Ezra 7:1-28
7 Kisha mambo hayo, wakati wa utawala wa Mufalme Artashasta+ wa Uajemi, Ezra*+ akarudia. Alikuwa mwana wa Seraya,+ mwana wa Azaria, mwana wa Hilkia,+
2 mwana wa Shalumu, mwana wa Sadoki, mwana wa Ahitubu,
3 mwana wa Amaria, mwana wa Azaria,+ mwana wa Merayoti,
4 mwana wa Zeraya, mwana wa Uzi, mwana wa Buki,
5 mwana wa Abishua, mwana wa Finehasi,+ mwana wa Eleazari,+ mwana wa Haruni,+ mukubwa wa makuhani.
6 Huyu Ezra alitoka Babiloni. Alikuwa mwandikaji* na alijua sana* Sheria ya Musa,+ yenye Yehova Mungu wa Israeli alikuwa ametoa. Mufalme alimupatia kila kitu chenye aliomba, kwa maana mukono wa Yehova Mungu wake ulikuwa juu yake.
7 Waisraeli fulani, makuhani, Walawi,+ waimbaji,+ walinzi wa milango mikubwa,+ na watumishi wa hekalu,*+ wakapanda kuenda Yerusalemu katika mwaka wa saba (7) wa Mufalme Artashasta.
8 Na Ezra akakuja Yerusalemu mwezi wa tano (5), katika mwaka wa saba (7) wa mufalme huyo.
9 Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, akaanza safari ya kutoka Babiloni, na akafika Yerusalemu siku ya kwanza ya mwezi wa tano (5), kwa sababu mukono mwema wa Mungu wake ulikuwa juu yake.+
10 Ezra alikuwa ametayarisha moyo* wake ili kuchunguza Sheria ya Yehova na kuifuata,+ na kufundisha masharti na hukumu katika Israeli.+
11 Hii ndiyo kopi ya barua yenye Mufalme Artashasta alimupatia Ezra kuhani na mwandikaji,* mwenye alijua sana* amri za Yehova na masharti yake yenye alipatia Israeli:
12 * “Artashasta,+ mufalme wa wafalme, kwa Ezra kuhani, mwandikaji* wa Sheria ya Mungu wa mbinguni: Ukuwe na amani kamilifu. Na sasa
13 nimetoa amri kwamba kila mutu katika utawala wangu mwenye kuwa mumoja wa watu wa Israeli na makuhani wao na Walawi, mwenye anapenda kuenda na wewe Yerusalemu, aende.+
14 Kwa maana umetumwa na mufalme na washauri wake saba ili kuchunguza kama Sheria ya Mungu wako, yenye uko nayo,* inafuatwa katika Yuda na Yerusalemu,
15 na kukamata feza na zahabu yenye mufalme na washauri wake wamemutolea kwa kupenda Mungu wa Israeli, mwenye makao yake iko Yerusalemu,
16 na feza na zahabu yote yenye utapokea* katika jimbo lote la* Babiloni, na zawadi yenye watu na makuhani wanatoa kwa kupenda kwa ajili ya nyumba ya Mungu wao, yenye iko Yerusalemu.+
17 Na mara moja utanunua kwa feza hizo ngombe-dume,+ kondoo-dume,+ wana-kondoo,+ na matoleo yao ya nafaka+ na matoleo yao ya kinywaji,+ na utavipeleka kwenye mazabahu ya nyumba ya Mungu wenu kule Yerusalemu.
18 “Na feza na zahabu yenye itabakia, wewe na ndugu zako munaweza kuitumia namna mutapenda, kulingana na mapenzi ya Mungu wenu.
19 Na vyombo vyote vyenye umepewa kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wako, uvipeleke mbele ya Mungu kule Yerusalemu.+
20 Na vitu vingine vya lazima kwa ajili ya nyumba ya Mungu wako vyenye unaombwa kutoa, utavikamata katika hazina ya mufalme na kuvitoa.+
21 “Mimi, Mufalme Artashasta, nimetoa amri kwa wachunga-hazina wote katika eneo la Ngambo ya ule Muto* kwamba kila kitu chenye Ezra,+ kuhani, mwandikaji* wa Sheria ya Mungu wa mbinguni, anawaomba kinapaswa kufanywa haraka,
22 mupaka kufikia talanta* mia moja (100) za feza, vipimo vya kori* mia moja vya ngano, vipimo vya bati* mia moja vya divai,+ vipimo vya bati mia moja vya mafuta,+ na chumvi+ kadiri ataomba.
23 Kila kitu chenye Mungu wa mbinguni anaamuru kifanywe kwa bidii kwa ajili ya nyumba ya Mungu wa mbinguni,+ ili kasirani kali isikuwe juu ya utawala wa mufalme na wana wake.+
24 Na munajulishwa tena kwamba hairuhusiwe kulipisha kodi, ushuru,+ ao malipo ya njia kwa makuhani na Walawi, wapiga-muziki,+ walinzi wa milango, watumishi wa hekalu,*+ na wafanyakazi wa nyumba hii ya Mungu.
25 “Na wewe, Ezra, kulingana na hekima yenye ulipewa na Mungu wako,* chagua waamuzi wa raia na waamuzi ili wahukumu watu wote wenye kuwa katika eneo la Ngambo ya ule Muto, wale wote wenye wanajua sheria za Mungu wako; na munapaswa kufundisha kila mutu mwenye hazijue.+
26 Na kila mutu mwenye hatafuata Sheria ya Mungu wako na sheria ya mufalme atahukumiwa bila kukawia, ikuwe ni kuuawa, kufukuzwa, kulipa amande,* ao kufungwa.”
27 Asifiwe Yehova Mungu wa mababu zetu, mwenye alitia katika moyo wa mufalme wazo la kupamba nyumba ya Yehova yenye iko Yerusalemu!+
28 Na amenionyesha upendo mushikamanifu mbele ya mufalme,+ washauri wake,+ na wakubwa wote wenye nguvu wa mufalme. Kwa hiyo nikapata uhodari* kwa sababu mukono wa Yehova Mungu wangu ulikuwa juu yangu, na nikakusanya wanaume wenye kuongoza wa* Israeli ili waende pamoja na mimi.
Maelezo ya Chini
^ Maana yake “Musaada.”
^ Ao “mwandishi.”
^ Ao “Alikuwa mwandishi mwenye ufundi wa.”
^ Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
^ Ao “alikuwa ameazimia katika moyo.”
^ Ao “mwandishi.”
^ Ao “mwandikaji wa maneno ya.”
^ Mwanzoni maandishi ya Ezr 7:12 mupaka 7:26 yaliandikwa katika Kiaramu.
^ Ao “mwandishi.”
^ Tnn., “yenye kuwa katika mukono wako.”
^ Ao “wilaya yote ya utawala wa.”
^ Tnn., “utapata.”
^ Ao “Eneo la Ngambo Ingine ya Efrati.”
^ Ao “mwandishi.”
^ Kori moja ilikuwa sawa na litre 220 (vibaba 200). Angalia Nyongeza B14.
^ Bati moja ilikuwa sawa na litre 22 (galoni 5.81). Angalia Nyongeza B14.
^ Talanta moja ilikuwa sawa na kilograme 34.2 (aunsi troi 1.101). Angalia Nyongeza B14.
^ Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
^ Tnn., “kulingana na hekima ya Mungu wako yenye iko katika mukono wako.”
^ Ao “faini.”
^ Ao “nikajipatia nguvu.”
^ Tnn., “vichwa vya.”