Hosea 14:1-9
14 “Ee Israeli, umurudilie Yehova Mungu wako,+Kwa maana umejikwaa kwa sababu ya kosa lako.
2 Mumurudilie Yehova na maneno haya,Mumuambie, ‘Usamehe kosa letu+ na ukubali mambo ya muzuri,Na tutatoa sifa ya midomo yetu+ kama vile tungetoa ngombe-dume wadogo.*
3 Ashuru haitatuokoa.+
Hatutapanda farasi,+Na hatutaambia tena kazi ya mikono yetu, “Ee Mungu wetu!”,Kwa maana kupitia wewe mutoto mwenye hana baba anaonyeshwa rehema.’+
4 Nitaponyesha ukosefu wao wa uaminifu.+
Nitawapenda kwa kupenda kwangu mwenyewe,+Kwa sababu kasirani yangu imegeuka kutoka kwake.+
5 Nitakuwa kama umande kwa Israeli;Atatoa maua kama ua la yungiyungiNa ataingiza mizizi yake katika udongo kama miti ya Lebanoni.
6 Matawi yake yatasambaa,Uzuri wake utakuwa kama wa muzeituni,Na harufu yake ya muzuri kama ile ya Lebanoni.
7 Watakaa tena katika kivuli chake.
Watakomalisha nafaka na watatoa maua kama muzabibu.+
Sifa yake itakuwa* kama divai ya Lebanoni.
8 Efraimu atasema, ‘Ningali na jambo gani tena la kufanya na sanamu?’+
Nitajibu na nitamuangalia kwa uangalifu.+
Nitakuwa kama muti wa muberoshi wenye afya ya muzuri.
Matunda yako yatapatikana kwangu.”
9 Ni nani mwenye hekima? Aelewe mambo haya.
Ni nani mwenye busara? Ayajue.
Kwa maana njia za Yehova ni zenye kunyooka,+Na wenye haki watatembea ndani yake;Lakini wakosaji watajikwaa ndani yake.

