Yona 2:1-10

  • Yona asali akiwa ndani ya tumbo la samaki (1-9)

  • Yona atapikwa kwenye nchi kavu (10)

2  Ndipo Yona akiwa ndani ya tumbo la samaki akasali kwa Yehova Mungu wake,+  na kusema: “Katika taabu yangu nilimlilia Yehova, naye akanijibu.+ Nikiwa ndani ya* Kaburi* nilililia msaada.+ Uliisikia sauti yangu.   Uliponitupa katika vilindi, katikati ya* bahari,Ndipo mikondo ya maji ikanifunika.+ Mawimbi yako yote makubwa na yale yanayoishia ufuoni yakanifunika.+   Nami nikasema, ‘Nimefukuzwa kutoka mbele za macho yako! Nitalikaziaje macho tena hekalu lako takatifu?’   Maji yalinifunika na kuhatarisha uhai wangu;*+Kilindi cha maji kilinizunguka. Kichwa changu kilisokotwa na magugu maji.   Nilizama sehemu za chini za milima. Milango ya dunia ilikuwa ikija kunifungia milele. Lakini uliutoa uhai wangu shimoni, Ee Yehova Mungu wangu.+   Uhai wangu ulipokuwa ukitoka polepole, Yehova Ndiye niliyemkumbuka.+ Ndipo sala yangu ikakufikia, ndani ya hekalu lako takatifu.+   Wale wanaoabudu sanamu ambazo ni ubatili huacha chanzo chao cha upendo mshikamanifu.*   Lakini mimi, kwa sauti ya shukrani nitakutolea dhabihu. Nadhiri nilizoweka, nitazitimiza.+ Wokovu unatoka kwa Yehova.”+ 10  Baadaye Yehova akamwamuru huyo samaki, naye akamtapika Yona kwenye nchi kavu.

Maelezo ya Chini

Tnn., “katika tumbo la.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “katika moyo wa.”
Au “Maji yaliizunguka nafsi yangu.”
Au labda, “cha ushikamanifu.”