Ufunuo kwa Yohana 5:1-14

  • Kitabu cha kukunjwa chenye mihuri saba (1-5)

  • Mwanakondoo achukua kitabu cha kukunjwa (6-8)

  • Mwanakondoo anastahili kufungua mihuri (9-14)

5  Nami nikaona katika mkono wa kuume wa Yule aliyeketi kwenye kile kiti cha ufalme,+ kitabu cha kukunjwa kilichoandikwa pande zote mbili,* kilichofungwa kabisa kwa mihuri saba.  Nami nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kubwa: “Ni nani anayestahili kukifungua kile kitabu cha kukunjwa na kuvunja mihuri yake?”  Lakini hakuna yeyote mbinguni au duniani au chini ya dunia aliyeweza kukifungua kitabu hicho cha kukunjwa au kutazama ndani yake.  Nikalia sana kwa sababu hakupatikana yeyote aliyestahili kukifungua kitabu hicho cha kukunjwa au kutazama ndani yake.  Lakini mmoja wa wale wazee akaniambia: “Acha kulia. Tazama! Simba wa kabila la Yuda,+ mzizi+ wa Daudi,+ ameshinda+ ili akifungue kitabu hicho cha kukunjwa na mihuri yake saba.”  Nami nikamwona mwanakondoo+ aliyeonekana kana kwamba amechinjwa,+ akiwa amesimama katikati ya kile kiti cha ufalme na katikati ya wale viumbe hai wanne na katikati ya wale wazee,+ akiwa na pembe saba na macho saba, na macho hayo yanamaanisha roho saba za Mungu+ ambazo zimetumwa katika dunia nzima.  Mara moja akaja na kukichukua kutoka katika mkono wa kuume wa Yule aliyeketi kwenye kile kiti cha ufalme.+  Alipokichukua kile kitabu cha kukunjwa, wale viumbe hai wanne na wale wazee 24+ wakaanguka chini mbele ya Mwanakondoo, na kila mmoja alikuwa na kinubi na mabakuli ya dhahabu yaliyojaa uvumba. (Uvumba huo unamaanisha sala za watakatifu.)+  Nao wanaimba wimbo mpya,+ wakisema: “Wewe unastahili kukichukua kile kitabu cha kukunjwa na kufungua mihuri yake, kwa sababu ulichinjwa na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu+ kutoka katika kila kabila na lugha na watu na taifa,+ 10  na ukawafanya kuwa ufalme+ na makuhani kwa Mungu wetu,+ nao watatawala wakiwa wafalme+ juu ya dunia.” 11  Nami nikaona, na kusikia sauti ya malaika wengi kuzunguka kile kiti cha ufalme na wale viumbe hai na wale wazee, na idadi yao ilikuwa makumi ya maelfu ya makumi ya maelfu na maelfu ya maelfu,+ 12  nao walikuwa wakisema kwa sauti kubwa: “Mwanakondoo aliyechinjwa+ anastahili kupokea uwezo na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na baraka.”+ 13  Nami nikasikia kila kiumbe kilicho mbinguni na duniani na chini ya dunia+ na baharini, na vitu vyote vilivyo ndani yake, vikisema: “Yule anayeketi kwenye kile kiti cha ufalme+ na Mwanakondoo+ na wawe na baraka na heshima+ na utukufu na nguvu milele na milele.”+ 14  Wale viumbe hai wanne walikuwa wakisema: “Amina!” na wale wazee wakaanguka chini na kuabudu.

Maelezo ya Chini

Tnn., “upande wa ndani na wa nyuma.”