Nehemia 4:1-23

  • Kazi inaendelea ijapokuwa upinzani (1-14)

  • Kazi ya kujenga inaendelea kufanywa na wajenzi wenye kuwa na silaha (15-23)

4  Sasa wakati tu Sanbalati+ alisikia kwamba tulikuwa tunajenga upya ukuta, akakasirika na kuwa na uchungu sana,* na akaendelea kuchekelea Wayahudi.  Na akasema mbele ya ndugu zake na jeshi la Samaria: “Wayahudi hawa wazaifu wako wanafanya nini? Je, watafanya jambo hili wao wenyewe? Je, watatoa zabihu? Je, watamaliza kwa siku moja? Je, watafanya majiwe yenye yalichomwa na moto na yenye kuwa katika marundo ya mabomoko yenye kuwa na vumbi yakuwe na uzima?”+  Sasa Tobia+ Mwamoni,+ mwenye alikuwa anasimama pembeni yake, akasema: “Hata mbweha akipanda juu ya kile chenye wako wanajenga, atabomoa ukuta wao wa majiwe.”  Sikia, Ee Mungu wetu, kwa maana tumezarauliwa;+ na urudishe haya yao juu ya vichwa vyao wenyewe,+ na uwatoe kuwa kitu cha kunyanganywa katika inchi ya utekwa.  Na usifunike hatia yao wala kuruhusu zambi yao ifutwe mbele yako,+ kwa sababu wametukana wajenzi.”  Kwa hiyo tukaendelea kujenga ukuta, na ukuta wote ukaunganishwa pamoja na kujengwa kufikia nusu ya urefu wake kuenda juu, na watu wakaendelea kufanya kazi kwa moyo wao wote.  Sasa wakati tu Sanbalati, Tobia,+ Waarabu,+ Waamoni, na Waashdodi+ walisikia kwamba kazi ya kutengeneza kuta za Yerusalemu zenye zilikuwa zimeharibika inaendelea na kwamba matundu yalikuwa yanaendelea kufunikwa, wakakasirika sana.  Wakafanya shauri pamoja ili kuja na kushambulia Yerusalemu na kuleta fujo ndani yake.  Lakini tulisali kwa Mungu wetu na kuweka walinzi muchana na usiku kwa sababu yao. 10  Lakini, watu wa Yuda walikuwa wanasema: “Nguvu za wafanyakazi* zimeisha, na kuko mabomoko mengi sana; hatutaweza kujenga ukuta hata kidogo.” 11  Na maadui wetu waliendelea kusema: “Mbele wajue jambo hilo ao kutuona, tutaingia kati yao na kuwaua na kusimamisha ile kazi.” 12  Kila mara wakati Wayahudi wenye waliishi karibu nao waliingia, walikuwa wanatuambia mara kwa mara:* “Watatushambulia kutoka kila upande.” 13  Kwa hiyo nilipanga wanaume kwenye sehemu za chini zenye kuwa wazi nyuma ya ukuta, na niliwapanga kulingana na familia zao, walikuwa na panga zao, mikuki yao, na pinde zao. 14  Wakati niliona kwamba wameogopa, mara moja nikasimama na kuambia watu wenye vyeo+ na watawala-wasaidizi na watu wengine wote: “Musiwaogope.+ Mumukumbuke Yehova, yeye ni mukubwa na mwenye kuogopesha sana;+ na mupigane kwa ajili ya ndugu zenu, watoto wenu wanaume na watoto wenu wanamuke, bibi zenu na nyumba zenu.” 15  Sasa wakati maadui wetu walisikia kwamba tumejua mambo yenye walikuwa wanafanya na kwamba Mungu wa kweli alikuwa amevunja mipango yao, sisi wote tukarudia kufanya kazi ya kujenga ukuta. 16  Kuanzia siku hiyo, nusu ya wanaume wangu walikuwa wanafanya kazi+ na nusu ingine walikuwa wanashika mikuki, ngao, pinde na makoti ya chuma. Na wakubwa+ walisimama nyuma ya watu wa nyumba yote ya Yuda 17  wenye walikuwa wanajenga ukuta. Wale wenye walikuwa wanabeba mizigo walifanya kazi kwa mukono mumoja na mukono mwingine ulikuwa unakamata silaha. 18  Na kila mujenzi alikuwa amejifunga upanga kwenye kiuno wakati alikuwa anajenga, na mupiga-baragumu+ alikuwa amesimama pembeni yangu. 19  Kisha niliambia watu wenye vyeo na watawala-wasaidizi na watu wengine wote: “Kazi hii ni kubwa na imeenea sehemu kubwa, na sisi tumesambazwa kwenye ukuta kila mumoja mbali na mwenzake. 20  Wakati mutasikia sauti ya baragumu, mujikusanye pamoja mahali kwenye tuko. Mungu wetu atatupigania.”+ 21  Kwa hiyo tuliendelea kufanya kazi na wakati huo nusu ya wanaume walikuwa wamekamata mikuki, kuanzia wakati kulipambazuka* mupaka wakati nyota zilitokea. 22  Wakati huo niliambia watu: “Wanaume wakae katikati ya Yerusalemu usiku, kila mwanaume na mutumishi wake, na watatulinda usiku na kufanya kazi muchana.” 23  Lakini mimi, ndugu zangu, watumishi wangu,+ na walinzi wenye walinifuata hatukuvua nguo zetu, na kila mumoja wetu aliendelea kukamata silaha yake kwa mukono wa kuume.

Maelezo ya Chini

Ao “akauzika.”
Ao “wabeba-mizigo.”
Tnn., “mara kumi.”
Ni kusema, wakati mwangaza wa jua ulianza kutokea.