Mathayo 28:1-20
28 Baada ya siku ya sabato, kulipokuwa kukipambazuka katika siku ya kwanza ya juma, Maria Magdalene na yule Maria mwingine wakaja kulitazama kaburi.+
2 Na, tazama! tetemeko kubwa la nchi lilikuwa limetukia; kwa maana malaika wa Yehova alikuwa ameshuka kutoka mbinguni akakaribia na kuliviringisha jiwe, naye alikuwa ameketi juu yake.+
3 Alionekana kama umeme,+ na mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji.+
4 Ndiyo, wale walinzi wakatetemeka na kuwa kama wafu kwa sababu ya kumwogopa.
5 Lakini malaika+ akawajibu wanawake hao, akawaambia: “Msiogope, kwa maana ninajua mnamtafuta Yesu+ aliyetundikwa mtini.
6 Hayupo hapa, kwa maana alifufuliwa,+ kama alivyosema. Njooni, tazameni mahali alipokuwa amelala.
7 Nanyi nendeni upesi mkawaambie wanafunzi wake kwamba amefufuliwa+ kutoka kwa wafu, na, tazama! atawatangulia kuingia Galilaya;+ huko mtamwona. Tazama! Nimewaambia ninyi.”+
8 Kwa hiyo, wakaondoka upesi kaburini, wakiwa na woga na shangwe kubwa, wakakimbia kuwajulisha wanafunzi wake.+
9 Na, tazama! Yesu akakutana nao na kusema: “Siku njema!” Wao wakakaribia, wakamshika miguu yake, wakamsujudia.
10 Ndipo Yesu akawaambia: “Msiogope! Nendeni, mkawajulishe ndugu zangu,+ ili wapate kwenda zao Galilaya; na huko wataniona.”
11 Walipokuwa wameondoka na kwenda, tazama! baadhi ya walinzi+ wakaingia jijini na kuwaambia wakuu wa makuhani mambo yote yaliyokuwa yametukia.
12 Na walipokuwa wamekusanyika pamoja wakiwa na wanaume wazee na kushauriana, wakawapa hao askari-jeshi kiasi cha kutosha cha vipande vya fedha+
13 na kusema: “Semeni, ‘Wanafunzi wake+ walikuja wakati wa usiku wakamwiba tulipokuwa tumelala usingizi.’
14 Na hilo likifika masikioni mwa gavana, tutamshawishi na tutawaondolea ninyi wasiwasi.”
15 Kwa hiyo wakachukua vile vipande vya fedha wakafanya kama walivyoagizwa; na maneno hayo yamesambazwa kotekote kati ya Wayahudi mpaka leo hii.
16 Hata hivyo, wale wanafunzi kumi na mmoja wakaingia Galilaya+ mpaka kwenye mlima ambako Yesu alikuwa amewafanyia mpango,
17 nao walipomwona wakasujudu, lakini baadhi yao walikuwa na shaka.+
18 Naye Yesu akakaribia na kuwaambia, akisema: “Nimepewa mamlaka yote+ mbinguni na duniani.
19 Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi+ kutoka kwa watu wa mataifa yote,+ mkiwabatiza+ katika jina la Baba+ na la Mwana+ na la roho takatifu,+
20 na kuwafundisha+ kushika+ mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.+ Na, tazama! mimi nipo pamoja nanyi+ siku zote mpaka umalizio wa mfumo wa mambo.”+