuzisha siku ya Sabato, hatutanunua kitu chao chochote siku ya Sabato+ ao siku takatifu.+ Pia, tutaachilia mazao ya mwaka wa saba (7)+ na hatutalipisha kila deni lenye halijalipwa.+
32 Pia, tuliweka amri juu yetu wenyewe kwamba kila mumoja wetu anapaswa kutoa sehemu moja ya tatu (1/3) ya shekeli* kila mwaka kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya* Mungu wetu,+
33 na kwa ajili ya mikate yenye kupangwa moja juu ya ingine,*+ toleo la nafaka lenye linatolewa kwa ukawaida,+ toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida la Sabato mbalimbali+ na miezi mipya,+ na kwa ajili ya sikukuu zenye kuwekwa,+ kwa ajili ya vitu vitakatifu, kwa ajili ya matoleo ya zambi+ ili kufunika zambi kwa ajili ya Israeli, na kwa ajili ya kazi zote za nyumba ya Mungu wetu.
34 Pia, tulipiga kura kuhusu kiasi cha kuni zenye makuhani, Walawi na watu walipaswa kuleta kwenye nyumba ya Mungu kulingana na jamaa zetu za upande wa baba, kwa nyakati zenye kuwekwa, mwaka kwa mwaka, ili kuwasha moto kwenye mazabahu ya Yehova Mungu wetu, kulingana na mambo yenye kuandikwa katika Sheria.+
35 Pia, tutaleta matunda ya kwanza yenye kukomaa ya mashamba yetu na matunda ya kwanza yenye kuivya ya kila aina ya muti wa matunda, mwaka kwa mwaka, kwenye nyumba ya Yehova,+
36 na pia muzaliwa wa kwanza wa wana wetu na wa mifugo yetu+—kulingana na mambo yenye kuandikwa katika Sheria—na muzaliwa wa kwanza wa mifugo yetu na makundi yetu. Tutawaleta kwenye nyumba ya Mungu wetu, kwa makuhani wenye wanatumikia kwenye nyumba ya Mungu wetu.+
37 Pia, matunda ya kwanza ya unga wetu wa chenga-chenga,+ michango yetu, matunda ya kila aina ya muti,+ divai mupya, na mafuta,+ tunapaswa kupelekea makuhani kwenye madepo ya* nyumba ya Mungu wetu,+ na kupelekea Walawi sehemu moja ya kumi (1/10)*+ ya mazao ya mashamba yetu, kwa maana wao ndio wanakusanya sehemu moja za kumi za miji yetu yote ya kilimo.
38 Na kuhani, mwana wa Haruni, anapaswa kuwa pamoja na Walawi wakati Walawi wanakusanya sehemu moja ya kumi (1/10); na Walawi wanapaswa kutoa sehemu moja ya kumi ya ile sehemu moja ya kumi kwa nyumba ya Mungu wetu,+ kwenye vyumba* vya depo.
39 Kwa maana Waisraeli na wana wa Walawi wanapaswa kuleta muchango+ wa nafaka, divai mupya, na mafuta+ kwenye madepo,* ni pale vyombo vya patakatifu vinapatikana, na pia makuhani wenye kutumikia, walinzi wa milango mikubwa, na waimbaji. Hatutapuuza nyumba ya Mungu wetu.”+
Maelezo ya Chini
^ Ao “Tirshata,” jina la cheo cha Kiajemi cha gavana wa jimbo.
^ Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
^ Ao pengine, “wote wenye miaka ya kuelewa.”
^ Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
^ Ao “hekalu la.”
^ Ni kusema, mikate ya wonyesho.
^ Ao “vyumba vya kukulia chakula vya.”
^ Ao “zaka.”
^ Ao “vyumba vya kukulia chakula.”
^ Ao “vyumba vya kukulia chakula.”