Barua ya Pili ya Petro 2:1-22

  • Walimu wa uwongo watatokea (1-3)

  • Hukumu dhidi ya walimu wa uwongo ni hakika (4-10a)

    • Malaika watupwa ndani ya Tartaro (4)

    • Gharika; Sodoma na Gomora (5-7)

  • Tabia za walimu wa uwongo (10b-22)

2  Hata hivyo, kulikuwa pia na manabii wa uwongo miongoni mwa watu, kama vile pia kutakavyokuwa na walimu wa uwongo miongoni mwenu.+ Hawa wataingiza kimyakimya madhehebu yenye kuharibu, na hata watamkana bwana aliyewanunua,+ na kujiletea maangamizi ya haraka.  Zaidi ya hayo, wengi watafuata mwenendo wao mpotovu,*+ na kwa sababu yao ile njia ya kweli itatukanwa.+  Pia, watawatumia ninyi vibaya kwa pupa wakisema maneno ya uwongo. Lakini hukumu yao iliyoamuliwa zamani za kale,+ haikawii, na maangamizi yao hayalali.+  Hakika Mungu hakujizuia kuwaadhibu malaika waliofanya dhambi,+ bali aliwatupa ndani ya Tartaro,*+ akiwaweka kwenye minyororo* ya giza zito ili wawekwe akiba kwa ajili ya hukumu.+  Naye hakujizuia kuuadhibu ulimwengu wa kale,+ bali alimlinda salama Noa, mhubiri wa uadilifu,+ pamoja na wengine saba+ alipoleta gharika juu ya ulimwengu wa watu wasiomwogopa Mungu.+  Na kwa kuyageuza majiji ya Sodoma na Gomora kuwa majivu, aliyahukumu+ akiweka kielelezo kwa watu wasiomwogopa Mungu kuhusu mambo yatakayokuja.+  Naye alimwokoa Loti mwadilifu,+ aliyetaabishwa sana na mwenendo mpotovu* wa waasi sheria—  kwa maana siku baada ya siku mtu huyo mwadilifu alikuwa akiitesa nafsi* yake yenye uadilifu kwa sababu ya matendo ya kuasi sheria aliyoona na kusikia alipokuwa akiishi miongoni mwao.  Hivyo basi, Yehova* anajua jinsi ya kuwakomboa kutoka kwenye jaribu watu wenye ujitoaji-kimungu,*+ lakini kuwaweka akiba watu wasio waadilifu ili waangamizwe* katika siku ya hukumu,+ 10  hasa wale wanaotaka kutia unajisi miili ya wengine+ na ambao hudharau mamlaka.+ Wana ujasiri na ushupavu, hawaogopi kuwatukana watukufu, 11  lakini malaika, ingawa ni wakuu zaidi katika nguvu na uwezo, hawawashtaki kwa matukano, kwa sababu wanamheshimu* Yehova.*+ 12  Lakini watu hawa, kama wanyama wanaotenda kwa silika na wanaozaliwa* ili kukamatwa na kuangamizwa, wanayatukana mambo wasioyajua.+ Watapata maangamizo yanayoletwa na mwendo wao wenyewe wa maangamizi, 13  wakipata madhara kama thawabu ya mwendo wao wenye madhara. Wanafurahia kuishi maisha ya anasa,+ hata mchana. Wao ni madoa na dosari, wanafurahia* mafundisho yao ya udanganyifu huku wakila karamu pamoja nanyi.+ 14  Macho yao yamejaa uzinzi+ na hawawezi kuachana na dhambi, nao huwashawishi wasio imara.* Moyo wao umezoezwa kuwa na pupa. Wao ni watoto waliolaaniwa. 15  Wameiacha njia iliyonyooka, wamepotoshwa. Wameifuata njia ya Balaamu+ mwana wa Beori, aliyependa thawabu ya kutenda makosa,+ 16  lakini akakaripiwa kwa sababu hakufanya yaliyo sawa.+ Mnyama wa kubeba mizigo asiye na sauti alizungumza kwa sauti ya mwanadamu na kuzuia mwendo wa kiwazimu wa nabii huyo.+ 17  Hao ni chemchemi zisizo na maji na ukungu unaosukumwa na dhoruba kali, nao wamewekewa akiba giza zito kabisa.+ 18  Wao husema maneno ya kujigamba yasiyo na maana. Kwa kuvutia tamaa za mwili+ na kwa matendo ya upotovu wa maadili,* wanawashawishi watu waliotoka tu kuponyoka kutoka kwa watu wanaoishi katika kosa.+ 19  Wanawaahidi uhuru, huku wao wenyewe wakiwa watumwa wa uharibifu;+ kwa maana yeyote anayeshindwa na mwingine, ni mtumwa wake.*+ 20  Hakika ikiwa baada ya kuponyoka unajisi wa ulimwengu+ kupitia ujuzi sahihi kumhusu Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, wanajiingiza tena katika mambo haya na kushindwa, mwisho wao unakuwa mbaya zaidi kuliko mwanzo wao.+ 21  Ingekuwa afadhali kwao kama hawangejua kwa usahihi njia ya uadilifu kuliko baada ya kuijua wageuke kutoka kwenye amri takatifu waliyopokea.+ 22  Wamepatwa na ukweli wa methali inayosema: “Mbwa ameyarudia matapishi yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaagaa kwenye matope.”+

Maelezo ya Chini

Au “ufidhuli; matendo yao ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki, a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au labda, “mashimo.”
Au “ufidhuli; matendo ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki, a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Tnn., “wakatiliwe mbali.”
Au “wana heshima mbele za.”
Au “wanazaliwa kiasili.”
Au “wanaojifurahisha bila kujizuia katika.”
Au “nafsi zisizo imara.”
Au “ufidhuli; matendo ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki, a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.
Au “anayeshindwa na kitu fulani, ni mtumwa wa kitu hicho.”