Ufunuo kwa Yohana 14:1-20

  • Mwanakondoo na wale 144,000 (1-5)

  • Ujumbe kutoka kwa malaika watatu (6-12)

    • Malaika katikati ya mbingu akiwa na habari njema (6, 7)

  • Wenye furaha ni wale wanaokufa katika muungano na Kristo (13)

  • Dunia yavunwa mara mbili (14-20)

14  Kisha nikaona, na tazama! Mwanakondoo+ amesimama juu ya Mlima Sayuni,+ na pamoja naye 144,000+ walioandikwa jina lake na jina la Baba yake+ kwenye mapaji ya nyuso zao.  Nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi na kama sauti ya ngurumo kubwa; na sauti niliyosikia ilikuwa kama ya waimbaji wanaofuatanisha sauti zao wakipiga vinubi vyao.  Nao wanaimba kana kwamba ni wimbo mpya+ mbele ya kile kiti cha ufalme na mbele ya wale viumbe hai wanne+ na wale wazee,+ na hakuna yeyote aliyeweza kujifunza kikamili wimbo ule ila wale 144,000,+ ambao wamenunuliwa kutoka duniani.  Hao ndio wale ambao hawakujitia unajisi na wanawake; kwa kweli, wao ni mabikira.+ Hao ndio wanaoendelea kumfuata Mwanakondoo popote anapoenda.+ Hao walinunuliwa+ kutoka kati ya wanadamu wakiwa matunda ya kwanza+ kwa Mungu na kwa Mwanakondoo,  na hamna udanganyifu uliopatikana katika vinywa vyao; wao hawana dosari.+  Nami nikamwona malaika mwingine akiruka katikati ya mbingu,* naye alikuwa na habari njema ya milele ili aitangaze kwa wale wanaokaa duniani, kwa kila taifa na kabila na lugha na watu.+  Alikuwa akisema kwa sauti kubwa: “Mwogopeni Mungu na kumpa utukufu, kwa sababu saa ya hukumu yake imefika,+ kwa hiyo mwabuduni Yule aliyeziumba mbingu na dunia na bahari+ na chemchemi za maji.”*  Na mwingine, malaika wa pili, akafuata, akisema: “Ameanguka! Babiloni Mkubwa+ ameanguka,+ yule aliyeyafanya mataifa yote yanywe divai ya hamu* ya uasherati* wake!”+  Malaika mwingine, wa tatu, akawafuata, akisema kwa sauti kubwa: “Yeyote akimwabudu yule mnyama wa mwituni+ na sanamu yake na kupokea alama kwenye paji la uso wake au kwenye mkono wake,+ 10  yeye pia atakunywa divai ya hasira ya Mungu inayomwagwa ndani ya kikombe cha ghadhabu Yake bila kuchanganywa na kitu,+ naye atateswa kwa moto na kiberiti+ machoni pa malaika watakatifu na machoni pa Mwanakondoo. 11  Na moshi wa kuteswa kwao unapanda milele na milele,+ nao hawana pumziko mchana na usiku, wale wanaomwabudu yule mnyama wa mwituni na sanamu yake na yeyote anayepokea alama ya jina lake.+ 12  Hapa ndipo watakatifu wanapohitaji uvumilivu,+ wale wanaoshika amri za Mungu na kushika imara imani+ kwa Yesu.” 13  Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wenye furaha ni wafu wanaokufa katika muungano na Bwana+ tangu wakati huu na kuendelea. Ndiyo, roho inasema, acheni wapumzike kutokana na kazi yao ngumu, kwa maana mambo waliyotenda yanaambatana nao moja kwa moja.”* 14  Kisha nikaona, na tazama! wingu jeupe, na mtu fulani kama mwana wa binadamu alikuwa ameketi juu ya wingu hilo,+ akiwa na taji la dhahabu juu ya kichwa chake na mundu mkali mkononi mwake. 15  Malaika mwingine akatokea katika patakatifu pa hekalu, akimwambia kwa sauti kubwa yule aliyeketi juu ya lile wingu: “Tia ndani mundu wako uvune, kwa sababu saa ya kuvuna imefika, kwa maana mavuno ya dunia yameiva kabisa.”+ 16  Na yule aliyeketi juu ya wingu akautia mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa. 17  Na bado malaika mwingine akatokea katika patakatifu pa hekalu palipo mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali. 18  Na bado malaika mwingine akatokea katika madhabahu naye alikuwa na mamlaka juu ya moto. Naye akamwambia kwa sauti kubwa yule aliyekuwa na mundu mkali: “Tia ndani mundu wako mkali ukusanye vishada vya mzabibu wa dunia, kwa sababu zabibu zake zimeiva.”+ 19  Yule malaika akatia mundu wake katika dunia na kuukusanya mzabibu wa dunia, naye akautupa ndani ya shinikizo kubwa la divai la hasira ya Mungu.+ 20  Lile shinikizo la divai likakanyagiwa nje ya jiji, na damu ikatoka katika lile shinikizo la divai hata kufikia juu kwenye lijamu za farasi umbali wa stadia 1,600.*

Maelezo ya Chini

Au “katikati ya anga; juu.”
Au “mabubujiko ya maji.”
Neno la Kigiriki, por·neiʹa. Angalia Kamusi.
Au “hasira.”
Au “pamoja nao.”
Karibu kilomita 296 (maili 184). Stadiamu moja ilikuwa sawa na mita 185 (futi 606.95). Angalia Nyongeza B14.