Barua ya Yakobo 1:1-27

  • Salamu (1)

  • Uvumilivu huleta furaha (2-15)

    • Sifa iliyojaribiwa ya imani (3)

    • Endelea kuomba ukiwa na imani (5-8)

    • Tamaa huongoza kwenye dhambi na kifo (14, 15)

  • Kila zawadi njema hutoka juu (16-18)

  • Kusikia na kutenda neno (19-25)

    • Mtu anayejitazama kwenye kioo (23, 24)

  • Ibada safi na isiyo na unajisi (26, 27)

1  Yakobo,+ mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo, kwa yale makabila 12 yaliyotawanyika sehemu mbalimbali: Salamu!  Oneni yote kuwa shangwe, ndugu zangu, mnapopata majaribu mbalimbali,+  mkijua kwamba sifa iliyojaribiwa ya imani yenu hutokeza uvumilivu.+  Lakini acheni uvumilivu ukamilishe kazi yake, ili muwe kamili na timamu katika mambo yote, bila kukosa kitu chochote.+  Kwa hiyo, ikiwa yeyote kati yenu anakosa hekima, na aendelee kumwomba Mungu,+ kwa maana yeye huwapa wote kwa ukarimu na bila kushutumu,*+ naye atapewa.+  Lakini na aendelee kuomba kwa imani,+ bila kuwa na shaka hata kidogo,+ kwa maana aliye na shaka ni kama wimbi la bahari linaloendeshwa na upepo na kupeperushwa huku na huku.  Kwa kweli, mtu huyo asitarajie kupokea kitu chochote kutoka kwa Yehova;*  yeye ni mtu anayesitasita,+ asiye imara katika njia zake zote.  Lakini ndugu wa hali ya chini na ashangilie katika* kuinuliwa kwake,+ 10  naye tajiri katika kushushwa kwake,+ kwa sababu atapitilia mbali kama ua la shambani. 11  Kwa maana kama jua linavyochomoza pamoja na joto lake linalounguza na kufanya mmea unyauke, na ua lake lianguke na kuharibu urembo wake wa nje, vivyo hivyo pia, tajiri atanyauka katika mambo anayofuatilia.+ 12  Mwenye furaha ni yule anayeendelea kuvumilia jaribu,+ kwa sababu atakapokubaliwa atapokea taji la uzima,+ ambalo Yehova* aliwaahidi wale wanaoendelea kumpenda.+ 13  Mtu akiwa chini ya jaribu, asiseme: “Mungu ananijaribu.” Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu, wala yeye mwenyewe hamjaribu yeyote. 14  Lakini kila mtu hujaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa* na tamaa yake mwenyewe.+ 15  Kisha tamaa, wakati imetunga mimba, huzaa dhambi; nayo dhambi, baada ya kufanywa, huleta kifo.+ 16  Msipotoshwe, ndugu zangu wapendwa. 17  Kila zawadi njema na kila tuzo kamilifu hutoka juu,+ hushuka kutoka kwa Baba wa mianga ya mbinguni,+ ambaye habadiliki au kugeuka kama kivuli.*+ 18  Yalikuwa mapenzi yake kutuzaa sisi kwa neno la kweli,+ ili kwa njia fulani tuwe matunda ya kwanza ya viumbe wake.+ 19  Jueni hili, ndugu zangu wapendwa: Kila mtu lazima awe mwepesi wa kusikia, si mwepesi wa kusema,+ si mwepesi wa hasira,+ 20  kwa maana hasira ya mwanadamu haitokezi uadilifu wa Mungu.+ 21  Kwa hiyo, ondoeni uchafu wote na ubaya wote,*+ na pokeeni kwa upole kupandwa kwa lile neno linaloweza kuwaokoa.* 22  Hata hivyo, iweni watendaji wa neno,+ na si wasikiaji tu, mkijidanganya wenyewe kwa mawazo ya uwongo. 23  Kwa maana ikiwa yeyote ni msikiaji wa neno, na si mtendaji,+ huyo ni kama mtu anayeutazama uso wake* katika kioo. 24  Kwa maana yeye hujitazama na kwenda zake na kusahau mara moja jinsi alivyo. 25  Lakini anayechunguza sheria kamilifu+ ambayo ni ya uhuru na kudumu katika hiyo, amekuwa, si msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi; naye atafurahia kile anachofanya.+ 26  Ikiwa mtu yeyote anafikiri yeye ni mwabudu wa Mungu* lakini haudhibiti* kabisa ulimi wake,+ anaudanganya moyo wake, na ibada yake ni ubatili. 27  Namna ya ibada* iliyo safi na isiyo na unajisi kwa maoni ya Mungu wetu na Baba ni hii: kuwatunza mayatima+ na wajane+ katika dhiki yao,+ na kuendelea kujitunza bila doa kutokana na ulimwengu.+

Maelezo ya Chini

Au “bila kutafuta makosa.”
Tnn., “ajivunie.”
Au “ kunaswa kama kwa kutumia chambo.”
Au “ambaye habadiliki kama kugeuka kwa kivuli.”
Au labda, “wingi wa ubaya.”
Au “kuokoa nafsi zenu.”
Au “uso wake wa asili.”
Au “ni mtu wa dini.”
Au “hauongozi kwa lijamu.”
Au “dini.”