Barua ya Yakobo 2:1-26

  • Upendeleo ni dhambi (1-13)

    • Upendo, sheria ya kifalme (8)

  • Imani bila matendo imekufa (14-26)

    • Roho waovu wanaamini na kutetemeka (19)

    • Abrahamu aliitwa rafiki ya Yehova (23)

2  Ndugu zangu, je, mnashika imani ya Bwana wetu mtukufu Yesu Kristo huku mkiwa na upendeleo?+  Kwa maana, ikiwa mtu aliyevaa pete za dhahabu kwenye vidole vyake na aliyevaa mavazi ya kifahari anaingia katika mkutano wenu, na mtu maskini aliyevaa mavazi yenye uchafu anaingia pia,  je, mnamtazama kwa kibali yule aliyevaa mavazi ya kifahari na kumwambia: “Wewe kalia kiti hiki kilicho mahali pazuri,” na kumwambia yule maskini: “Wewe simama tu,” au, “Kalia kile kiti pale chini ya kiti changu cha miguu”?+  Ikiwa ndivyo ilivyo, je, hamna tofauti za kitabaka kati yenu wenyewe+ na je, hamjawa waamuzi wanaotoa maamuzi maovu?+  Sikilizeni, ndugu zangu wapendwa. Je, Mungu hakuwachagua walio maskini kwa maoni ya ulimwengu ili wawe matajiri katika imani+ na warithi wa Ufalme, aliowaahidi wale wanaompenda?+  Lakini ninyi mmemvunjia heshima maskini. Je, si matajiri wanaowakandamiza ninyi+ na kuwakokota wakiwapeleka mahakamani?  Je, hawalikufuru lile jina zuri ambalo kwa hilo mliitwa?  Basi, ikiwa mnaifuata ile sheria ya kifalme kulingana na andiko, “Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe,”+ mnafanya vema.  Lakini mkiendelea kuonyesha upendeleo,+ mnafanya dhambi, na sheria inawahukumu* kuwa wakosaji.+ 10  Kwa maana ikiwa yeyote anatii Sheria yote lakini anajikwaa katika jambo moja, amekosa kuitii Sheria yote.+ 11  Kwa maana yule aliyesema, “Usifanye uzinzi,”+ alisema pia: “Usiue.”+ Basi, ikiwa hufanyi uzinzi lakini unaua, umeivunja sheria. 12  Endeleeni kusema na kutenda kama wale watakaohukumiwa kwa sheria ya watu huru.*+ 13  Kwa maana yule asiye na mazoea ya kuonyesha rehema atahukumiwa bila rehema.+ Rehema hushinda hukumu. 14  Kuna faida gani, ndugu zangu, mtu fulani akisema ana imani lakini hana matendo?+ Je, imani hiyo inaweza kumwokoa?+ 15  Ikiwa ndugu au dada hawana nguo* na chakula cha kutosha kwa ajili ya siku, 16  na mmoja wenu awaambie, “Nendeni kwa amani; mwote moto na mle vizuri,” lakini bila kuwapatia mahitaji ya mwili wao, kuna faida gani?+ 17  Vivyo hivyo pia, imani bila matendo imekufa.+ 18  Hata hivyo, mtu fulani atasema: “Wewe una imani, nami nina matendo. Nionyeshe imani yako bila matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu.” 19  Wewe unaamini kuna Mungu mmoja, sivyo? Unafanya vema. Hata hivyo, roho waovu pia wanaamini na kutetemeka.+ 20  Lakini je, unataka kujua, ewe mwanadamu usiye na akili, kwamba imani bila matendo haifai kitu? 21  Je, Abrahamu baba yetu hakutangazwa kuwa mwadilifu kwa matendo baada ya kumtoa Isaka mwana wake juu ya madhabahu?+ 22  Mnaona kwamba imani yake ilitenda pamoja na matendo yake na imani yake ilikamilishwa kwa matendo yake,+ 23  na andiko likatimizwa linalosema: “Abrahamu alikuwa na imani katika Yehova,* na ikahesabiwa kwake kuwa uadilifu,”+ naye akaitwa rafiki ya Yehova.*+ 24  Mnaona kwamba mtu hutangazwa kuwa mwadilifu kwa matendo, na si kwa imani peke yake. 25  Vivyo hivyo, je, Rahabu yule kahaba hakutangazwa pia kuwa mwadilifu kwa matendo, baada ya kuwakaribisha wale wajumbe na kuwatoa nje kupitia njia nyingine?+ 26  Kwa kweli, kama vile mwili bila roho* umekufa,+ vivyo hivyo, imani bila matendo imekufa.+

Maelezo ya Chini

Au “inawakaripia.”
Tnn., “sheria ya uhuru.”
Tnn., “wako uchi.”
Au “pumzi.”