Malaki 4:1-6

  • Kuja kwa Eliya kabla ya siku ya Yehova (1-6)

    • “Jua la uadilifu litawaangazia” (2)

4  “Kwa maana tazama! siku inakuja inayowaka kama tanuru,+ wakati ambapo wote wenye kimbelembele na wote wanaotenda uovu watakuwa kama majani makavu. Siku hiyo inayokuja kwa hakika itawateketeza,” asema Yehova wa majeshi, “nayo haitawaachia mzizi wala tawi.  Lakini ninyi mnaoliheshimu* jina langu, jua la uadilifu litawaangazia likiwa na miale inayoponya;* nanyi mtaruka huku na huku kama ndama waliononeshwa.”  “Nanyi mtawakanyaga-kanyaga waovu chini ya miguu yenu, kwa sababu watakuwa kama mavumbi chini ya nyayo zenu siku nitakayochukua hatua,” asema Yehova wa majeshi.  “Kumbukeni Sheria ya Musa mtumishi wangu, masharti na maamuzi niliyoamuru kule Horebu ili Waisraeli wote wayatii.+  “Tazama! Namtuma kwenu nabii Eliya+ kabla haijaja ile siku kuu ya Yehova yenye kuogopesha.+  Naye ataigeuza mioyo ya akina baba iwarudie wana,+ na mioyo ya wana iwarudie akina baba, ili nisije na kuipiga dunia, na hivyo kuiangamiza.”

Maelezo ya Chini

Tnn., “mnaoliogopa.”
Tnn., “mabawa yanayoponya.”