Hosea 12:1-14

  • Efraimu anapaswa kumurudilia Yehova (1-14)

    • Yakobo alishindana na Mungu (3)

    • Yakobo alilia ili Mungu amuonyeshe wema (4)

12  “Efraimu anajikulisha upepo. Anafukuza upepo wa mashariki siku nzima. Anaongeza uongo na jeuri. Wanafanya agano pamoja na Ashuru+ na kupeleka mafuta Misri.+  2  Yehova iko* na kesi ya hukumu juu ya Yuda;+Atamuomba Yakobo atoe hesabu kulingana na njia zake,Na atamulipa kulingana na matendo yake.+  3  Katika tumbo la uzazi alimushika ndugu yake kwenye kisigino,+Na kwa nguvu zake alishindana na Mungu.+  4  Aliendelea kushindana na malaika na akashinda. Alilia na kuomba amuonyeshe wema.”+ Alimukuta kule Beteli, na kule Yeye alisema pamoja na sisi,+  5  Yehova Mungu wa majeshi,+Yehova ndilo jina la ukumbusho wake.*+  6  “Basi rudia kwa Mungu wako,+Endelea kuwa na upendo mushikamanifu na haki,+Na umutumainie Mungu wako sikuzote.  7  Lakini katika mukono wa mufanyabiashara kuko mizani* ya udanganyifu;Anapenda kupunja.+  8  Efraimu anaendelea kusema, ‘Kwa kweli, nimekuwa tajiri;+Nimepata utajiri.+ Na katika kazi yangu yote ya jasho, hawatapata jambo lolote lenye kuwa kosa ao lenye kuwa zambi.’  9  Lakini mimi ni Yehova Mungu wako kuanzia* inchi ya Misri.+ Nitakufanya tena ukae katika mahemaKama katika siku za wakati wenye uliwekwa.* 10  Nilisema na manabii,+Niliongeza maono yao,Na nilisema kwa mifano kupitia manabii. 11  Gileadi amekuwa na udanganyifu*+ na uongo. Katika Gilgali wametoa zabihu za ngombe-dume,+Na mazabahu zao ni kama marundo ya majiwe katika mifereji ya shamba.+ 12  Yakobo alikimbilia katika eneo* la Aramu;*+Israeli+ alitumika kule ili apate bibi,+Na ili apate bibi alichunga kondoo.+ 13  Kupitia nabii, Yehova alipandisha Israeli kutoka Misri,+Na kupitia nabii alilindwa.+ 14  Efraimu amechukiza kwa uchungu;+Hatia yake ya damu inabakia juu yake;Bwana wake atamulipa kwa sababu ya lawama yake.”+

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “anakumbukwa kwa jina hilo.”
Ao “kilo.”
Ao “tangu.”
Ao pengine, “sikukuu.”
Ao “mambo ya uchawi.”
Ao “Siria.”
Tnn., “shamba.”