Nehemia 1:1-11

  • Habari kutoka Yerusalemu (1-3)

  • Sala ya Nehemia (4-11)

1  Maneno ya Nehemia*+ mwana wa Hakalia: Sasa katika mwezi wa Kislevu,* katika mwaka wa makumi mbili (20), nilikuwa katika ngome* ya Shushani.*+  Wakati huo Hanani,+ mumoja wa ndugu zangu, akakuja pamoja na wanaume wengine kutoka Yuda, na nikawauliza kuhusu Wayahudi wenye walibakia wenye walikuwa wameponyoka utekwa,+ na pia kuhusu Yerusalemu.  Wakajibu: “Wale wenye wamebakia kule katika jimbo* wenye waliponyoka utekwa, wako katika hali ya mubaya sana na yenye kuleta haya.+ Kuta za Yerusalemu zimebomoka,+ na milango yake mikubwa imeteketezwa kwa moto.”+  Wakati tu nilisikia maneno hayo, nikakaa chini na kuanza kulia na kuomboleza kwa siku nyingi, na nikaendelea kufunga+ na kusali mbele ya Mungu wa mbinguni.  Nikasema: “Ee Yehova Mungu wa mbinguni, Mungu mukubwa na mwenye kuogopesha sana, mwenye kushika agano lake na kuonyesha upendo mushikamanifu kwa wale wenye wanamupenda na kushika amri zake,+  tafazali, tega sikio lako na ufungue macho yako ili kusikiliza sala ya mutumishi wako yenye ninakutolea leo, muchana na usiku,+ kuhusu watumishi wako Waisraeli, wakati ninaungama zambi zenye watu wa Israeli wamekutendea. Tumetenda zambi, mimi pamoja na nyumba ya baba yangu.+  Kwa kweli tumekutendea kwa upotovu+ kwa kukosa kushika amri, masharti, na maamuzi ya hukumu yenye ulimupatia Musa mutumishi wako.+  “Tafazali, kumbuka lile neno lenye ulimuamuru* Musa mutumishi wako: ‘Kama hamutakuwa waaminifu, nitawasambaza kati ya vikundi vya watu.+  Lakini mukirudia kwangu na kushika amri zangu na kuzitii, hata kama watu wenu wenye kutawanywa wangekuwa kwenye mwisho wa mbingu, nitawakusanya+ na kuwaleta mahali kwenye nimechagua jina langu likae.’+ 10  Wao ni watumishi wako na watu wako, wenye ulikomboa kwa uwezo wako mukubwa na kwa mukono wako wenye nguvu.+ 11  Ee Yehova, tafazali, tega sikio lako lisikilize sala ya mutumishi wako na sala ya watumishi wako wenye wanafurahia kuogopa jina lako, na tafazali, ufanye mutumishi wako apate matokeo ya muzuri leo, na mwanaume huyu anionyeshe rehema.”+ Wakati huo nilikuwa munyweshaji wa mufalme.+

Maelezo ya Chini

Maana yake “Yah Anafariji.”
Ao “nyumba ya mufalme.”
Ao “Susa.”
Ao “wilaya ya utawala.”
Ao “onyo lenye ulimupatia.”