Mathayo 3:1-17
3 Katika siku hizo Yohana Mbatizaji+ alikuja akihubiri katika nyika+ ya Yudea,
2 akisema: “Tubuni,+ kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.”+
3 Huyu, kwa kweli, ndiye anayesemwa kupitia nabii Isaya+ kwa maneno haya: “Sikilizeni! Mtu fulani anapaaza sauti nyikani, ‘Tayarisheni+ njia ya Yehova! Nyoosheni barabara zake.’ ”
4 Lakini Yohana huyu mavazi yake yalikuwa ya manyoya ya ngamia+ na alikuwa na mshipi wa ngozi+ kiunoni mwake; nacho chakula chake kilikuwa nzige+ na asali ya mwituni.+
5 Ndipo Yerusalemu na Yudea yote na nchi yote kandokando ya Yordani zikamwendea,
6 naye akawabatiza watu katika Mto Yordani,+ wakiungama waziwazi dhambi zao.
7 Alipoona wengi wa Mafarisayo na Masadukayo+ wakija kwenye ubatizo, akawaambia: “Ninyi uzao wa nyoka-vipiri,+ ni nani ambaye amewaonyesha ninyi kuikimbia ghadhabu+ inayokuja?
8 Kwa hiyo basi zaeni matunda yanayofaa toba;+
9 na msiseme moyoni mwenu, ‘Abrahamu ndiye baba yetu.’+ Kwa maana ninawaambia ninyi kwamba Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu+ watoto kutoka katika mawe haya.
10 Tayari shoka+ limewekwa kwenye mzizi wa miti; basi, kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa+ na kutupwa ndani ya moto.+
11 Mimi ninawabatiza ninyi kwa maji+ kwa sababu ya toba+ yenu; lakini yule anayekuja+ nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, ambaye viatu vyake mimi sistahili kuvivua.+ Huyo atawabatiza ninyi kwa roho takatifu+ na kwa moto.+
12 Sepetu yake ya kupepetea imo mkononi mwake, naye atausafisha uwanja wake wa kupuria, na kukusanya ngano yake katika ghala+ lakini makapi atayateketeza kwa moto+ usioweza kuzimwa.”
13 Ndipo Yesu akaja kutoka Galilaya+ mpaka Yordani kwa Yohana, kusudi ambatize.+
14 Lakini Yohana akajaribu kumzuia, akisema: “Mimi ndiye ninayehitaji kubatizwa na wewe, na je, wewe unakuja kwangu?”
15 Yesu akajibu, akamwambia: “Acha iwe hivyo, wakati huu, kwa maana katika njia hiyo inafaa kwetu kufanya yote yaliyo ya uadilifu.”+ Ndipo akaacha kumzuia.
16 Baada ya kubatizwa Yesu akapanda mara moja kutoka katika maji; na, tazama! mbingu zikafunguliwa,+ naye akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa,+ ikija juu yake.+
17 Tazama! Kulikuwa pia na sauti+ kutoka mbinguni iliyosema: “Huyu ni Mwanangu,+ mpendwa,+ ambaye nimemkubali.”+