Mathayo 9:1-38
9 Basi, akaipanda mashua, akaanza kuvuka na kwenda katika jiji lake.+
2 Na, tazama! wakamletea mtu aliyepooza akiwa amelala juu ya kitanda.+ Alipoona imani yao Yesu akamwambia yule mwenye kupooza: “Jipe moyo, mwanangu; dhambi zako zimesamehewa.”+
3 Na, tazama! baadhi ya waandishi wakaambiana wao kwa wao: “Mtu huyu anakufuru.”+
4 Naye Yesu, akijua fikira zao,+ akasema: “Kwa nini mnafikiri mambo maovu mioyoni mwenu?+
5 Kwa mfano, ni jambo gani lililo rahisi zaidi, kusema, Dhambi zako zimesamehewa, au kusema, Simama, utembee?+
6 Hata hivyo, ili mjue kwamba Mwana wa binadamu ana mamlaka duniani ya kusamehe dhambi+—” ndipo akamwambia yule mwenye kupooza: “Simama, chukua kitanda chako, uende nyumbani kwako.”+
7 Naye akasimama, akaenda nyumbani kwake.
8 Umati ulipoona hilo wakaingiwa na woga, nao wakamtukuza Mungu,+ aliyewapa wanadamu mamlaka+ ya namna hiyo.
9 Halafu, alipokuwa akiondoka mahali hapo, Yesu akamwona mtu anayeitwa Mathayo akiwa ameketi kwenye ofisi ya kodi, naye akamwambia: “Uwe mfuasi wangu.”+ Akasimama mara moja na kumfuata.+
10 Baadaye, huku akiwa ameketi mezani katika nyumba,+ tazama! wakusanya-kodi wengi na watenda-dhambi wakaja na kuanza kuketi pamoja na Yesu na wanafunzi wake.
11 Mafarisayo walipoona hilo wakaanza kuwaambia wanafunzi wake: “Kwa nini mwalimu wenu anakula pamoja na wakusanya-kodi na watenda-dhambi?”+
12 Alipowasikia, akasema: “Watu wenye afya hawahitaji tabibu,+ bali wenye kuugua ndio wanaomhitaji.
13 Nendeni, basi, mkajifunze maana ya jambo hili, ‘Ninataka rehema, wala si dhabihu.’+ Kwa maana nilikuja kuwaita, si watu waadilifu, bali watenda-dhambi.”
14 Ndipo wanafunzi wa Yohana wakamjia na kuuliza: “Kwa nini sisi na Mafarisayo hufunga lakini wanafunzi wako hawafungi?”+
15 Ndipo Yesu akawaambia: “Je, rafiki za bwana-arusi wana sababu ya kuomboleza, maadamu bwana-arusi+ yupo pamoja nao? Lakini siku zitakuja wakati ambapo bwana-arusi ataondolewa+ kwao, ndipo watakapofunga.+
16 Hakuna mtu anayeshona kiraka cha nguo mpya juu ya vazi la nje la zamani; kwa maana nguvu zake zingelivuta lile vazi la nje nalo lingeraruka vibaya zaidi.+
17 Wala watu hawaweki divai mpya ndani ya viriba vya divai vilivyozeeka; lakini wakifanya hivyo, vile viriba hupasuka na ile divai humwagika navyo viriba huharibika.+ Bali watu huweka divai mpya ndani ya viriba vipya vya divai, na vitu vyote viwili huhifadhiwa.”+
18 Alipokuwa akiwaambia mambo hayo, tazama! mtawala+ fulani aliyekuwa amekaribia, alianza kumsujudia,+ akisema: “Kufikia sasa binti yangu lazima awe amekufa;+ lakini njoo uweke mkono wako juu yake naye atakuwa hai.”+
19 Basi Yesu akaondoka, akaanza kumfuata; pia wanafunzi wake wakamfuata.
20 Na, tazama! mwanamke mwenye kutaabika miaka kumi na miwili kutokana na mtiririko wa damu+ akaja nyuma na kuugusa upindo wa vazi lake la nje;+
21 kwa maana alikuwa akisema moyoni mwake: “Nikigusa tu vazi lake la nje nitapona.”+
22 Yesu akageuka, akamwona, na kusema: “Jipe moyo, binti yangu; imani yako imekuponya.”+ Na kutoka saa hiyo mwanamke huyo akapona.+
23 Basi, alipoingia katika nyumba ya yule mtawala+ na kuwaona wapiga-filimbi na umati wa watu wakipiga kelele kwa kuvurugika,+
24 Yesu akaanza kusema: “Ondokeni hapa, kwa maana msichana mdogo hakufa, bali analala usingizi.”+ Ndipo wakaanza kumcheka kwa dharau.+
25 Mara tu umati ulipokuwa umetoka nje, akaingia na kuushika mkono wake,+ na huyo msichana akainuka.+
26 Bila shaka, habari za jambo hilo zikaenea katika eneo hilo lote.
27 Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, wanaume wawili vipofu+ wakamfuata, wakipaaza sauti na kusema: “Uturehemu,+ Mwana wa Daudi.”
28 Alipokuwa amekwisha kuingia katika ile nyumba, wale wanaume vipofu wakamjia, naye Yesu akawauliza: “Je, mna imani+ kwamba ninaweza kufanya hivyo?” Wakamjibu: “Ndiyo, Bwana.”
29 Ndipo akayagusa macho yao,+ akisema: “Na iwe hivyo kwenu kulingana na imani yenu.”
30 Na macho yao yakapata kuona. Zaidi ya hayo, Yesu akawaagiza kwa kusisitiza, akisema: “Msimwambie mtu yeyote jambo hilo.”+
31 Lakini wao, baada ya kufika nje, wakajulisha habari zake katika eneo hilo lote.+
32 Sasa walipokuwa wakiondoka, tazama! watu wakamletea bubu aliyeingiwa na roho mwovu;+
33 na yule roho mwovu alipokuwa amekwisha kufukuzwa yule bubu akaongea.+ Basi, ule umati ukashangaa+ na kusema: “Jambo kama hili halijapata kuonekana kamwe katika Israeli.”
34 Lakini Mafarisayo wakaanza kusema: “Yeye huwafukuza roho waovu kwa nguvu za mtawala wa roho waovu.”+
35 Na Yesu akaondoka ili kutembelea majiji na vijiji vyote, akifundisha katika masinagogi yao na kuhubiri habari njema ya ufalme na kuponya kila namna ya magonjwa na kila namna ya udhaifu.+
36 Alipouona umati akawasikitikia,+ kwa sababu walikuwa wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji.+
37 Ndipo akawaambia wanafunzi wake: “Ndiyo, mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache.+
38 Kwa hiyo, mwombeni Bwana wa mavuno awatume wafanyakazi katika mavuno yake.”+