Hosea 14:1-9

  • Mwito wa kumurudilia Yehova (1-3)

    • Kutoa sifa ya midomo (2)

  • Israeli ataponyeshwa ukosefu wa uaminifu (4-9)

14  “Ee Israeli, umurudilie Yehova Mungu wako,+Kwa maana umejikwaa kwa sababu ya kosa lako.  2  Mumurudilie Yehova na maneno haya,Mumuambie, ‘Usamehe kosa letu+ na ukubali mambo ya muzuri,Na tutatoa sifa ya midomo yetu+ kama vile tungetoa ngombe-dume wadogo.*  3  Ashuru haitatuokoa.+ Hatutapanda farasi,+Na hatutaambia tena kazi ya mikono yetu, “Ee Mungu wetu!”,Kwa maana kupitia wewe mutoto mwenye hana baba anaonyeshwa rehema.’+  4  Nitaponyesha ukosefu wao wa uaminifu.+ Nitawapenda kwa kupenda kwangu mwenyewe,+Kwa sababu kasirani yangu imegeuka kutoka kwake.+  5  Nitakuwa kama umande kwa Israeli;Atatoa maua kama ua la yungiyungiNa ataingiza mizizi yake katika udongo kama miti ya Lebanoni.  6  Matawi yake yatasambaa,Uzuri wake utakuwa kama wa muzeituni,Na harufu yake ya muzuri kama ile ya Lebanoni.  7  Watakaa tena katika kivuli chake. Watakomalisha nafaka na watatoa maua kama muzabibu.+ Sifa yake itakuwa* kama divai ya Lebanoni.  8  Efraimu atasema, ‘Ningali na jambo gani tena la kufanya na sanamu?’+ Nitajibu na nitamuangalia kwa uangalifu.+ Nitakuwa kama muti wa muberoshi wenye afya ya muzuri. Matunda yako yatapatikana kwangu.”  9  Ni nani mwenye hekima? Aelewe mambo haya. Ni nani mwenye busara? Ayajue. Kwa maana njia za Yehova ni zenye kunyooka,+Na wenye haki watatembea ndani yake;Lakini wakosaji watajikwaa ndani yake.

Maelezo ya Chini

Tnn., “na sisi tutatoa ngombe-dume wachanga wa midomo yetu.”
Tnn., “Ukumbusho wake utakuwa.”