Kwa Waebrania 1:1-14
1 Zamani sana Mungu alisema na mababu zetu kupitia manabii mara nyingi na kwa njia nyingi.+
2 Sasa kwenye mwisho wa siku hizi amesema na sisi kupitia Mwana,+ mwenye aliweka kuwa muriti wa vitu vyote,+ na mwenye kupitia yeye alifanya mipangilio ya mambo.*+
3 Yeye ndiye murudisho wa utukufu wa Mungu+ na mufano kamili wa utu wake,+ na anategemeza vitu vyote kwa neno la nguvu zake. Na kisha yeye kufanya utakaso wa zambi zetu,+ alikaa kwenye mukono wa kuume wa Ukubwa kule juu.+
4 Kwa hiyo amekuwa muzuri kuliko malaika+ kwa maana ameriti jina la muzuri sana kuliko jina lao.+
5 Kwa mufano, ni nani kati ya malaika mwenye Mungu amekwisha kuambia: “Wewe ni mwana wangu; leo mimi nimekuwa baba yako”?+ Na tena: “Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwana wangu”?+
6 Lakini wakati anamuleta tena Muzaliwa wake wa kwanza+ katika dunia yenye kuikaliwa na watu, anasema: “Na malaika wote wa Mungu wainame mbele yake.”
7 Pia, anasema kuhusu malaika: “Anafanya malaika wake kuwa roho, na watumishi wake*+ kuwa mwali wa moto.”+
8 Lakini juu ya Mwana, anasema: “Mungu ni kiti chako cha ufalme+ milele na milele, na fimbo ya Ufalme wako ni fimbo ya unyoofu.*
9 Ulipenda haki, na ukachukia uvunjaji wa sheria. Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, alikutia mafuta+ kwa mafuta ya furaha kuliko wenzako.”+
10 Na: “Katika mwanzo, Ee Bwana, uliweka misingi ya dunia, na mbingu ni kazi za mikono yako.
11 Hizo zitaangamia, lakini wewe utaendelea kuwa; na zote zitazeeka kama vile nguo,
12 na utazikunja kama ile nguo ya inje, kama nguo, na zitabadilishwa. Lakini wewe ni uleule, na miaka yako haitafikia mwisho hata siku moja.”+
13 Lakini ni juu ya nani kati ya malaika amekwisha kusema: “Kaa kwenye mukono wangu wa kuume mupaka niweke maadui wako kuwa kiti cha miguu yako”?+
14 Je, wao wote hawako roho kwa ajili ya utumishi mutakatifu,*+ wenye walitumwa ili kutumikia wale wenye watariti wokovu?
Maelezo ya Chini
^ Ao “mifumo ya mambo.” Angalia Maana ya Maneno.
^ Ao “watumishi wake wa watu wote.”
^ Ao “haki.”
^ Ao “utumishi wa watu wote.”

