Nehemia 11:1-36
-
Watu wanaanza kuishi tena Yerusalemu (1-36)
11 Sasa wakubwa wa watu walikuwa wanaishi Yerusalemu;+ lakini watu wengine walipiga kura+ ili kuleta mutu mumoja kati ya watu kumi (10) aishi Yerusalemu, ule muji mutakatifu, wakati huo wale wengine kenda (9) walibakia katika miji ingine.
2 Zaidi ya hilo, watu walibariki watu wote wenye walijitolea ili kuishi Yerusalemu.
3 Na hawa ndio vichwa vya jimbo* wenye waliishi Yerusalemu. (Israeli wengine, makuhani, Walawi, watumishi wa hekalu,*+ na wana wa watumishi wa Sulemani,+ waliishi katika miji ingine ya Yuda, kila mumoja katika uriti wake mwenyewe katika muji wake.+
4 Pia, wamoja kati ya watu wa Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu.) Kati ya watu wa Yuda kulikuwa Ataya mwana wa Uzia mwana wa Zekaria mwana wa Amaria mwana wa Shefatia mwana wa Mahalaleli wa wana wa Perezi;+
5 na Maaseya mwana wa Baruku mwana wa Kolhoze mwana wa Hazaya mwana wa Adaya mwana wa Yoyaribu mwana wa Zekaria mwana wa Mushela.
6 Wana wote wa Perezi wenye walikuwa wanaishi Yerusalemu walikuwa wanaume mia ine makumi sita na munane (468) wenye uwezo.
7 Na hawa ndio walikuwa watu wa Benyamini: Salu+ mwana wa Meshulamu mwana wa Yoedi mwana wa Pedaya mwana wa Kolaya mwana wa Maaseya mwana wa Itieli mwana wa Yeshaya;
8 na kisha yeye Gabai na Salai, watu mia kenda makumi mbili na munane (928);
9 na Yoeli mwana wa Zikri, alikuwa musimamizi wao, na Yuda mwana wa Hasenua alikuwa wa pili katika kusimamia muji.
10 Kati ya makuhani: Yedaya mwana wa Yoyaribu, Yakini,+
11 Seraya mwana wa Hilkia mwana wa Meshulamu mwana wa Sadoki mwana wa Merayoti mwana wa Ahitubu,+ kiongozi wa nyumba ya* Mungu wa kweli;
12 na ndugu zao wenye walifanya kazi ya ile nyumba, watu mia munane makumi mbili na mbili (822); na Adaya mwana wa Yerohamu mwana wa Pelalia mwana wa Amzi mwana wa Zekaria mwana wa Pashuri+ mwana wa Malkiya,
13 na ndugu zake, vichwa vya jamaa za upande wa baba, watu mia mbili makumi ine na mbili (242), na Amashisai mwana wa Azareli mwana wa Azai mwana wa Meshilemoti mwana wa Imeri,
14 na ndugu zao wenye walikuwa wanaume wenye nguvu, na hodari, watu mia moja makumi mbili na munane (128), na musimamizi wao alikuwa Zabdieli, mutu wa familia ya watu wa maana.
15 Na kati ya Walawi: Shemaya+ mwana wa Hashubu mwana wa Azrikamu mwana wa Hashabia mwana wa Buni,
16 na Shabetai+ na Yozabadi,+ wa vichwa vya Walawi, wenye walisimamia kazi za inje ya nyumba ya Mungu wa kweli;
17 na Matania,+ mwana wa Mika mwana wa Zabdi mwana wa Asafu,+ kiongozi wa nyimbo, mwenye aliongoza nyimbo za sifa wakati wa sala,+ na Bakbukia, wa pili kati ya ndugu zake, na Abda mwana wa Shamua mwana wa Galali mwana wa Yedutuni.+
18 Walawi wote katika muji mutakatifu walikuwa mia mbili makumi munane na ine (284).
19 Na walinzi wa milango mikubwa walikuwa Akubu, Talmoni,+ na ndugu zao wenye walikuwa wanalinda milango mikubwa, watu mia moja makumi saba na mbili (172).
20 Israeli wengine, makuhani, na Walawi wenye walikuwa katika miji ingine yote ya Yuda, kila mutu katika sehemu yake ya uriti.*
21 Watumishi wa hekalu*+ walikuwa wanaishi Ofeli,+ na Siha na Gishpa walisimamia watumishi wa hekalu.*
22 Na musimamizi wa Walawi katika Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani mwana wa Hashabia mwana wa Matania+ mwana wa Mika, wa wana wa Asafu, waimbaji; alisimamia kazi ya nyumba ya Mungu wa kweli.
23 Kwa maana mufalme alikuwa ametoa amri kwa ajili yao,+ na kulikuwa mupango fulani kwa ajili ya mahitaji ya kila siku ya waimbaji.
24 Na Petahia mwana wa Meshezabeli wa wana wa Zera mwana wa Yuda alikuwa mushauri* wa mufalme kwa kila jambo lenye lilihusu watu.
25 Kuhusu makao katika maeneo yao ya mashamba, wamoja kati ya watu wa Yuda waliishi Kiriat-arba,+ na miji yake ya pembeni-pembeni,* Diboni na miji yake ya pembeni-pembeni, Yekabzeeli+ na makao yake.
26 katika Yeshua, katika Molada,+ katika Bet-peleti+
27 katika Hasar-shuali,+ katika Beer-sheba na miji yake ya pembeni-pembeni,*
28 katika Siklagi,+ katika Mekona na miji yake ya pembeni-pembeni,*
29 katika En-rimoni,+ katika Sora,+ na katika Yarmuti,
30 katika Zanoa,+ katika Adulamu na makao yake, katika Lakishi+ na maeneo yake ya mashamba, na katika Azeka+ na miji yake ya pembeni-pembeni.* Wakaishi* kuanzia Beer-sheba mupaka Bonde la Hinomu.+
31 Na watu wa kabila la Benyamini waliishi Geba,+ Mikmashi, Aiya, Beteli+ na miji yake ya pembeni-pembeni,*
32 Anatoti,+ Nobu,+ Ananiya,
33 Hasori, Rama,+ Gitaimu,
34 Hadidi, Seboimu, Nebalati,
35 Lodi, na Ono,+ bonde la mafundi.
36 Na vikundi fulani vya Walawi kutoka Yuda viliombwa kuishi katika eneo la Benyamini.
Maelezo ya Chini
^ Ao “wilaya ya utawala.”
^ Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
^ Ao “hekalu la.”
^ Ao “uriti wake mwenyewe.”
^ Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
^ Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
^ Tnn., “alikuwa kwenye mukono wa mufalme.”
^ Ao “yenye kuizunguka.”
^ Ao “yenye kuizunguka.”
^ Ao “yenye kuizunguka.”
^ Ao “yenye kuizunguka.”
^ Ao “Wakapiga kambi.”
^ Ao “yenye kuizunguka.”