Hosea 11:1-12
11 “Wakati Israeli alikuwa kijana mudogo, nilimupenda,+Na kutoka Misri nilimuita mwana wangu.+
2 Kadiri waliwaita,*Ni vile walienda mbali nao.+
Waliendelea kutoa zabihu kwa sanamu za Baali+Na kutoa zabihu kwa sanamu za kuchongwa.+
3 Lakini mimi ndiye nilimufundisha Efraimu kutembea,+ nikiwakamata katika mikono yangu;+Na hawakutambua kama nilikuwa nimewaponyesha.
4 Niliendelea kuwakokota kwa kamba za wanadamu,* ndiyo, kwa kamba za upendo;+Na nilikuwa kwao kama mutu mwenye kutosha nira kwenye mataya* yao,Na kwa upole nililetea kila mumoja chakula.
5 Hawatarudia katika inchi ya Misri, lakini Ashuru atakuwa mufalme wao,+Kwa sababu walikataa kurudia kwangu.+
6 Na upanga utazunguka-zunguka juu ya miji yake+Na kuharibu mapingo* yake na kumeza miji yake kwa sababu ya mipango yao ya mubaya.+
7 Watu wangu wako na muelekeo wa kukosa uaminifu kwangu.+
Hata kama waliwaita kuelekea juu,* hakuna mutu yeyote mwenye anasimama.
8 Namna gani ninaweza kukuacha, Ee Efraimu?+
Namna gani ninaweza kukutoa, Ee Israeli?
Namna gani ninaweza kukutendea kama Adma?
Namna gani ninaweza kukufanya ukuwe kama Seboimu?+
Nilikuwa nimebadilisha moyo wangu;Wakati uleule huruma zangu zinachochewa.*+
9 Sitaonyesha kasirani yangu yenye kuwaka.
Sitaharibu tena Efraimu,+Kwa maana mimi ni Mungu, siko mwanadamu,Mutakatifu mwenye kuwa katikati yenu;Na sitakuja kwenu kwa kasirani kali.
10 Watamufuata Yehova, na atanguruma kama simba;+Wakati atanguruma, wana wake watakuja wakitetemeka kutoka mangaribi.+
11 Watatetemeka kama ndege wakati watakuja kutoka Misri,Kama njiwa kutoka inchi ya Ashuru;+Na nitawafanya wakae katika nyumba zao,” ni vile Yehova anasema.+
12 “Efraimu amenizunguka kwa maneno ya uongo,Na nyumba ya Israeli kwa udanganyifu.+
Lakini Yuda anaendelea kuenda huku na huku* pamoja na Mungu,Na ni muaminifu kwa Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi.”+
Maelezo ya Chini
^ Ni kusema, manabii na watu wengine wenye walitumwa ili kufundisha Israeli.
^ Ao “kamba za fazili,” kama za muzazi.
^ Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
^ Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
^ Ni kusema, kuelekea aina fulani yenye kuinuka ya ibada.
^ Tnn., “zimekuwa moto.”
^ Ao “kutembea.”

