Mathayo 14:1-36
14 Wakati huo Herode, mtawala wa wilaya, akasikia habari juu ya Yesu+
2 na kuwaambia watumishi wake: “Huyu ndiye Yohana Mbatizaji. Alifufuliwa kutoka kwa wafu, na ndiyo sababu anatenda kazi zenye nguvu.”+
3 Kwa maana Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga na kumweka gerezani kwa sababu ya Herodia mke wa Filipo ndugu yake.+
4 Kwa maana Yohana alikuwa akimwambia: “Si halali wewe kuwa na mwanamke huyo.”+
5 Hata hivyo, ijapokuwa alitaka kumuua, aliuogopa umati, kwa sababu walimwona kuwa nabii.+
6 Lakini sikukuu ya kuzaliwa+ kwa Herode ilipokuwa ikisherehekewa binti ya Herodia alicheza dansi na kumpendeza sana Herode
7 hivi kwamba akaahidi kwa kiapo kumpa chochote kile ambacho angeomba.+
8 Ndipo yeye, chini ya mwelekezo wa mama yake, akasema: “Nipe hapa juu ya sahani kichwa cha Yohana Mbatizaji.”+
9 Ajapokuwa na huzuni, mfalme kwa kufikiria viapo vyake na kwa ajili ya wale wenye kuketi pamoja naye akaamuru apewe hicho;+
10 naye akatuma watu wakamkate Yohana kichwa huko gerezani.
11 Na kichwa chake kikaletwa juu ya sahani na yule mwanamwali akapewa, naye akampelekea mama yake.+
12 Mwishowe wanafunzi wake wakaja na kuiondoa maiti na kumzika+ nao wakaja na kumjulisha Yesu.
13 Aliposikia hilo Yesu akaondoka hapo kwa mashua kwenda mahali pasipo na watu ili awe peke yake;+ lakini umati, uliposikia hilo, ukamfuata kwa miguu kutoka katika majiji.
14 Basi alipotokea akaona umati mkubwa; naye akawasikitikia,+ akaponya wagonjwa wao.+
15 Lakini jioni ilipofika wanafunzi wake wakamjia na kusema: “Mahali hapa hapana watu na saa tayari imesonga sana; acha umati waende zao, ili wapate kwenda vijijini na kujinunulia chakula.”+
16 Hata hivyo, Yesu akawaambia: “Si lazima waondoke: Ninyi wapeni chakula.”+
17 Wakamwambia: “Hatuna kitu hapa ila mikate mitano na samaki wawili.”+
18 akasema: “Vileteni hapa.”
19 Halafu akauamuru umati uketi kwenye majani naye akachukua ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akatoa baraka+ na, baada ya kuimega ile mikate, akawagawia wanafunzi, nao wanafunzi wakaugawia ule umati.+
20 Kwa hiyo wote wakala wakashiba, nao wakaokota vipande vilivyobaki, vikapu kumi na viwili vilivyojaa.+
21 Na bado wale waliokula walikuwa wanaume karibu elfu tano, bila kuhesabu wanawake na watoto wachanga.+
22 Ndipo, bila kukawia, akawaagiza wanafunzi wake waipande mashua na kumtangulia kwenda upande ule mwingine, huku akiwaruhusu umati waende zao.+
23 Mwishowe, baada ya kuwaruhusu umati waende zao, akapanda mlimani akiwa peke yake ili kusali.+ Ingawa ilikuwa jioni, alikuwa huko peke yake.
24 Kufikia sasa mashua ilikuwa mamia mengi ya meta mbali na nchi kavu, ikitaabishwa sana na mawimbi,+ kwa sababu upepo ulikuwa ukivuma kinyume chao.
25 Lakini katika kipindi cha kesha la nne la usiku akawajia, akitembea juu ya bahari.+
26 Walipomwona akitembea juu ya bahari, wanafunzi wakahangaika, wakisema: “Ni mzuka!”+ Nao wakapaaza sauti katika woga wao.
27 Lakini Yesu akasema nao mara moja kwa maneno haya: “Jipeni moyo, ni mimi;+ msiogope.”
28 Petro akajibu, akamwambia: “Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.”
29 Akasema: “Njoo!” Petro akashuka mara moja kutoka kwenye mashua,+ akatembea juu ya maji na kumwendea Yesu.
30 Lakini akiitazama ile dhoruba ya upepo, akaogopa na, alipoanza kuzama, akapaaza sauti: “Bwana, niokoe!”
31 Mara moja Yesu akaunyoosha mkono wake, akamshika na kumwambia: “Wewe mwenye imani kidogo, kwa nini umekuwa na shaka?”+
32 Na baada ya kupanda katika mashua, dhoruba ya upepo ikapunguka.
33 Ndipo wale waliokuwa ndani ya mashua wakamsujudia, wakisema: “Wewe kwa kweli ni Mwana wa Mungu.”+
34 Nao wakavuka na kuja kwenye nchi kavu katika Genesareti.+
35 Walipomtambua, watu wa mahali hapo wakapeleka habari katika nchi yote hiyo jirani, na watu wakamletea wale wote waliokuwa wagonjwa.+
36 Nao wakaanza kumsihi ili wapate kuugusa tu upindo wa vazi lake la nje;+ na wale wote waliougusa wakapona kabisa.