Ezra 10:1-44
10 Wakati Ezra alikuwa anasali+ na kuungama, akilia na akiwa amelala uso chini mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli, kikundi kikubwa cha wanaume, wanamuke na watoto wa Israeli wakakuja na kumuzunguka, kwa sababu watu walikuwa wanalia sana.
2 Kisha Shekania mwana wa Yehieli+ wa wana wa Elamu+ akamuambia Ezra: “Tumekosa kuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa* wanamuke wa kigeni kutoka katika vikundi vya watu wa inchi.+ Ijapokuwa hivyo, kungali tumaini kwa ajili ya Israeli.
3 Sasa, tufanye agano pamoja na Mungu wetu+ na kufukuza wanamuke hao wote na watoto wao, kulingana na muongozo wa Yehova na wa wale wenye kuheshimia sana* sheria ya Mungu wetu.+ Tutende kulingana na Sheria.
4 Simama, kwa maana jambo hili ni daraka lako, na sisi tuko pamoja na wewe. Ukuwe na nguvu na uchukue hatua.”
5 Basi Ezra akasimama na kuapisha wakubwa wa makuhani, Walawi, na Israeli wote ili wafanye mambo yenye yalikuwa yamesemwa.+ Kwa hiyo wakafanya kiapo.
6 Sasa Ezra akatoka mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli na kuenda katika chumba* cha Yehohanani mwana wa Eliashibu. Hata kama alienda kule, hakukula chakula wala kunywa maji, kwa maana alikuwa anaomboleza kwa sababu ya ukosefu wa uaminifu wa watu wenye walikuwa wamepelekwa katika uhamisho.+
7 Kisha wakatangaza katika Yuda na Yerusalemu yote kwamba watu wote wenye walikuwa wamepelekwa zamani katika uhamisho wakusanyike pamoja Yerusalemu;
8 na kulingana na uamuzi wa wakubwa na wazee, mutu yeyote mwenye hangekuja katika muda wa siku tatu (3), vitu vyake vyote vingenyanganywa* na angefukuzwa katika kutaniko la watu wenye walikuwa wamepelekwa katika uhamisho.+
9 Kwa hiyo wanaume wote wa Yuda na Benyamini wakakusanyika pamoja kule Yerusalemu kwa siku tatu (3), ni kusema, katika mwezi wa kenda (9), siku ya makumi mbili (20) ya mwezi huo. Watu wote walikuwa wamekaa kwenye kiwanja cha nyumba ya Mungu wa kweli, wakitetemeka kwa sababu ya jambo hilo na kwa sababu ya mvua nyingi.
10 Kisha Ezra kuhani akasimama na kuwaambia: “Mumekosa uaminifu kwa kuoa wanamuke wa kigeni,+ na hivyo mumeongeza hatia ya Israeli.
11 Sasa muungame kwa Yehova Mungu wa mababu zenu na mufanye mapenzi yake. Mujitenge na vikundi vya watu wa inchi na wanamuke hao wa kigeni.”+
12 Kwa hiyo kutaniko lote likajibu hivi kwa sauti kubwa: “Ni daraka letu kufanya sawasawa na vile unasema.
13 Lakini, watu ni wengi, na hiki ni kipindi cha mvua. Haiwezekane kusimama inje, na jambo hili halitamalizika kwa siku moja ao mbili tu, kwa maana tumeasi sana kuhusu jambo hili.
14 Kwa hiyo, tafazali, wakubwa wetu wabakie hapa ili washugulikie mambo hayo kwa ajili ya kutaniko lote;+ na wote katika miji yetu wenye wameoa wanamuke wa kigeni wakuje wakati wenye uliwekwa, pamoja na wazee na waamuzi wa kila muji, mupaka wakati tutageuzia mbali kasirani yenye kuwaka ya Mungu kutoka kwetu kwa sababu ya jambo hili.”
15 Hata hivyo, Yonatani mwana wa Asaheli na Yahzeya mwana wa Tikva wakapinga jambo hilo, na Meshulamu na Shabetai+ Walawi wakawaunga mukono.
16 Lakini watu wenye walikuwa wamepelekwa zamani katika uhamisho wakafanya mambo yenye walikuwa wamekubaliana; na Ezra kuhani na vichwa vya jamaa za upande wa baba, wenye walikuwa wametajwa kwa majina yao, wakakusanyika peke yao siku ya kwanza ya mwezi wa kumi (10) ili kuchunguza jambo hilo;
17 na kufikia siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakamaliza kuchunguza wanaume wenye walikuwa wameoa wanamuke wa kigeni.
18 Na ikavumbuliwa kwamba kati ya wana wa makuhani kulikuwa wale wenye walikuwa wameoa wanamuke wa kigeni:+ kati ya wana wa Yeshua+ mwana wa Yehosadaki na ndugu zake, Maaseya, Eliezeri, Yaribu, na Gedalia.
19 Lakini wakaahidi* kufukuza wanamuke wao, na kwa sababu walikuwa na hatia, walipaswa kutoa kondoo-dume wa kundi kwa ajili ya hatia yao.+
20 Kati ya wana wa Imeri,+ kulikuwa Hanani na Zebadia;
21 na kati ya wana wa Harimu,+ Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli, na Uzia;
22 na kati ya wana wa Pashuri,+ Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Netaneli, Yozabadi, na Eleasa.
23 Na kati ya Walawi, kulikuwa Yozabadi, Shimei, Kelaya (ni kusema, Kelita), Petahia, Yuda, na Eliezeri;
24 na kati ya waimbaji, Eliashibu; na kati ya walinzi wa milango mikubwa, Shalumu, Telemu, na Uri.
25 Na kati ya Israeli, kati ya wana wa Paroshi,+ kulikuwa Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya, na Benaya;
26 na kati ya wana wa Elamu,+ Matania, Zekaria, Yehieli,+ Abdi, Yeremoti, na Eliya;
27 na kati ya wana wa Zatu,+ Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremoti, Zabadi, na Aziza;
28 na kati ya wana wa Bebai,+ Yehohanani, Hanania, Zabai, na Atlai;
29 na kati ya wana wa Bani, Meshulamu, Maluku, Adaya, Yashubu, Sheali, na Yeremoti;
30 na kati ya wana wa Pahat-moabu,+ Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui, na Manase;
31 na kati ya wana wa Harimu,+ Eliezeri, Ishiya, Malkiya,+ Shemaya, Shimeoni,
32 Benyamini, Maluku, na Shemaria;
33 kati ya wana wa Hashumu,+ Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase, na Shimei;
34 kati ya wana wa Bani, Maadai, Amramu, na Ueli,
35 Benaya, Bedeya, Keluhi,
36 Vania, Meremoti, Eliashibu,
37 Matania, Matenai, na Yaasu;
38 na kati ya wana wa Binui, Shimei,
39 Shelemia, Natani, Adaya,
40 Maknadebai, Shashai, Sharai,
41 Azareli, Shelemia, Shemaria,
42 Shalumu, Amaria, na Yosefu;
43 na kati ya wana wa Nebo, Yeieli, Matitia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli, na Benaya.
44 Wote hao walikuwa wameoa wanamuke wa kigeni,+ na walifukuza bibi zao pamoja na wana wao.+
Maelezo ya Chini
^ Ao “kuingiza katika nyumba zetu.”
^ Tnn., “wenye kutetemeka mbele ya.”
^ Ao “chumba cha kukulia chakula.”
^ Ao “vingepigwa marufuku.”
^ Tnn., “wakapana mikono yao ili.”