Hosea 11:1-12

  • Upendo wa Mungu kwa Israeli tangu utoto wake (1-12)

    • “Kutoka Misri nilimuita mwana wangu” (1)

11  “Wakati Israeli alikuwa kijana mudogo, nilimupenda,+Na kutoka Misri nilimuita mwana wangu.+  2  Kadiri waliwaita,*Ni vile walienda mbali nao.+ Waliendelea kutoa zabihu kwa sanamu za Baali+Na kutoa zabihu kwa sanamu za kuchongwa.+  3  Lakini mimi ndiye nilimufundisha Efraimu kutembea,+ nikiwakamata katika mikono yangu;+Na hawakutambua kama nilikuwa nimewaponyesha.  4  Niliendelea kuwakokota kwa kamba za wanadamu,* ndiyo, kwa kamba za upendo;+Na nilikuwa kwao kama mutu mwenye kutosha nira kwenye mataya* yao,Na kwa upole nililetea kila mumoja chakula.  5  Hawatarudia katika inchi ya Misri, lakini Ashuru atakuwa mufalme wao,+Kwa sababu walikataa kurudia kwangu.+  6  Na upanga utazunguka-zunguka juu ya miji yake+Na kuharibu mapingo* yake na kumeza miji yake kwa sababu ya mipango yao ya mubaya.+  7  Watu wangu wako na muelekeo wa kukosa uaminifu kwangu.+ Hata kama waliwaita kuelekea juu,* hakuna mutu yeyote mwenye anasimama.  8  Namna gani ninaweza kukuacha, Ee Efraimu?+ Namna gani ninaweza kukutoa, Ee Israeli? Namna gani ninaweza kukutendea kama Adma? Namna gani ninaweza kukufanya ukuwe kama Seboimu?+ Nilikuwa nimebadilisha moyo wangu;Wakati uleule huruma zangu zinachochewa.*+  9  Sitaonyesha kasirani yangu yenye kuwaka. Sitaharibu tena Efraimu,+Kwa maana mimi ni Mungu, siko mwanadamu,Mutakatifu mwenye kuwa katikati yenu;Na sitakuja kwenu kwa kasirani kali. 10  Watamufuata Yehova, na atanguruma kama simba;+Wakati atanguruma, wana wake watakuja wakitetemeka kutoka mangaribi.+ 11  Watatetemeka kama ndege wakati watakuja kutoka Misri,Kama njiwa kutoka inchi ya Ashuru;+Na nitawafanya wakae katika nyumba zao,” ni vile Yehova anasema.+ 12  “Efraimu amenizunguka kwa maneno ya uongo,Na nyumba ya Israeli kwa udanganyifu.+ Lakini Yuda anaendelea kuenda huku na huku* pamoja na Mungu,Na ni muaminifu kwa Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi.”+

Maelezo ya Chini

Ni kusema, manabii na watu wengine wenye walitumwa ili kufundisha Israeli.
Ao “kamba za fazili,” kama za muzazi.
Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Ni kusema, kuelekea aina fulani yenye kuinuka ya ibada.
Tnn., “zimekuwa moto.”
Ao “kutembea.”