Barua kwa Wakolosai 1:1-29

  • Salamu (1, 2)

  • Shukrani kwa sababu ya imani ya Wakolosai (3-8)

  • Sala kwa ajili ya ukuzi wa kiroho (9-12)

  • Jukumu muhimu la Kristo (13-23)

  • Kazi ngumu ya Paulo kwa ajili ya kutaniko (24-29)

1  Paulo, mtume wa Kristo Yesu kupitia mapenzi ya Mungu, na Timotheo+ ndugu yetu,  kwa watakatifu na ndugu waaminifu katika muungano na Kristo huko Kolosai: Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.  Sikuzote tunamshukuru Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, tunaposali kwa ajili yenu,  kwa kuwa tulisikia kuhusu imani yenu katika Kristo Yesu na upendo mlio nao kwa watakatifu wote  kwa sababu ya tumaini mlilowekewa akiba mbinguni.+ Hapo mwanzoni, mlisikia kuhusu tumaini hili kupitia ujumbe wa kweli ya habari njema  ambayo imekuja kwenu. Kama vile habari njema inavyozaa matunda na kuongezeka ulimwenguni kote,+ ndivyo pia inavyofanya miongoni mwenu, tangu siku mliposikia na kujua kwa usahihi fadhili zisizostahiliwa za Mungu katika kweli.  Hivyo ndivyo mmejifunza kutoka kwa mtumwa mwenzetu mpendwa Epafra,+ ambaye ni mhudumu mwaminifu wa Kristo kwa ajili yetu.  Pia alitujulisha kuhusu upendo wenu katika njia ya kiroho.*  Hiyo ndiyo sababu pia tangu siku tuliposikia kuhusu jambo hilo, hatujaacha kamwe kusali kwa ajili yenu+ na kuomba mjazwe ujuzi sahihi+ wa mapenzi yake katika hekima yote na utambuzi wa kiroho,+ 10  na hivyo mtembee kwa kumstahili Yehova* ili kumpendeza kikamili mnapoendelea kuzaa matunda katika kila kazi njema na kuongezeka katika ujuzi sahihi wa Mungu;+ 11  nanyi mwimarishwe kwa nguvu zote kwa uwezo wake wenye utukufu+ ili mvumilie kikamili kwa subira na shangwe, 12  huku mkimshukuru Baba, aliyewafanya mstahili kushiriki urithi wa watakatifu+ katika nuru. 13  Alituokoa kutoka kwenye mamlaka ya giza+ na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wake mpendwa, 14  ambaye kupitia kwake tunaachiliwa huru kwa fidia, kusamehewa dhambi zetu.+ 15  Yeye ndiye mfano wa Mungu asiyeonekana,+ mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote;+ 16  kwa sababu kupitia kwake vitu vingine vyote viliumbwa mbinguni na duniani, vitu vinavyoonekana na vitu visivyoonekana,+ iwe ni viti vya ufalme au utawala au serikali au mamlaka. Vitu vingine vyote vimeumbwa kupitia kwake+ na kwa ajili yake. 17  Pia, yeye ni wa kabla ya vitu vingine vyote,+ na kupitia kwake vitu vingine vyote vilifanywa kuwapo, 18  naye ndiye kichwa cha mwili, kutaniko.+ Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu,+ ili awe wa kwanza katika mambo yote; 19  kwa sababu Mungu alipenda ujazo wote ukae ndani yake,+ 20  na kupitia yeye apatanishe kwake mwenyewe vitu vingine vyote+ kwa kufanya amani kupitia damu+ aliyomwaga juu ya mti wa mateso,* iwe ni vitu vilivyo duniani au vitu vilivyo mbinguni. 21  Kwa kweli, ninyi ambao zamani mlikuwa mmetengwa, nanyi mlikuwa adui kwa sababu akili zenu zilikuwa zikifikiria matendo maovu, 22  sasa amewapatanisha tena kwa njia ya mwili wenye nyama wa huyo kupitia kifo chake, ili awatoe ninyi mkiwa watakatifu na wasio na dosari na bila shtaka lolote mbele zake+ 23  bora tu, bila shaka, mwendelee katika imani,+ mkiwekwa imara juu ya msingi+ na kuwa thabiti,+ bila kuondoshwa kwenye tumaini la habari njema mliyoisikia, na ambayo ilihubiriwa katika uumbaji wote chini ya mbingu.+ Mimi Paulo, nilikuja kuwa mhudumu wa hii habari njema.+ 24  Ninashangilia sasa katika mateso yangu kwa ajili yenu,+ nami ninakabili dhiki za Kristo ambazo bado hazimo katika mwili wangu kwa ajili ya mwili wake,+ ambao ni kutaniko.+ 25  Nilikuja kuwa mhudumu wa kutaniko hili kupatana na usimamizi+ kutoka kwa Mungu niliopewa kwa ajili yenu ili kulihubiri neno la Mungu kwa ukamili, 26  siri takatifu+ iliyokuwa imefichwa tangu mifumo ya mambo iliyopita*+ na tangu vizazi vilivyopita. Lakini sasa imefunuliwa kwa watakatifu wake,+ 27  ambao Mungu amependezwa kuwajulisha kati ya mataifa utajiri wenye utukufu wa hii siri takatifu,+ ambayo ni Kristo katika muungano nanyi, tumaini la utukufu wake.+ 28  Yeye ndiye tunayemtangaza, tukimwonya kila mtu na kumfundisha kila mtu katika hekima yote, ili tumtoe kila mtu akiwa kamili katika muungano na Kristo.+ 29  Kwa kusudi hili kwa kweli ninafanya kazi kwa bidii, nikijikaza kwa uwezo wake unaotenda ndani yangu kwa nguvu.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “katika roho.”
Angalia Kamusi.
Au “vizazi vya kale.” Angalia Kamusi.