Hosea 10:1-15

  • Israeli, muzabibu wenye kuharibika, ataharibiwa (1-15)

10  “Israeli ni muzabibu wenye kuharibika* wenye unazaa matunda yake.+ Kadiri matunda yake yanaongezeka, ni vile anaongeza mazabahu zake;+Kadiri inchi yake inazaa muzuri, ni vile nguzo zake takatifu zinakuwa muzuri zaidi.+  2  Moyo wao ni munafiki;*Sasa watapatikana na hatia. Kuko ule mwenye atavunja mazabahu zao na kuharibu nguzo zao.  3  Sasa watasema, ‘Hatuna mufalme,+ kwa maana hatukumuogopa Yehova. Na mufalme angetufanyia nini?’  4  Wanasema maneno yenye hayana maana, wanaapa viapo vya uongo,+ na wanafanya maagano;Basi hukumu yenye imechipuka ni kama magugu yenye sumu katika mifereji ya shamba.+  5  Wakaaji wa Samaria wataogopa kwa sababu ya sanamu ya kitoto-dume cha ngombe cha Bet-aveni.+ Watu wake wataiombolezea,Na vilevile makuhani wake wa mungu wa kigeni wenye walifurahi juu yake na juu ya utukufu wake,Kwa maana itatoka kwao na kuenda katika uhamisho.  6  Itapelekwa Ashuru kama zawadi kwa mufalme mukubwa.+ Efraimu atapatishwa haya,Na Israeli atasikia haya kwa sababu ya shauri lenye alifuata.+  7  Samaria na mufalme wake hakika wataharibiwa,*+Kama tawi lenye lilikatwa lenye kuwa juu ya uso wa maji.  8  Mahali pa juu pa Bet-aveni,+ zambi ya Israeli,+ pataharibiwa.+ Miiba na michongoma itakomaa juu ya mazabahu zao.+ Watu wataambia milima, ‘Mutufunike!’ Na vilima, ‘Mutuangukie!’+  9  Tangu siku za Gibea umetenda zambi,+ Ee Israeli. Kule waliendelea katika mwenendo uleule. Vita haikufikia* wana wa ukosefu wa haki katika Gibea. 10  Nitawatia pia nizamu wakati nitapenda. Na vikundi vya watu vitakusanyika ili kuwashambulia,Wakati makosa yao mbili yatafungwa kwao.* 11  Efraimu alikuwa kitoto-dike cha ngombe chenye kilizoezwa na chenye kilipenda kukanyanga-kanyanga nafaka,Basi nililinda shingo yake ya muzuri. Sasa nitafanya mutu fulani apande* juu ya Efraimu.+ Yuda atalima; Yakobo atamulimia. 12  Mupande mbegu kwa ajili yenu katika haki na muvune upendo mushikamanifu. Mulime kwa ajili yenu udongo wenye unafaa kulimwa+Kukiwa bado wakati wa kumutafuta Yehova,+Mupaka wakati atakuja na kukufundisha haki.+ 13  Lakini mumelima uovu,Mumevuna ukosefu wa haki,+Na mumekula matunda ya udanganyifu;Kwa maana mumeweka tegemeo katika njia yenu wenyewe,Katika wingi wa wapiganaji-vita wenu. 14  Fujo itatokea juu ya watu wako,Na miji yako yote yenye ngome itaharibiwa,+Kama vile Shalmani aliharibu nyumba ya Arbeli,Katika siku ya pigano, wakati mama walivunjwa vipande-vipande pembeni ya watoto wao. 15  Ni vile mutatendewa, Ee Beteli,+ kwa sababu ya uovu wenu mwingi. Wakati wa mapambazuko* kwa hakika mufalme wa Israeli ataharibiwa.”*+

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “wenye kupanuka.”
Ao “mujanja; mudanganyifu.”
Tnn., “watanyamazishwa.”
Ao “haikuharibu kabisa.”
Ni kusema, wakati watabeba azabu yao kama nira.
Ao “aweke nira.”
Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
Tnn., “atanyamazishwa.”