Mathayo 10:1-42

10  Kwa hiyo akawaita wanafunzi wake kumi na wawili na kuwapa mamlaka juu ya roho wachafu,+ ili wawafukuze na kuponya kila namna ya ugonjwa na kila namna ya udhaifu.  Majina ya wale mitume kumi na wawili+ ndiyo haya:+ Kwanza, Simoni, anaiyeitwa Petro,+ na Andrea+ ndugu yake; na Yakobo mwana wa Zebedayo+ na Yohana ndugu yake;  Filipo na Bartholomayo;+ Tomasi+ na Mathayo+ mkusanya-kodi; Yakobo mwana wa Alfayo,+ na Thadayo;  Simoni Mkananayo,+ na Yuda Iskariote, ambaye baadaye alimsaliti.+  Yesu aliwatuma hao kumi na wawili, akiwapa maagizo haya:+ “Msiende katika barabara ya mataifa, na msiingie katika jiji la Wasamaria;+  bali, badala ya hivyo, nendeni kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.+  Mnapoenda, hubirini, mkisema, ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’+  Ponyeni wagonjwa,+ fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, fukuzeni roho waovu. Mlipokea bure, toeni bure.+  Msichukue dhahabu wala fedha wala shaba kwa ajili ya mikoba yenu ya mshipi,+ 10  wala mfuko wa chakula kwa ajili ya safari, wala mavazi mawili ya ndani, wala viatu wala fimbo; kwa maana mfanyakazi anastahili chakula chake.+ 11  “Katika jiji lolote lile au kijiji chochote kile mtakapoingia, tafuteni ni nani humo anayestahili, mkae humo mpaka mtakapoondoka.+ 12  Mnapoingia ndani ya nyumba, wapeni salamu watu wa nyumba hiyo; 13  na ikiwa nyumba hiyo inastahili, acheni amani mnayoitakia ikae juu yake;+ lakini ikiwa haistahili, acheni amani yenu irudi kwenu. 14  Popote pale ambapo mtu hawakaribishi au hasikilizi maneno yenu, mnapoondoka katika nyumba hiyo au jiji hilo yakung’uteni mavumbi kutoka miguuni penu.+ 15  Kwa kweli mimi ninawaambia ninyi, Itakuwa rahisi zaidi kwa nchi ya Sodoma+ na Gomora kwenye Siku ya Hukumu kuliko kwa jiji hilo.+ 16  “Tazama! Mimi ninawatuma ninyi kama kondoo katikati ya mbwa-mwitu;+ kwa hiyo jionyesheni wenyewe kuwa wenye kujihadhari kama nyoka+ na hata hivyo wasio na hatia kama njiwa.+ 17  Jihadharini na watu;+ kwa maana watawapeleka mahakamani,+ nao watawapiga ninyi mijeledi+ katika masinagogi yao.+ 18  Naam, mtakokotwa na kupelekwa mbele ya magavana na wafalme+ kwa ajili yangu, ili kuwa ushahidi+ kwao na kwa mataifa. 19  Hata hivyo, watakapowapeleka ninyi, msihangaike juu ya jambo mtakalosema au jinsi mtakavyolisema; kwa maana mtapewa jambo la kusema katika saa hiyo;+ 20  kwa maana wanaosema si ninyi tu, bali ni roho ya Baba yenu inayosema kupitia ninyi.+ 21  Zaidi ya hayo, mtu atamtoa ndugu+ yake afe, na baba mtoto wake, na watoto watainuka juu ya wazazi na kufanya wauawe.+ 22  Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa sababu ya jina langu;+ lakini yule atakayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokolewa.+ 23  Wakati wanapowatesa ninyi katika jiji moja, kimbilieni jiji lingine;+ kwa maana kwa kweli ninawaambia ninyi, Hamtamaliza kuyazunguka+ majiji ya Israeli mpaka Mwana wa binadamu atakapofika.+ 24  “Mwanafunzi hampiti mwalimu wake, wala mtumwa hampiti bwana wake.+ 25  Inatosha kwa mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumwa kama bwana wake.+ Ikiwa watu wamemwita mwenye nyumba Beelzebuli,+ je, hawatawaita hivyo wale watu wa nyumbani mwake hata zaidi? 26  Kwa hiyo msiwaogope; kwa maana hakuna kitu chochote kilichofunikwa ambacho hakitafunuliwa, na cha siri ambacho hakitajulikana.+ 27  Lile ninalowaambia ninyi gizani, lisemeni nuruni; na lile mnalolisikia likinong’onwa, lihubirini juu ya paa za nyumba.+ 28  Na msiwaogope+ wale ambao wanaua mwili lakini hawawezi kuiua nafsi; lakini badala ya hivyo mwogopeni+ yeye anayeweza kuangamiza vyote viwili nafsi na mwili katika Gehena.*+ 29  Je, shomoro wawili hawauzwi kwa sarafu ya thamani ndogo?+ Na bado hakuna hata mmoja wao atakayeanguka chini bila Baba yenu kujua.+ 30  Lakini nywele zenyewe za kichwa chenu zimehesabiwa zote.+ 31  Kwa hiyo msiogope: Ninyi ni bora kuliko shomoro wengi.+ 32  “Basi, kila mtu anayekiri mbele ya wanadamu kwamba yuko katika umoja pamoja nami, mimi pia nitakiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni kwamba niko katika umoja pamoja naye;+ 33  lakini yeyote yule anayenikana mimi mbele ya watu, mimi pia nitamkana+ mbele za Baba yangu aliye mbinguni. 34  Msifikiri nilikuja kuleta amani duniani; nilikuja kuleta, si amani,+ bali upanga. 35  Kwa maana nilikuja kuleta mgawanyiko, mtu kumpinga baba yake, binti kumpinga mama yake, mke aliye mchanga kumpinga mama-mkwe wake.+ 36  Kwa kweli, adui za mtu watakuwa watu wa nyumbani kwake mwenyewe. 37  Anayempenda baba au mama kuliko mimi hanistahili; naye anayempenda mwana au binti kuliko mimi hanistahili.+ 38  Na yeyote yule asiyeuchukua mti wake wa mateso na kunifuata hanistahili.+ 39  Yeye anayeipata nafsi yake ataipoteza, naye anayeipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataipata.+ 40  “Yeye anayewapokea ninyi ananipokea mimi pia, naye anayenipokea mimi anampokea pia yule aliyenituma.+ 41  Anayempokea nabii kwa sababu ni nabii atapata thawabu ya nabii,+ naye anayempokea mtu mwadilifu kwa sababu ni mtu mwadilifu atapata thawabu ya mtu mwadilifu.+ 42  Na yeyote yule anayempa mmoja wa wadogo hawa kikombe tu cha maji baridi ya kunywa kwa sababu ni mwanafunzi, kwa kweli ninawaambia ninyi, huyo hatapoteza thawabu yake kamwe.”+

Maelezo ya Chini

Bonde la Hinomu. Tazama Nyongeza 2.