Hosea 6:1-11

  • Wanaombwa kumurudilia Yehova (1-3)

  • Upendo mushikamanifu wenye haudumu wa watu (4-6)

    • Upendo mushikamanifu ni wa muzuri kuliko zabihu (6)

  • Mwenendo wa haya wa watu (7-11)

6  “Mukuje, na tumurudilie Yehova,Kwa maana ametupasua vipande-vipande,+ lakini atatuponyesha. Alitupiga, lakini atafunga vidonda vyetu.  2  Ataturudisha kwenye uzima kisha siku mbili. Katika siku ya tatu (3) atatuinua,Na tutaishi mbele yake.  3  Tutajua, tutatafuta kwa bidii kumujua Yehova. Kutokea kwake ni hakika kama mapambazuko;*Atakuja kwetu kama mvua kubwa,Kama mvua ya kipindi cha mvua ya mwisho, yenye inalowanisha dunia.”  4  “Nikufanye nini, Ee Efraimu? Nikufanye nini, Ee Yuda? Kwa maana upendo wenu mushikamanifu ni kama mawingu ya asubui,Kama umande wenye unapotea haraka.  5  Ndiyo sababu nitawakata-kata kwa kutumia manabii;+Nitawaua kwa maneno ya kinywa changu.+ Na hukumu juu yako zitangaa kama mwangaza.+  6  Kwa maana ninapendezwa na upendo mushikamanifu,* hapana zabihu,Na ujuzi wa Mungu kuliko matoleo mazima ya kuteketezwa.+  7  Lakini wao, kama wanadamu tu, wamevunja agano.+ Pale wamenisaliti.  8  Gileadi ni muji wa watenda-maovu,+Umefunikwa na alama za miguu yenye damu.+  9  Ushirika wa makuhani ni kama vikundi vya wanyanganyi wenye wanamuvizia mutu. Wanafanya mauaji katika njia kule Shekemu,+Kwa maana mwenendo wao ni wa haya. 10  Nimeona jambo la kuchukiza sana katika nyumba ya Israeli. Kule Efraimu anazoea kufanya ukahaba;+Israeli amejichafua.+ 11  Zaidi ya hayo, Ee Yuda, mavuno yamewekwa kwa ajili yako,Wakati nitakusanya na kurudisha watu wangu wenye walikamatwa mateka.”+

Maelezo ya Chini

Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
Ao “rehema.”