Mathayo 1:1-25

1  Kitabu cha historia+ ya Yesu Kristo, mwana wa Daudi,+ mwana wa Abrahamu:+   Abrahamu akamzaa Isaka;+Isaka akamzaa Yakobo;+Yakobo akamzaa Yuda+ na ndugu zake;   Yuda akamzaa Perezi+ na Zera kwa Tamari;Perezi akamzaa Hezroni;+Hezroni akamzaa Ramu;+   Ramu akamzaa Aminadabu;Aminadabu akamzaa Nashoni;+Nashoni akamzaa Salmoni;+   Salmoni akamzaa Boazi kwa Rahabu;+Boazi akamzaa Obedi kwa Ruthu;+Obedi akamzaa Yese;+   Yese akamzaa Daudi+ mfalme.+  Daudi akamzaa Sulemani+ kupitia mke wa Uria;   Sulemani akamzaa Rehoboamu;+Rehoboamu akamzaa Abiya;Abiya+ akamzaa Asa;+   Asa akamzaa Yehoshafati;+Yehoshafati akamzaa Yehoramu;+Yehoramu akamzaa Uzia;   Uzia akamzaa Yothamu;Yothamu+ akamzaa Ahazi;+Ahazi akamzaa Hezekia;+ 10  Hezekia akamzaa Manase;+Manase+ akamzaa Amoni;+Amoni+ akamzaa Yosia; 11  Yosia+ akamzaa Yekonia+ na ndugu zake wakati wa ule uhamisho wa kwenda Babiloni.+ 12  Baada ya ule uhamisho wa kwenda Babiloni Yekonia akamzaa Shealtieli;+Shealtieli akamzaa Zerubabeli;+ 13  Zerubabeli akamzaa Abiudi;Abiudi akamzaa Eliakimu;Eliakimu akamzaa Azori; 14  Azori akamzaa Sadoki;Sadoki akamzaa Akimu;Akimu akamzaa Eliudi; 15  Eliudi akamzaa Eleazari;Eleazari akamzaa Mathani;Mathani akamzaa Yakobo; 16  Yakobo akamzaa Yosefu mume wa Maria, ambaye kwake Yesu alizaliwa,+ anayeitwa Kristo.+ 17  Basi, vizazi vyote kutoka Abrahamu mpaka Daudi vilikuwa vizazi kumi na vinne, na kutoka Daudi mpaka uhamisho wa kwenda Babiloni vizazi kumi na vinne, na kutoka uhamisho wa kwenda Babiloni mpaka Kristo vizazi kumi na vinne. 18  Lakini kuzaliwa kwa Yesu Kristo kulikuwa katika njia hii. Katika wakati ambapo Maria mama yake alikuwa amechumbiwa+ na Yosefu, alionekana kuwa ana mimba kwa njia ya roho takatifu+ kabla ya wao kuungana pamoja. 19  Hata hivyo, Yosefu mume wake, kwa sababu alikuwa mwadilifu na hakutaka kumtia aibu mbele ya watu,+ alikusudia kumtaliki+ kwa siri. 20  Lakini alipokuwa amekwisha kufikiria mambo haya, tazama! malaika wa Yehova alimtokea katika ndoto, akisema: “Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria mke wako na kwenda naye nyumbani, kwa maana mimba iliyo ndani yake imetokana na roho takatifu.+ 21  Yeye atazaa mwana, nawe lazima umwite jina lake Yesu,+ kwa maana ataokoa+ watu wake+ kutoka katika dhambi zao.”+ 22  Yote haya kwa kweli yalitukia ili litimizwe lile lililosemwa na Yehova+ kupitia nabii wake,+ akisema: 23  “Tazama! Bikira+ atapata mimba naye atazaa mwana, nao watamwita jina lake Imanueli,”+ ambalo linapotafsiriwa humaanisha, “Mungu Yuko Pamoja Nasi.”+ 24  Ndipo Yosefu akaamka kutoka katika usingizi na kufanya kama malaika wa Yehova alivyokuwa amemwagiza, naye akamchukua mke wake na kwenda naye nyumbani. 25  Lakini hakufanya ngono naye+ mpaka alipozaa mwana;+ na Yosefu akamwita jina lake Yesu.+

Maelezo ya Chini