Hosea 8:1-14
8 “Tia baragumu kwenye kinywa chako!+
Mutu mumoja anakuja kama tai ili kushambulia nyumba ya Yehova,+Kwa maana wamevunja agano langu+ na wamekosea sheria yangu.+
2 Wananililia, ‘Mungu wangu, sisi, Israeli, tunakujua!’+
3 Israeli amekataa mambo ya muzuri.+
Adui amufuatilie.
4 Wameweka wafalme, lakini hapana kupitia mimi.
Wameweka wakubwa, lakini sikuwatambua.
Kwa feza yao na zahabu yao wametengeneza sanamu,+Kwa uharibifu wao wenyewe.+
5 Kitoto-dume chako cha ngombe kimekataliwa, Ee Samaria.+
Kasirani yangu inawaka juu yao.+
Watashindwa kuwa bila kosa* mupaka wakati gani?
6 Kwa maana kitu hiki kimetoka Israeli.
Fundi ndiye alikitengeneza, hapana Mungu;Kitoto-dume cha ngombe wa Samaria kitavunjwa vipande-vipande.
7 Kwa maana ni upepo ndio wanapanda,Na watavuna upepo wa zoruba.+
Hakuna mumea wenye unatokeza nafaka yenye kukomaa;*+Kitu chochote chenye kuota hakitokeze unga.
Kama kitu chochote kinatokezwa, wageni watakimeza.+
8 Israeli atamezwa.+
Sasa watakuwa kati ya mataifa,+Kama chombo chenye hakipendwe.
9 Kwa maana wamepanda kuenda Ashuru,+ kama punda wa pori mwenye kuwa peke yake.
Efraimu amelipa wanamuke ili wakuwe wapenzi wake.+
10 Hata kama wapenzi wenye wao walilipa wametoka kati ya mataifa,Sasa nitawakusanya pamoja;Wataanza kuteseka+ kwa sababu ya muzigo wenye mufalme na wakubwa waliwalazimisha kubeba.
11 Kwa maana Efraimu ameongeza mazabahu ili kutenda zambi.+
Yamekuwa mazabahu yake ili atende zambi.+
12 Nilimuandikia mambo mengi ya sheria yangu,*Lakini yalionwa kama kitu kigeni.+
13 Wananitolea zawadi za zabihu, na wanakula nyama,Lakini Yehova hapendezwe nazo.+
Sasa atakumbuka kosa lao na kuwapatia azabu kwa sababu ya zambi zao.+
Wamerudia* Misri.+
14 Israeli amesahau Mutengenezaji wake+ na amejenga mahekalu,+Na Yuda ameongeza miji yenye ngome.+
Lakini nitatuma moto katika miji yake,Na utateketeza minara ya kila muji.”+

