Mathayo 23:1-39

23  Ndipo Yesu akasema na umati na wanafunzi wake,+ akisema:  “Waandishi+ na Mafarisayo wamejiketisha katika kiti cha Musa.+  Kwa hiyo mambo yote wanayowaambia ninyi,+ yafanyeni na kuyashika, lakini msifanye kulingana na matendo yao,+ kwa maana wao husema lakini hawatendi.  Wao hufunga mizigo mizito na kuiweka juu ya mabega ya watu,+ lakini wao wenyewe hawataki kuisogeza kwa kidole chao.+  Kazi zote wanazozifanya wao huzifanya ili watazamwe na watu;+ kwa maana wanapanua vibweta+ vyenye maandiko ambavyo wao huvaa kama ulinzi, na kuongeza ukubwa wa pindo zenye nyuzinyuzi+ za mavazi yao.  Wao hupenda mahali penye kuonekana zaidi+ kwenye milo ya jioni na viti vya mbele katika masinagogi,+  na salamu+ katika masoko na kuitwa Rabi na watu.+  Lakini ninyi, msiitwe Rabi, kwa maana mwalimu+ wenu ni mmoja, lakini ninyi nyote ni ndugu.  Zaidi ya hayo, msimwite mtu yeyote baba yenu duniani, kwa maana Baba+ yenu ni mmoja, Yule wa mbinguni. 10  Wala msiitwe ‘viongozi,’+ kwa maana Kiongozi wenu ni mmoja, Kristo. 11  Lakini aliye mkubwa zaidi katikati yenu lazima awe mhudumu wenu.+ 12  Yeyote yule anayejiinua atanyenyekezwa,+ na yeyote yule anayejinyenyekeza atainuliwa.+ 13  “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa sababu mnawafungia+ watu ufalme wa mbinguni; kwa maana ninyi+ wenyewe hamwingii, wala hamwaruhusu wale wanaoenda huko waingie. 14  —— 15  “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki!+ kwa sababu mnasafiri katika bahari na katika nchi kavu ili kugeuza imani ya mtu mmoja, na anapogeuka ninyi humfanya astahili Gehena* mara mbili zaidi kuliko ninyi wenyewe. 16  “Ole wenu ninyi, viongozi vipofu,+ mnaosema, ‘Mtu yeyote akiapa kwa hekalu, si kitu; lakini mtu yeyote akiapa kwa dhahabu ya hekalu, atakuwa na wajibu.’+ 17  Wapumbavu na vipofu! Kwa kweli, ni kipi kilicho kikubwa zaidi, dhahabu au hekalu ambalo limeitakasa dhahabu?+ 18  Pia, ‘Mtu yeyote akiapa kwa madhabahu, si kitu; lakini mtu yeyote akiapa kwa zawadi iliyo juu yake, atakuwa na wajibu.’ 19  Vipofu! Kwa kweli, ni kipi kilicho kikubwa zaidi, zawadi au madhabahu+ ambayo huitakasa zawadi? 20  Kwa hiyo yeye anayeapa kwa madhabahu anaapa kwa hiyo na kwa vitu vyote vilivyo juu yake; 21  naye anayeapa kwa hekalu anaapa kwa hilo na kwa yeye anayekaa ndani yake;+ 22  naye anayeapa kwa mbingu anaapa kwa kiti cha ufalme cha Mungu+ na kwa yeye anayeketi juu yake. 23  “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa sababu ninyi huitoa sehemu ya kumi+ ya mnanaa na dili na bizari, lakini mmepuuza mambo mazito zaidi ya Sheria, yaani, haki+ na rehema+ na uaminifu.+ Ilikuwa lazima kuyafanya mambo haya, na bado kutopuuza yale mambo mengine. 24  Viongozi vipofu,+ ambao humchuja mbu+ lakini hummeza ngamia!+ 25  “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! kwa sababu ninyi husafisha upande wa nje wa kikombe+ na wa sahani, lakini upande wa ndani vimejaa vitu vilivyoporwa+ na mambo yenye kupita kiasi. 26  Farisayo kipofu,+ kwanza safisha upande wa ndani wa kikombe+ na wa sahani, ili upande wake wa nje upate kuwa safi pia. 27  “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki!+ kwa sababu mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa,+ ambayo kwa nje yanaonekana kwa kweli kuwa mazuri lakini ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila namna ya ukosefu wa usafi. 28  Katika njia hiyo ninyi pia, kwa kweli, mnaonekana kwa nje kuwa waadilifu kwa watu,+ lakini ndani mmejaa unafiki na uasi-sheria. 29  “Ole wenu ninyi, waandishi na Mafarisayo, wanafiki!+ kwa sababu mnajenga makaburi ya manabii na kuyarembesha makaburi ya waadilifu,+ 30  nanyi mnasema, ‘Kama tungekuwa katika siku za mababu zetu, hatungekuwa washiriki pamoja nao katika damu ya manabii.’+ 31  Kwa hiyo mnatoa ushahidi juu yenu wenyewe kwamba ninyi ni wana wa wale waliowaua manabii.+ 32  Hivyo, basi, kijazeni kipimo+ cha mababu zenu. 33  “Nyoka, uzao wa nyoka-vipiri,+ mtaikimbiaje hukumu ya Gehena?*+ 34  Kwa sababu hiyo, tazameni, ninatuma+ kwenu manabii na watu wenye hekima na wafundishaji wa watu wote.+ Baadhi yao mtawaua+ na kuwatundika mtini, na baadhi yao mtawapiga mijeledi+ katika masinagogi yenu na kuwatesa jiji baada ya jiji; 35  ili ije juu yenu damu yote ya uadilifu iliyomwagwa juu ya dunia,+ tangu damu+ ya Abeli+ mwadilifu mpaka damu ya Zekaria mwana wa Barakia, ambaye mlimuua katikati ya patakatifu na madhabahu.+ 36  Kwa kweli ninawaambia ninyi, Mambo yote haya yatakipata kizazi hiki.+ 37  “Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji wa manabii+ na ambaye huwapiga kwa mawe+ wale waliotumwa kwake,+​—⁠ni mara ngapi nilitaka kuwakusanya watoto wako, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake!+ Lakini hamkutaka.+ 38  Tazama! Nyumba yenu+ mmeachiwa hali ya ukiwa.+ 39  Kwa maana ninawaambia ninyi, Hamtaniona kamwe tangu sasa mpaka mtakaposema, ‘Aliyebarikiwa ni yule anayekuja katika jina la Yehova!’ ”+

Maelezo ya Chini

Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.
Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.