Hosea 7:1-16
7 “Wakati ninaponyesha Israeli,Kosa la Efraimu linafunuliwa pia,+Na uovu wa Samaria.+
Kwa maana wamezoea kutenda kwa udanganyifu;+Wezi wanaingia kwa nguvu na vikundi vya wanyanganyi vinashambulia inje kwa kushitukia.+
2 Lakini hawaseme katika moyo wao kwamba nitakumbuka uovu wao wote.+
Sasa matendo yao yamewazunguka pande zote;Yako mbele ya uso wangu.
3 Wanafurahisha mufalme kwa uovu wao,Na wakubwa kwa udanganyifu wao.
4 Wote ni wazinifu,Wamewaka kama tanuru yenye mutengenezaji wa mikate amewasha,Mwenye anaacha kuchochea moto kisha kuponda donge mupaka linatiwa chachu.
5 Katika siku ya mufalme wetu, wakubwa wamekuwa wagonjwa—Wako na kasirani kali kwa sababu ya divai.+
Amenyoosha mukono wake kwa wazihaki.
6 Kwa maana wanakaribia wakiwa na mioyo yenye kuwaka kama tanuru.*
Mutengenezaji wa mikate analala usiku muzima;Asubui tanuru inawaka kama mwali wa moto.
7 Wote wamekuwa moto kama tanuru,Na wanateketeza watawala* wao.
Wafalme wao wote wameanguka;+Hakuna mutu yeyote kati yao mwenye ananiita.+
8 Efraimu anachangamana na mataifa.+
Efraimu ni kama keki ya muviringo yenye imeachwa bila kugeuzwa.
9 Wageni wamenyonya nguvu yake,+ lakini yeye hajue jambo hilo.
Na imvi zake zimegeuka kuwa nyeupe, lakini yeye hatambue jambo hilo.
10 Kiburi cha Israeli kimeshuhudia juu yake,+Lakini hawakumurudilia Yehova Mungu wao,+Na hawakumutafuta ijapokuwa mambo hayo yote.
11 Efraimu ni kama njiwa mujinga, mwenye kukosa akili.*+
Wameita Misri;+ wameenda Ashuru.+
12 Kila mahali wanaenda, nitatandika wavu wangu* juu yao.
Nitawashusha chini kama ndege wa mbinguni.
Nitawatia nizamu kulingana na onyo lenye lilitolewa kwa mukusanyiko wao.+
13 Ole wao, kwa maana wamenikimbia!
Waangamie, kwa maana wamenikosea!
Nilikuwa tayari kuwakomboa, lakini wamesema uongo juu yangu.+
14 Hawakuniita mimi kutoka katika moyo wao ili niwasaidie,+Hata kama waliendelea kulalamika katika vitanda vyao.
Kwa ajili ya nafaka yao na divai yao mupya walikuwa wanajikata-kata;Wanageuka ili kunipinga.
15 Hata kama niliwatia nizamu na kutia nguvu mikono yao,Wananipinga, wanapanga mambo ya mubaya.
16 Waligeuza mwendo, lakini hapana kuelekea jambo fulani lenye kuinuka;*Walikuwa wenye hawatumainike kama upinde wenye kuregea.+
Wakubwa wao wataanguka kwa upanga kwa sababu ya ndimi zao zenye kukosa heshima.
Kwa sababu ya jambo hilo watakuwa kitu cha kuchekelewa katika inchi ya Misri.”+

