Hosea 4:1-19
4 Musikie neno la Yehova, ninyi watu wa Israeli,Kwa maana Yehova iko* na mashitaka juu ya wakaaji wa inchi,+Kwa sababu hakuna kweli wala upendo mushikamanifu wala ujuzi wa Mungu katika inchi.+
2 Viapo vya uongo na kudanganya+ na mauaji+Na kuiba na uzinifu+ vimeenea sana,Na tendo moja la kumwanga damu linafuata tendo lingine la kumwanga damu.+
3 Ndiyo sababu inchi itaomboleza+Na kila mukaaji ndani yake ataregea;Wanyama wa pori na ndege wa mbinguni,Hata samaki wa bahari, watakufa.
4 “Lakini, mutu yeyote asishindane wala kukaripia,+Kwa maana watu wako ni kama wale wenye wanashindana na kuhani.+
5 Basi utajikwaa wakati wa muchana,Na nabii atajikwaa pamoja na wewe, kama wakati wa usiku.
Na mimi nitamunyamazisha* mama yako.
6 Watu wangu watanyamazishwa,* kwa sababu hakuna ujuzi.
Kwa sababu umekataa ujuzi,+Mimi pia nitakukataa usinitumikie kama kuhani wangu;Na kwa sababu umesahau sheria ya* Mungu wako,+Mimi mwenyewe nitasahau wana wako.
7 Kadiri walikuwa wanaongezeka, ni vile waliendelea kunitendea zambi.+
Nitabadilisha utukufu wao kuwa haya.*
8 Wanakula zambi ya watu wangu,Na wako na pupa ya* kosa lao.
9 Itakuwa kwa watu kama vile itakuwa kwa kuhani;Nitawaomba watoe hesabu kwa sababu ya njia zao,Na nitaleta juu yao matokeo ya matendo yao.+
10 Watakula lakini hawatashiba.+
Watafanya umalaya,* lakini hawataongezeka,+Kwa sababu hawakumuheshimia Yehova.
11 Ukahaba* na divai na divai mupyaVinaondoa nia ya kufanya mambo yenye kuwa sawa.*+
12 Watu wangu wanatafuta habari kwa sanamu zao za miti,Wanafanya yale fimbo* yao inawaambia;Kwa sababu roho ya ukahaba* inawapoteza,Na kupitia ukahaba* wao wanakataa kujinyenyekeza mbele ya Mungu wao.
13 Wanatoa zabihu kwenye vichwa vya milima,+Na kwenye vilima wanachoma zabihu ili zitoe moshi,Chini ya miti ya mialoni na miti ya milubna na kila muti mukubwa,+Kwa sababu kivuli cha miti hiyo ni kizuri.
Ndiyo sababu mabinti wenu wanafanya ukahaba*Na mabinti-wakwe wenu wanafanya uzinifu.
14 Sitaomba mabinti wenu watoe hesabu kwa sababu ya ukahaba* wao,Na mabinti-wakwe wenu kwa sababu ya uzinifu wao.
Kwa maana wanaume wanajitenga wakiwa na makahabaNa wanatoa zabihu pamoja na makahaba wa hekalu;Watu hao wenye hawana uelewaji+ wataangamia.
15 Hata kama unafanya ukahaba,* Ee Israeli,+Yuda asikuwe na hatia.+
Musikuje Gilgali+ ao Bet-aveni,+Na musiape, ‘Kama vile hakika Yehova anaishi!’+
16 Kwa maana kama vile ngombe mwenye iko* kichwa-nguvu, Israeli amekuwa kichwa-nguvu.+
Je, sasa Yehova atawachunga kama mwana-kondoo dume katika malisho yenye kuwa wazi?*
17 Efraimu amejiunga na sanamu.+
Mumuache!
18 Wakati pombe* yao inaisha,Wanafanya umalaya.*
Na watawala* wake wanapenda sana mambo ya haya.+
19 Upepo utamufunika* katika mabawa yake,Na watasikilia zabihu zao haya.”
Maelezo ya Chini
^ Ao “eko.”
^ Ao “nitamuharibu.”
^ Ao “wataharibiwa.”
^ Ao “agizo la.”
^ Ao pengine, “Wamebadilisha utukufu wangu mwenyewe kuwa haya.”
^ Ao “wanainua nafsi yao kwenye.” Angalia Maana ya Maneno, “Nafsi.”
^ Ao “Watakuwa waasherati sana; Watafanya ukahaba.”
^ Tnn., “Vinaondoa moyo.”
^ Ao “Uasherati; Umalaya.”
^ Ao “fimbo ya muaguzi.”
^ Ao “uasherati; umalaya.”
^ Ao “uasherati; umalaya.”
^ Ao “uasherati; umalaya.”
^ Ao “uasherati; umalaya.”
^ Ao “uasherati; umalaya.”
^ Ao “eko.”
^ Tnn., “mahali penye nafasi kubwa?”
^ Ao “pombe ya ngano.”
^ Ao “wanakuwa waasherati sana; wanakuwa makahaba.”
^ Tnn., “ngao.”
^ Ao “utamufagilia mbali.”

