Barua ya Kwanza ya Yohana 5:1-21

  • Kumwamini Yesu huushinda ulimwengu (1-12)

    • Maana ya kumpenda Mungu (3)

  • Uhakika katika nguvu za sala (13-17)

  • Jihadharini katika ulimwengu mwovu (18-21)

    • Ulimwengu mzima katika nguvu za yule mwovu (19)

5  Kila mtu anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo amezaliwa kutokana na Mungu,+ na kila mtu anayempenda yule aliyesababisha kuzaliwa humpenda yule ambaye amezaliwa kutokana na huyo.  Hivi ndivyo tunavyojua kwamba tunawapenda watoto wa Mungu,+ kwa kumpenda Mungu na kushika amri zake.  Kwa maana kumpenda Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake;+ na bado amri zake si mzigo mzito,+  kwa sababu kila mtu aliyezaliwa* kutokana na Mungu huushinda ulimwengu.+ Na huu ndio ushindi ambao umeushinda ulimwengu, imani yetu.+  Ni nani anayeweza kuushinda ulimwengu?+ Ni yule anayeamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.+  Huyu ndiye aliyekuja kupitia maji na damu, Yesu Kristo, si kwa maji tu,+ bali kwa maji na kwa damu.+ Na roho inatoa ushahidi,+ kwa sababu roho ndiyo kweli.  Kwa maana kuna vitu vitatu vinavyotoa ushahidi:  roho+ na maji+ na damu;+ na hivyo vitatu vinakubaliana.  Tukikubali ushahidi wa wanadamu, ushahidi wa Mungu ni mkuu zaidi. Kwa sababu huu ndio ushahidi ambao Mungu hutoa, ushahidi ambao ametoa kumhusu Mwana wake. 10  Mtu anayemwamini Mwana wa Mungu, ana ushahidi ndani yake. Mtu asiyemwamini Mungu amemfanya yeye kuwa mwongo,+ kwa sababu hana imani katika ushahidi uliotolewa na Mungu kumhusu Mwana wake. 11  Na huu ndio ushahidi, kwamba Mungu alitupatia uzima wa milele,+ na uzima huu umo ndani ya Mwana wake.+ 12  Mtu aliye na Mwana ana uzima huu; mtu ambaye hana Mwana wa Mungu hana uzima huu.+ 13  Ninawaandikia mambo haya ili ninyi mlio na imani katika jina la Mwana wa Mungu+ mjue kwamba mna uzima wa milele.+ 14  Na huu ndio uhakika tulio nao kwake,+ kwamba tukiomba chochote kulingana na mapenzi yake, yeye hutusikia.+ 15  Na ikiwa tunajua kwamba anatusikia kuhusiana na chochote tunachoomba, tunajua kwamba tutapata mambo tuliyomwomba, kwa kuwa tumeyaomba kwake.+ 16  Yeyote akimwona ndugu yake akifanya dhambi isiyoleta kifo, yeye ataomba, na Mungu atampa huyo uzima,+ ndiyo, kwa wale ambao hawafanyi dhambi inayoleta kifo. Kuna dhambi ambayo huleta kifo.+ Simwambii aombe kuhusu dhambi hiyo. 17  Ukosefu wote wa uadilifu ni dhambi,+ na bado kuna dhambi isiyoleta kifo. 18  Tunajua kwamba kila mtu aliyezaliwa kutokana na Mungu hana mazoea ya kufanya dhambi, lakini yeye hulindwa na yule aliyezaliwa kutokana na Mungu,* na yule mwovu hawezi kumshika.*+ 19  Tunajua tunatokana na Mungu, lakini ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.+ 20  Hata hivyo, tunajua kwamba Mwana wa Mungu amekuja,+ naye ametupatia ufahamu* ili tuweze kumjua yule aliye wa kweli. Nasi tumo katika muungano na yule aliye wa kweli,+ kupitia Mwana wake, Yesu Kristo. Huyo ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.+ 21  Watoto wadogo, jiepusheni na sanamu.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kila kitu kilichozaliwa.”
Yaani, Yesu Kristo, Mwana wa Mungu.
Au “hamshiki imara.”
Tnn., “uwezo wa kufikiri; uwezo wa akili.”