Mathayo 4:1-25
4 Ndipo Yesu akaongozwa na roho kuingia nyikani+ ili kujaribiwa+ na Ibilisi.
2 Alipokuwa amefunga siku 40,+ mchana na usiku, akaona njaa.
3 Pia, Mjaribu+ akaja na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu,+ yaambie mawe haya yawe mikate.”
4 Lakini akajibu na kusema: “Imeandikwa, ‘Mwanadamu ataishi, si kwa mkate tu, bali kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Yehova.’ ”+
5 Ndipo Ibilisi akamchukua, akaenda pamoja naye, na kuingia katika lile jiji takatifu,+ naye akamsimamisha juu ya mnara wa hekalu
6 na kumwambia: “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu, jitupe chini;+ kwa maana imeandikwa, ‘Atawaagiza malaika zake kukuhusu wewe, nao watakuchukua mikononi mwao, ili usipate kamwe kuugonga mguu wako juu ya jiwe.’ ”+
7 Yesu akamwambia: “Tena imeandikwa, ‘Usimjaribu Yehova Mungu wako.’ ”+
8 Tena Ibilisi akamchukua, akaenda pamoja naye kwenye mlima mrefu isivyo kawaida, na kumwonyesha falme zote za ulimwengu+ na utukufu wazo,
9 naye akamwambia: “Nitakupa mambo yote haya+ ukianguka chini na kunifanyia tendo la ibada.”+
10 Ndipo Yesu akamwambia: “Nenda zako, Shetani! Kwa maana imeandikwa, ‘Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu,+ na yeye peke yake+ ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’ ”+
11 Ndipo Ibilisi akamwacha,+ na, tazama! malaika wakaja na kuanza kumhudumia.+
12 Sasa aliposikia kwamba Yohana alikuwa amekamatwa,+ aliondoka akaingia Galilaya.+
13 Zaidi ya hayo, baada ya kuondoka Nazareti, alikuja na kukaa katika Kapernaumu+ kando ya bahari katika wilaya za Zabuloni na Naftali,+
14 ili lipate kutimizwa lile lililosemwa kupitia Isaya nabii, akisema:
15 “Ewe nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, kando ya barabara ya bahari, katika upande ule mwingine wa Yordani, Galilaya+ ya mataifa!
16 watu wanaokaa katika giza+ waliona nuru kuu,+ na kwa habari ya wale wanaokaa katika eneo la kivuli cha kifo, nuru+ iliwazukia.”+
17 Kutoka wakati huo na kuendelea Yesu alianza kuhubiri na kusema: “Tubuni,+ kwa maana ufalme+ wa mbinguni umekaribia.”
18 Alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya aliona ndugu wawili, Simoni+ anayeitwa Petro+ na Andrea ndugu yake, wakishusha wavu wa kuvulia samaki ndani ya bahari, kwa maana walikuwa wavuvi.
19 Naye akawaambia: “Nifuateni, nami nitawafanya ninyi kuwa wavuvi wa watu.”+
20 Mara moja wakaziacha nyavu,+ wakamfuata.
21 Pia, alipoendelea mbele kutoka hapo akaona wengine wawili+ waliokuwa ndugu, Yakobo mwana wa Zebedayo+ na Yohana ndugu yake, katika mashua pamoja na Zebedayo baba yao, wakitengeneza nyavu zao, naye akawaita.
22 Mara moja wakaacha ile mashua na baba yao, wakamfuata.
23 Ndipo akaenda akizunguka+ katika Galilaya+ yote, akifundisha katika masinagogi+ yao na kuhubiri habari njema ya ufalme na kuponya kila namna ya ugonjwa+ na kila namna ya udhaifu katikati ya watu.
24 Na habari juu yake ikaenea katika Siria+ yote; nao wakamletea wote waliokuwa na hali mbaya,+ waliokuwa wakitaabishwa na magonjwa na kuteswa kwa namna mbalimbali, wenye roho waovu na wenye kifafa+ na watu waliopooza, naye akawaponya.
25 Kwa sababu hiyo umati mkubwa ukamfuata kutoka Galilaya+ na Dekapoli na Yerusalemu+ na Yudea na kutoka upande ule mwingine wa Yordani.