Hosea 12:1-14
12 “Efraimu anajikulisha upepo.
Anafukuza upepo wa mashariki siku nzima.
Anaongeza uongo na jeuri.
Wanafanya agano pamoja na Ashuru+ na kupeleka mafuta Misri.+
2 Yehova iko* na kesi ya hukumu juu ya Yuda;+Atamuomba Yakobo atoe hesabu kulingana na njia zake,Na atamulipa kulingana na matendo yake.+
3 Katika tumbo la uzazi alimushika ndugu yake kwenye kisigino,+Na kwa nguvu zake alishindana na Mungu.+
4 Aliendelea kushindana na malaika na akashinda.
Alilia na kuomba amuonyeshe wema.”+
Alimukuta kule Beteli, na kule Yeye alisema pamoja na sisi,+
5 Yehova Mungu wa majeshi,+Yehova ndilo jina la ukumbusho wake.*+
6 “Basi rudia kwa Mungu wako,+Endelea kuwa na upendo mushikamanifu na haki,+Na umutumainie Mungu wako sikuzote.
7 Lakini katika mukono wa mufanyabiashara kuko mizani* ya udanganyifu;Anapenda kupunja.+
8 Efraimu anaendelea kusema, ‘Kwa kweli, nimekuwa tajiri;+Nimepata utajiri.+
Na katika kazi yangu yote ya jasho, hawatapata jambo lolote lenye kuwa kosa ao lenye kuwa zambi.’
9 Lakini mimi ni Yehova Mungu wako kuanzia* inchi ya Misri.+
Nitakufanya tena ukae katika mahemaKama katika siku za wakati wenye uliwekwa.*
10 Nilisema na manabii,+Niliongeza maono yao,Na nilisema kwa mifano kupitia manabii.
11 Gileadi amekuwa na udanganyifu*+ na uongo.
Katika Gilgali wametoa zabihu za ngombe-dume,+Na mazabahu zao ni kama marundo ya majiwe katika mifereji ya shamba.+
12 Yakobo alikimbilia katika eneo* la Aramu;*+Israeli+ alitumika kule ili apate bibi,+Na ili apate bibi alichunga kondoo.+
13 Kupitia nabii, Yehova alipandisha Israeli kutoka Misri,+Na kupitia nabii alilindwa.+
14 Efraimu amechukiza kwa uchungu;+Hatia yake ya damu inabakia juu yake;Bwana wake atamulipa kwa sababu ya lawama yake.”+

