Barua ya Kwanza ya Yohana 2:1-29

  • Yesu, dhabihu ya upatanisho (1, 2)

  • Kushika amri zake (3-11)

    • Amri ya zamani na amri mpya (7, 8)

  • Sababu za kuandika (12-14)

  • Msiupende ulimwengu (15-17)

  • Onyo dhidi ya mpinga-Kristo (18-29)

2  Watoto wangu wadogo, ninawaandikia mambo haya ili msitende dhambi. Na bado, yeyote akitenda dhambi, tuna msaidizi* kwa Baba, Yesu Kristo,+ mtu mwadilifu.+  Naye ni dhabihu ya upatanisho*+ kwa ajili ya dhambi zetu,+ lakini si kwa ajili ya dhambi zetu tu bali pia dhambi za ulimwengu wote.+  Na kwa jambo hili tunatambua kwamba tumemjua yeye, yaani, tukiendelea kuzishika amri zake.  Mtu anayesema, “Mimi nimemjua,” na bado hashiki amri zake ni mwongo, na kweli haimo ndani ya mtu huyo.  Lakini yeyote anayeshika neno lake, kwa kweli upendo wa Mungu umekamilishwa katika mtu huyo.+ Hivyo ndivyo tunajua kwamba sisi tumo katika muungano na yeye.+  Mtu anayesema kwamba anakaa katika muungano na yeye, ana wajibu wa kuendelea kutembea kama huyo alivyotembea.+  Wapendwa, siwaandikii amri mpya, bali amri ya zamani ambayo mmekuwa nayo tangu mwanzo.+ Amri hiyo ya zamani ni neno ambalo mlisikia.  Tena, ninawaandikia amri mpya, ambayo ni ya kweli kumhusu yeye na kuwahusu ninyi, kwa sababu giza linapitilia mbali na nuru ya kweli tayari inaangaza.+  Mtu anayesema kwamba yumo katika nuru na bado anamchukia+ ndugu yake bado yumo katika giza.+ 10  Mtu anayempenda ndugu yake hukaa katika nuru,+ naye hana kikwazo chochote. 11  Lakini mtu anayemchukia ndugu yake yumo katika giza na anatembea katika giza,+ naye hajui anakoenda,+ kwa sababu giza limeyapofusha macho yake. 12  Ninawaandikia ninyi watoto wadogo, kwa sababu mmesamehewa dhambi zenu kwa ajili ya jina lake.+ 13  Ninawaandikia ninyi akina baba, kwa sababu mmemjua yule aliye wa tangu mwanzo. Ninawaandikia ninyi vijana, kwa sababu mmemshinda yule mwovu.+ Ninawaandikia ninyi watoto wadogo, kwa sababu mmemjua Baba.+ 14  Ninawaandikia ninyi akina baba, kwa sababu mmemjua yule aliye wa tangu mwanzo. Ninawaandikia ninyi vijana, kwa sababu mna nguvu+ na neno la Mungu hukaa ndani yenu+ nanyi mmemshinda yule mwovu.+ 15  Msiupende ulimwengu au vitu vilivyo katika ulimwengu.+ Yeyote akiupenda ulimwengu, kumpenda Baba hakumo ndani yake;+ 16  kwa sababu kila kitu katika ulimwengu—tamaa ya mwili+ na tamaa ya macho+ na mtu kujionyesha mali zake maishani*—hakitokani na Baba, bali hutokana na ulimwengu. 17  Zaidi ya hayo, ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake,+ lakini yule anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.+ 18  Watoto wadogo, ni saa ya mwisho, na kama vile mlivyosikia kwamba mpinga-Kristo anakuja,+ hata sasa wapinga-Kristo wengi wametokea,+ na kwa sababu hiyo tunajua kwamba ni saa ya mwisho. 19  Waliondoka miongoni mwetu, lakini hawakuwa wa namna yetu;*+ kwa maana kama wangekuwa wa namna yetu, wangebaki pamoja nasi. Lakini waliondoka ili ionekane kwamba si wote walio wa namna yetu.+ 20  Nanyi mmetiwa mafuta kutoka kwa yule mtakatifu,+ na nyote mna ujuzi. 21  Ninawaandikia, si kwa sababu hamwijui kweli,+ bali kwa sababu mnaijua, na kwa sababu hakuna uwongo unaotokana na kweli.+ 22  Ni nani aliye mwongo kama si yule anayekana kwamba Yesu ndiye Kristo?+ Huyo ndiye mpinga-Kristo,+ yule anayemkana Baba na Mwana. 23  Kila mtu anayemkana Mwana hana Baba pia.+ Bali yeyote anayemkiri Mwana+ ana Baba pia.+ 24  Lakini mambo mliyosikia tangu mwanzo yanapaswa kukaa ndani yenu.+ Ikiwa mambo mliyosikia tangu mwanzo yanakaa ndani yenu, ninyi pia mtakaa katika muungano na Mwana na katika muungano na Baba. 25  Zaidi ya hayo, hili ndilo jambo alilotuahidi yeye mwenyewe, uzima wa milele.+ 26  Ninawaandikia mambo haya kuhusu wale wanaojaribu kuwapotosha ninyi.⁠ 27  Kutiwa mafuta ambako mlipokea kutoka kwake+ hukaa ndani yenu, na hamhitaji kufundishwa na yeyote; lakini kutiwa mafuta kutoka kwake kunawafundisha kuhusu mambo yote,+ na ni kweli si uwongo. Kama kulivyowafundisha ninyi, kaeni katika muungano na yeye.+ 28  Basi sasa, watoto wadogo, kaeni katika muungano na yeye, ili atakapofunuliwa tuwe na uhuru wa kusema+ bali tusiaibike wakati wa kuwapo kwake. 29  Ikiwa mnajua yeye ni mwadilifu, mnajua pia kwamba kila mtu aliye na mazoea ya kufanya uadilifu amezaliwa kutokana naye.+

Maelezo ya Chini

Au “wakili.”
Au “dhabihu ya kufunika dhambi; njia ya kuleta maelewano.”
Au “mtu kujigamba kuhusu mali zake.”
Au “hawakuwa wenzetu.”