Hosea 5:1-15
-
Hukumu juu ya Efraimu na Yuda (1-15)
5 “Musikie jambo hili, ninyi makuhani,+Mukaze uangalifu, Ee nyumba ya Israeli,Musikilize, Ee nyumba ya mufalme,Kwa maana hukumu hii inawahusu ninyi pia;Kwa sababu ninyi ni mutego kwa MispaNa wavu wenye* kutandikwa juu ya Tabori.+
2 Na wale wenye kuanguka* wamezama sana* katika mauaji,Na ninawaonya* wote.
3 Ninajua Efraimu,Na Israeli haijifiche kwangu.
Kwa maana sasa, Ee Efraimu, umetenda kwa umalaya;*Israeli amejichafua.+
4 Matendo yao hayawaruhusu wamurudilie Mungu wao,Kwa sababu kuko roho ya ukahaba* kati yao;+Na hawamutambue Yehova.
5 Kiburi cha Israeli kimeshuhudia juu yake;*+Israeli na pia Efraimu wamejikwaa katika kosa lao,Na Yuda imejikwaa pamoja nao.+
6 Walienda kumutafuta Yehova wakiwa na makundi yao na mifugo yao,Lakini hawakumupata.
Alikuwa amejitenga nao.+
7 Wamemusaliti Yehova,+Kwa maana wamekuwa baba za wana wa kigeni.
Sasa mwezi mumoja utawameza* pamoja na mafungu* yao.
8 Mupige baragumu+ katika Gibea, tarumbeta katika Rama!+
Mufanye makelele ya vita katika Bet-aveni+—nyuma yako, Ee Benyamini!
9 Ee Efraimu, utakuwa kitu cha kuogopesha sana katika siku ya azabu.+
Nimejulisha jambo lenye litatendeka hakika kati ya makabila ya Israeli.
10 Wakubwa wa Yuda ni kama watu wenye wanasogeza mupaka.+
Nitawamwangia kasirani yangu kali kama maji.
11 Efraimu amekandamizwa, amepondwa kwa hukumu,Kwa maana alikusudia kufuata adui yake.+
12 Basi nilikuwa kama nondo* kwa EfraimuNa kama kuoza kwa ajili ya nyumba ya Yuda.
13 Wakati Efraimu aliona ugonjwa wake, na Yuda kidonda chake,Efraimu alienda Ashuru+ na kutuma ujumbe kwa mufalme mukubwa.
Lakini hakuweza kuwaponyesha ninyi,Na hakuweza kuponyesha kidonda chenu.
14 Kwa maana nitakuwa kama mwana-simba kwa ajili ya Efraimu,Na kama simba mwenye nguvu* kwa ajili ya nyumba ya Yuda.
Mimi mwenyewe nitapasua vipande-vipande na kuondoka;+Nitawachukua, na hakuna mwenye atawaokoa.+
15 Nitaenda na kurudia mahali pangu mupaka wakati watabeba matokeo ya hatia yao,Na kisha watatafuta kukubaliwa na mimi.*+
Wakati watakuwa katika taabu, watanitafuta.”+
Maelezo ya Chini
^ Ao “makila yenye.”
^ Ao “waasi.”
^ Ao “wamejiingiza sana.”
^ Ao “nitawatia nizamu.”
^ Ao “umefanya uasherati; umefanya ukahaba.”
^ Ao “uasherati; umalaya.”
^ Tnn., “mbele ya uso wake.”
^ Ao “mashamba.”
^ Ao pengine, “Katika mwezi mumoja watamezwa.”
^ Nondo ni kidudu fulani cha kuruka chenye kinakula nguo.
^ Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
^ Tnn., “watatafuta uso wangu.”

