Hosea 5:1-15

  • Hukumu juu ya Efraimu na Yuda (1-15)

5  “Musikie jambo hili, ninyi makuhani,+Mukaze uangalifu, Ee nyumba ya Israeli,Musikilize, Ee nyumba ya mufalme,Kwa maana hukumu hii inawahusu ninyi pia;Kwa sababu ninyi ni mutego kwa MispaNa wavu wenye* kutandikwa juu ya Tabori.+  2  Na wale wenye kuanguka* wamezama sana* katika mauaji,Na ninawaonya* wote.  3  Ninajua Efraimu,Na Israeli haijifiche kwangu. Kwa maana sasa, Ee Efraimu, umetenda kwa umalaya;*Israeli amejichafua.+  4  Matendo yao hayawaruhusu wamurudilie Mungu wao,Kwa sababu kuko roho ya ukahaba* kati yao;+Na hawamutambue Yehova.  5  Kiburi cha Israeli kimeshuhudia juu yake;*+Israeli na pia Efraimu wamejikwaa katika kosa lao,Na Yuda imejikwaa pamoja nao.+  6  Walienda kumutafuta Yehova wakiwa na makundi yao na mifugo yao,Lakini hawakumupata. Alikuwa amejitenga nao.+  7  Wamemusaliti Yehova,+Kwa maana wamekuwa baba za wana wa kigeni. Sasa mwezi mumoja utawameza* pamoja na mafungu* yao.  8  Mupige baragumu+ katika Gibea, tarumbeta katika Rama!+ Mufanye makelele ya vita katika Bet-aveni+⁠—⁠nyuma yako, Ee Benyamini!  9  Ee Efraimu, utakuwa kitu cha kuogopesha sana katika siku ya azabu.+ Nimejulisha jambo lenye litatendeka hakika kati ya makabila ya Israeli. 10  Wakubwa wa Yuda ni kama watu wenye wanasogeza mupaka.+ Nitawamwangia kasirani yangu kali kama maji. 11  Efraimu amekandamizwa, amepondwa kwa hukumu,Kwa maana alikusudia kufuata adui yake.+ 12  Basi nilikuwa kama nondo* kwa EfraimuNa kama kuoza kwa ajili ya nyumba ya Yuda. 13  Wakati Efraimu aliona ugonjwa wake, na Yuda kidonda chake,Efraimu alienda Ashuru+ na kutuma ujumbe kwa mufalme mukubwa. Lakini hakuweza kuwaponyesha ninyi,Na hakuweza kuponyesha kidonda chenu. 14  Kwa maana nitakuwa kama mwana-simba kwa ajili ya Efraimu,Na kama simba mwenye nguvu* kwa ajili ya nyumba ya Yuda. Mimi mwenyewe nitapasua vipande-vipande na kuondoka;+Nitawachukua, na hakuna mwenye atawaokoa.+ 15  Nitaenda na kurudia mahali pangu mupaka wakati watabeba matokeo ya hatia yao,Na kisha watatafuta kukubaliwa na mimi.*+ Wakati watakuwa katika taabu, watanitafuta.”+

Maelezo ya Chini

Ao “makila yenye.”
Ao “waasi.”
Ao “wamejiingiza sana.”
Ao “nitawatia nizamu.”
Ao “umefanya uasherati; umefanya ukahaba.”
Ao “uasherati; umalaya.”
Tnn., “mbele ya uso wake.”
Ao “mashamba.”
Ao pengine, “Katika mwezi mumoja watamezwa.”
Nondo ni kidudu fulani cha kuruka chenye kinakula nguo.
Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Tnn., “watatafuta uso wangu.”