Nehemia 3:1-32

  • Kuta zinajengwa upya (1-32)

3  Eliashibu+ kuhani mukubwa na ndugu zake makuhani wakasimama na kuanza kujenga Mulango Mukubwa wa Kondoo.+ Wakautakasa*+ na kuweka milango yake; wakautakasa mupaka kwenye Munara wa Mea,+ mupaka kwenye Munara wa Hananeli.+  Na karibu nao watu wa Yeriko+ walikuwa wanajenga; na karibu nao Zakuri mwana wa Imri alikuwa anajenga.  Wana wa Hasenaa wakajenga Mulango Mukubwa wa Samaki;+ wakautengeneza kwa mbao+ na kisha wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo* yake.  Na karibu nao Meremoti+ mwana wa Uriya mwana wa Hakozi akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, na karibu nao Meshulamu+ mwana wa Berekia mwana wa Meshezabeli akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, na karibu nao Sadoki mwana wa Baana akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika.  Na karibu nao Watekoa+ wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, lakini watu wao wa maana hawakutaka kujishusha ili kushiriki katika* kazi za mabwana wao.  Yoyada mwana wa Pasea na Meshulamu mwana wa Besodeya wakatengeneza Mulango Mukubwa wa Muji wa Zamani+ wenye ulikuwa umeharibika, wakautengeneza kwa mbao, wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo* yake.  Karibu nao Melatia Mugibeoni+ na Yadoni Mumeronoti wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, watu wa Gibeoni na Mispa,+ wenye walikuwa chini ya mamlaka ya* gavana wa eneo la Ngambo ya ule Muto.*+  Karibu nao Uzieli mwana wa Harhaya, mumoja wa mafundi wa zahabu, akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, na karibu naye Hanania, mumoja wa watu wenye kuchanganya mafuta yenye marashi;* wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika; wakatandika majiwe Yerusalemu mupaka kwenye Ukuta Mupana.+  Na karibu nao Refaya mwana wa Huru, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika. 10  Na karibu nao Yedaya mwana wa Harumafu akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika mbele ya nyumba yake mwenyewe, na karibu naye Hatushi mwana wa Hashabneya akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika. 11  Malkiya mwana wa Harimu+ na Hashubu mwana wa Pahat-moabu+ wakatengeneza sehemu ingine yenye kuharibika,* na vilevile Munara wa Majiko.+ 12  Na karibu nao Shalumu mwana wa Haloheshi, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, pamoja na mabinti wake. 13  Hanuni na wakaaji wa Zanoa+ wakatengeneza Mulango Mukubwa wa Bonde+ wenye ulikuwa umeharibika; wakaujenga na kisha wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo* yake, na wakatengeneza sehemu ya ukuta yenye urefu wa mikono* elfu moja (1 000) mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Marundo ya Majivu.+ 14  Malkiya mwana wa Rekabu, mukubwa wa wilaya ya Bet-hakeremu+ alitengeneza Mulango Mukubwa wa Marundo ya Majivu wenye ulikuwa umeharibika; aliujenga na kuweka milango yake, makomeo yake, na mapingo* yake. 15  Shaluni mwana wa Kolhoze, mukubwa wa wilaya ya Mispa,+ alitengeneza Mulango Mukubwa wa Chemchemi+ wenye ulikuwa umeharibika; aliujenga na pia sehemu yake ya juu, akaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo* yake, na pia akatengeneza ukuta wenye ulikuwa umeharibika wa Kiziwa cha Maji+ cha Mufereji wenye unaelekea kwenye Bustani ya Mufalme+ mupaka kwenye Ngazi+ yenye kushuka kutoka kwenye Muji wa Daudi.+ 16  Kisha yeye, Nehemia mwana wa Azbuki, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Bet-suri,+ akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika kuanzia mbele ya Makaburi ya Daudi+ mupaka kwenye kiziwa cha maji+ chenye kilikuwa kimetengenezwa na mupaka kwenye Nyumba ya Wenye Nguvu. 17  Kisha yeye, Walawi wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika: Rehumu mwana wa Bani; na karibu naye Hashabia, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Keila,+ akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika kwa ajili ya wilaya yake. 18  Kisha yeye, ndugu zao wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika: Bavai mwana wa Henadadi, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Keila. 19  Na karibu naye, Ezeri mwana wa Yeshua,+ mukubwa wa Mispa, alikuwa anatengeneza sehemu ingine yenye kuharibika mbele ya mupando wenye kuenda kwenye Depo ya Silaha karibu na Nguzo.+ 20  Kisha yeye, Baruku mwana wa Zabai+ akafanya kazi kwa bidii na akatengeneza sehemu ingine yenye ilikuwa imeharibika, kuanzia kwenye Nguzo mupaka muingilio wa nyumba ya Eliashibu,+ kuhani mukubwa. 21  Kisha yeye, Meremoti+ mwana wa Uriya mwana wa Hakozi akatengeneza sehemu ingine yenye ilikuwa imeharibika, kuanzia muingilio wa nyumba ya Eliashibu mupaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu. 22  Na kisha yeye, makuhani, wanaume wa Wilaya ya Yordani,*+ wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika. 23  Kisha wao, Benyamini na Hashubu wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika mbele ya nyumba yao wenyewe. Na kisha wao, Azaria mwana wa Maaseya mwana wa Ananiya akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika karibu na nyumba yake mwenyewe. 24  Kisha yeye, Binui mwana wa Henadadi akatengeneza sehemu ingine yenye ilikuwa imeharibika, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mupaka kwenye Nguzo+ na mupaka kwenye pembe. 25  Kisha yeye, Palali mwana wa Uzai akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika mbele ya Nguzo na munara wenye unaanzia kwenye Nyumba ya Mufalme,+ ule wa juu wenye kuwa kwenye Kiwanja cha Walinzi.+ Kisha yeye, kulikuwa Pedaya mwana wa Paroshi.+ 26  Na watumishi wa hekalu*+ wenye waliishi Ofeli+ wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika mupaka mbele ya Mulango Mukubwa wa Maji+ upande wa mashariki na munara wenye kutokea inje. 27  Kisha wao, Watekoa+ walitengeneza sehemu ingine yenye ilikuwa imeharibika, kuanzia mbele ya ule munara mukubwa wenye kutokea inje mupaka kwenye ukuta wa Ofeli. 28  Makuhani wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika juu ya Mulango Mukubwa wa Farasi,+ kila mumoja mbele ya nyumba yake mwenyewe. 29  Kisha wao, Sadoki+ mwana wa Imeri akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika mbele ya nyumba yake mwenyewe. Na kisha yeye, Shemaya mwana wa Shekania, mulinzi wa Mulango Mukubwa wa Mashariki,+ akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika. 30  Kisha yeye, Hanania mwana wa Shelemia na Hanuni mwana wa sita (6) wa Zalafu wakatengeneza sehemu ingine yenye ilikuwa imeharibika. Na kisha yeye, Meshulamu+ mwana wa Berekia akafanya kazi ya kutengeneza sehemu yenye ilikuwa imeharibika mbele ya jumba lake mwenyewe. 31  Kisha yeye, Malkiya, mushiriki wa chama cha mafundi wa zahabu akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika mupaka kwenye nyumba ya watumishi wa hekalu*+ na wafanyabiashara, mbele ya Mulango Mukubwa wa Uchunguzi mupaka kwenye chumba cha juu cha pembe. 32  Na kati ya chumba cha juu cha pembe na Mulango Mukubwa wa Kondoo,+ mafundi wa zahabu na wafanyabiashara walifanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika.

Maelezo ya Chini

Ao “Wakautolea Mungu.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Tnn., “hawakutia shingo zao katika.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Tnn., “wa kiti cha ufalme cha.”
Ao “Eneo la Ngambo Ingine ya Efrati.”
Ao “watengenezaji wa marashi.”
Ao “sehemu ingine yenye kupimwa.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Karibu metre 445 (futi 1460).
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Ao pengine, “wilaya ya pembeni-pembeni.”
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”