Nehemia 12:1-47

  • Makuhani na Walawi (1-26)

  • Kuzindua kuta (27-43)

  • Kutegemeza utumishi wa hekalu (44-47)

12  Hawa ndio makuhani na Walawi wenye walipanda pamoja na Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli+ na Yeshua:+ Seraya, Yeremia, Ezra,  Amaria, Maluku, Hatushi,  Shekania, Rehumu, Meremoti,  Ido, Ginetoi, Abiya,  Miyamini, Maadia, Bilga,  Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,  Salu, Amoki, Hilkia, na Yedaya. Hao ndio walikuwa vichwa vya makuhani na ndugu zao katika siku za Yeshua.  Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli,+ Sherebia, Yuda, na Matania,+ mwenye aliongoza nyimbo za shukrani pamoja na ndugu zake.  Na Bakbukia na Uni ndugu zao walisimama kwa kuangaliana nao ili kufanya kazi za ulinzi.* 10  Yeshua akamuzaa Yoyakimu, Yoyakimu akamuzaa Eliashibu,+ Eliashibu akamuzaa Yoyada,+ 11  Yoyada akamuzaa Yonatani, naye Yonatani akamuzaa Yadua. 12  Katika siku za Yoyakimu, hawa walikuwa makuhani, vichwa vya jamaa za upande wa baba: kwa ajili ya Seraya,+ Meraya; kwa ajili ya Yeremia, Hanania; 13  kwa ajili ya Ezra,+ Meshulamu; kwa ajili ya Amaria, Yehohanani; 14  kwa ajili ya Maluki, Yonatani; kwa ajili ya Shebania, Yosefu; 15  kwa ajili ya Harimu,+ Adna; kwa ajili ya Merayoti, Helkai; 16  kwa ajili ya Ido, Zekaria; kwa ajili ya Ginetoni, Meshulamu; 17  kwa ajili ya Abiya,+ Zikri; kwa ajili ya Miniamini, . . . ;* kwa ajili ya Moadia, Piltai; 18  kwa ajili ya Bilga,+ Shamua; kwa ajili ya Shemaya, Yehonatani; 19  kwa ajili ya Yoyaribu, Matenai; kwa ajili ya Yedaya,+ Uzi; 20  kwa ajili ya Salai, Kalai; kwa ajili ya Amoki, Eberi; 21  kwa ajili ya Hilkia, Hashabia; kwa ajili ya Yedaya, Netaneli. 22  Vichwa vya jamaa za upande wa baba za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani, na Yadua+ waliandikishwa, sawasawa na makuhani, mupaka wakati wa ufalme wa Dario Mwajemi. 23  Walawi wenye walikuwa vichwa vya jamaa za upande wa baba waliandikishwa katika kitabu cha historia za nyakati hizo, mupaka siku za Yohanani mwana wa Eliashibu. 24  Vichwa vya Walawi walikuwa Hashabia, Sherebia, na Yeshua+ mwana wa Kadmieli,+ na ndugu zao walisimama kwa kuangaliana nao ili kutoa sifa na shukrani kulingana na maagizo ya Daudi+ mutu wa Mungu wa kweli, kikundi cha ulinzi kwa kikundi cha ulinzi. 25  Matania,+ Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni, na Akubu+ walikuwa walinzi wa milango mikubwa,+ walilinda madepo karibu na milango mikubwa. 26  Hao walitumika katika siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua+ mwana wa Yozadaki na katika siku za Nehemia gavana na Ezra+ mwenye alikuwa kuhani na mwandikaji.* 27  Wakati wa kuzindua kuta za Yerusalemu, walitafuta Walawi na kuwatosha kila mahali kwenye waliishi ili kuwaleta Yerusalemu kusudi wazindue kwa kushangilia, kwa nyimbo za shukrani,+ na kwa matoazi, vyombo vya kamba, na vinubi. 28  Na wana wa waimbaji* walikusanyika kutoka katika Wilaya,* kutoka sehemu zote zenye zilizunguka Yerusalemu pande zote, na makao ya Wanetofa,+ 29  kutoka Bet-gilgali,+ na kutoka katika maeneo ya mashamba ya Geba+ na Azmaveti,+ kwa maana waimbaji walikuwa wamejijengea makao kuzunguka Yerusalemu pande zote. 30  Na makuhani na Walawi walijitakasa, na walitakasa watu,+ milango mikubwa,+ na ukuta.+ 31  Kisha nilipandisha wakubwa wa Yuda kwenye sehemu ya juu ya ukuta. Tena, nikatia vikundi mbili vikubwa vya waimbaji wa kutoa shukrani na vikundi vya kuwafuata, na kikundi kimoja kilitembea kuelekea upande wa kuume juu ya ukuta, kuelekea kwenye Mulango Mukubwa wa Marundo ya Majivu.+ 32  Hoshaya na nusu ya wakubwa wa Yuda walitembea nyuma yao, 33  pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu, 34  Yuda, Benyamini, Shemaya, na Yeremia. 35  Walikuwa pamoja na wamoja kati ya wana wa makuhani wenye walikuwa na tarumbeta:+ Zekaria mwana wa Yonatani mwana wa Shemaya mwana wa Matania mwana wa Mikaya mwana wa Zakuri mwana wa Asafu,+ 36  na ndugu zake Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Netaneli, Yuda, na Hanani, walikuwa na vyombo vya muziki vya Daudi+ ule mutu wa Mungu wa kweli; na Ezra+ mwandikaji* aliwatangulia. 37  Kwenye Mulango Mukubwa wa Chemchemi+ walienda moja kwa moja mbele yao, wakapanda Ngazi+ ya Muji wa Daudi+ kupitia njia yenye kupanda kwenye ukuta, juu ya Nyumba ya Daudi na mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Maji,+ upande wa mashariki. 38  Kikundi cha pili cha waimbaji wa kutoa shukrani kilitembea kuelekea upande mwingine,* na mimi nilikifuata pamoja na nusu ya watu, kwenye ukuta, juu ya Munara wa Majiko,+ na mupaka kwenye Ukuta Mupana,+ 39  na juu ya Mulango Mukubwa wa Efraimu,+ na mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Muji wa Zamani,+ na mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Samaki,+ Munara wa Hananeli,+ Munara wa Mea, na mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Kondoo;+ na wakakuja kusimama kwenye Mulango Mukubwa wa Mulinzi. 40  Mwishowe vikundi hivyo mbili vya waimbaji wa kutoa shukrani vikasimama mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli; na mimi pia nikafanya vile na nusu ya watawala-wasaidizi wenye walikuwa pamoja na mimi, 41  na makuhani Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria, na Hanania, wenye walikuwa na tarumbeta, 42  na Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu, na Ezeri. Na waimbaji wakaimba kwa sauti kubwa na Izrahia alikuwa musimamizi wao. 43  Siku hiyo walitoa zabihu nyingi na kushangilia,+ kwa maana Mungu wa kweli aliwafanya wafurahi sana. Wanamuke na watoto pia walishangilia,+ mupaka sauti za kushangilia za Yerusalemu zikasikika mbali sana.+ 44  Siku hiyo wanaume waliwekwa ili kusimamia madepo+ ya michango,+ matunda ya kwanza,+ na sehemu moja za kumi (1/10).*+ Kutoka katika maeneo ya mashamba ya miji, walipaswa kukusanya ndani ya madepo hayo sehemu zenye Sheria iliomba+ kwa ajili ya makuhani na Walawi,+ kwa maana kulikuwa furaha nyingi katika Yuda kwa sababu ya makuhani na Walawi wenye walikuwa wanatumikia. 45  Na walianza kutimiza kazi za Mungu wao na sharti la kutakasa, kama vile waimbaji na walinzi wa milango mikubwa walifanya, kulingana na maagizo ya Daudi na Sulemani mwana wake. 46  Kwa maana zamani sana katika siku za Daudi na Asafu, kulikuwa viongozi wa* waimbaji na wa nyimbo za kumusifu na kumushukuru Mungu.+ 47  Na katika siku za Zerubabeli+ na siku za Nehemia, Israeli wote walipatia waimbaji+ na walinzi wa milango mikubwa mafungu yao,+ kulingana na mahitaji yao ya kila siku. Pia, walitia pembeni fungu la Walawi,+ na Walawi nao wakatia pembeni fungu la wazao wa Haruni.

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “wakati wa kazi.”
Inaonekana jina fulani limeondolewa hapa katika maandishi ya Kiebrania.
Ao “mwandishi.”
Ao “Na waimbaji wenye kuzoezwa.”
Ni kusema, wilaya yenye ilizunguka Yordani.
Ao “mwandishi.”
Ao “mbele.”
Ao “zaka.”
Tnn., “vichwa vya.”