Malaki 2:1-17

  • Makuhani washindwa kuwafundisha watu (1-9)

    • Midomo ya kuhani inapaswa kulinda ujuzi (7)

  • Watu wawataliki wake zao bila msingi (10-17)

    • “‘Ninachukia talaka,’ asema Yehova” (16)

2  “Na sasa, enyi makuhani, amri hii inawahusu.+  Mkikataa kusikiliza na kuitia moyoni mwenu ili kulitukuza jina langu,” asema Yehova wa majeshi, “nitawaletea laana,+ nami nitabadili baraka zenu ziwe laana.+ Naam, nimebadili baraka ziwe laana, kwa sababu hamwitii moyoni mwenu.”  “Tazameni! Nitaharibu* mbegu zenu zilizopandwa kwa sababu yenu,+ nami nitawapaka kinyesi cha wanyama usoni, kinyesi cha sherehe zenu; nanyi mtabebwa na kupelekwa kwenye kinyesi hicho.*  Ndipo mtakapojua kwamba nimewapa amri hii ili agano langu pamoja na Lawi liendelee,”+ asema Yehova wa majeshi.  “Agano langu pamoja naye lilikuwa la uzima na amani, ambalo nilimpa, pamoja na hofu.* Aliniogopa, naam, aliliheshimu jina langu.  Sheria ya kweli ilikuwa* kinywani mwake,+ na ukosefu wa uadilifu haukupatikana midomoni mwake. Alitembea pamoja nami kwa amani na kwa unyoofu,+ naye aliwageuza wengi kutoka katika uovu.  Kwa maana midomo ya kuhani inapaswa kulinda ujuzi, na watu wanapaswa kutafuta sheria* kutoka kinywani mwake,+ kwa sababu yeye ni mjumbe wa Yehova wa majeshi.  “Lakini ninyi wenyewe mmegeuka na kuiacha njia. Mmewafanya wengi wajikwae kuhusiana na sheria.*+ Mmeliharibu agano la Lawi,”+ asema Yehova wa majeshi.  “Kwa hiyo nitawafanya ninyi mdharauliwe na kuwa duni mbele ya watu wote, kwa sababu hamkushika njia zangu badala yake mliitekeleza sheria kwa upendeleo.”*+ 10  “Je, sisi sote hatuna baba mmoja?+ Je, hatukuumbwa na Mungu yuleyule? Basi kwa nini tunatendeana kwa hila,+ na kulitia unajisi agano la mababu zetu? 11  Yuda ametenda kwa hila, na jambo fulani lenye kuchukiza limetendwa Israeli na Yerusalemu; kwa maana Yuda ameutia unajisi utakatifu wa* Yehova,+ Anaoupenda, naye amemchukua binti ya mungu wa kigeni kuwa bibi harusi.+ 12  Yehova atamwangamiza kutoka katika mahema ya Yakobo mtu yeyote anayefanya hivyo, mtu yeyote yule,* hata ingawa anamtolea zawadi Yehova wa majeshi.”+ 13  “Na kuna jambo lingine* mnalotenda linalofanya madhabahu ya Yehova ifunikwe kwa machozi na kilio na maombolezo, hivi kwamba hakazii tena uangalifu zawadi mnayomtolea wala kutazama kwa kibali kitu chochote kinachotoka mikononi mwenu.+ 14  Nanyi mnauliza, ‘Kwa sababu gani?’ Ni kwa sababu Yehova amekuwa shahidi kati yako na mke wa ujana wako, ambaye umemtendea kwa hila, ingawa yeye ni mwenzi wako na mke wako kupitia agano.*+ 15  Lakini kuna mtu ambaye hakufanya hivyo, kwa sababu ya roho iliyobaki ndani yake. Na mtu huyo alikuwa akitafuta nini? Uzao wa* Mungu. Basi jilindeni kuhusiana na roho yenu, na usimtendee kwa hila mke wa ujana wako. 16  Kwa maana ninachukia* talaka,”+ asema Yehova Mungu wa Israeli, “na pia yule anayefunika vazi lake kwa ukatili,”* asema Yehova wa majeshi. “Nanyi jilindeni wenyewe kuhusiana na roho yenu, na hampaswi kutenda kwa hila.+ 17  “Mmemchosha Yehova kwa maneno yenu.+ Lakini mnauliza, ‘Tumemchoshaje?’ Kwa kusema, ‘Kila mtu anayetenda maovu ni mwema machoni pa Yehova, naye hupendezwa na mtu huyo,’+ au kwa kuuliza, ‘Yuko wapi Mungu wa haki?’”

Maelezo ya Chini

Tnn., “Nitakemea.”
Yaani, mahali ambapo kinyesi cha wanyama wa dhabihu kilitupwa.
Au “heshima, adhama.”
Au “Mafundisho ya kweli yalikuwa.”
Au “mafundisho.”
Au labda, “kwa mafundisho yenu.”
Au “ubaguzi.”
Au labda, “ametia unajisi mahali patakatifu pa.”
Tnn., “yule aliye macho na yule anayejibu.”
Tnn., “la pili.”
Au “mke wako halali.”
Tnn., “Mbegu ya.”
Tnn., “anachukia.”
Tnn., “anayetenda ukatili.”