Nehemia 3:1-32

  • Kuta zajengwa upya (1-32)

3  Kuhani mkuu Eliashibu+ na ndugu zake makuhani wakaanza kujenga Lango la Kondoo.+ Wakalitakasa*+ na kuweka milango yake; wakalitakasa mpaka kwenye Mnara wa Mea,+ na mpaka kwenye Mnara wa Hananeli.+  Sehemu iliyofuata ilikuwa ikijengwa na watu wa Yeriko;+ na sehemu iliyofuata ikajengwa na Zakuri mwana wa Imri.  Wana wa Hasenaa walijenga Lango la Samaki;+ walilitengeneza kwa mbao,+ wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo yake.  Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Meremothi+ mwana wa Uriya mwana wa Hakozi, naye Meshulamu+ mwana wa Berekia mwana wa Meshezabeli akarekebisha sehemu iliyofuata, naye Sadoki mwana wa Baana akarekebisha sehemu iliyofuata.  Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Watekoa,+ lakini watu wao mashuhuri hawakutaka kujishusha ili kushiriki kufanya* utumishi wa mabwana wao.  Yoyada mwana wa Pasea na Meshulamu mwana wa Besodeya wakarekebisha Lango la Jiji la Kale;+ walilitengeneza kwa mbao, wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo yake.  Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Melatia Mgibeoni+ na Yadoni Mmeronothi, watu wa Gibeoni na Mispa,+ waliokuwa chini ya mamlaka ya* gavana wa eneo lililo Ng’ambo ya Mto.*+  Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa mafundi wa dhahabu, na sehemu iliyofuata ikarekebishwa na Hanania, mmoja wa watengenezaji wa marashi;* nao wakatandaza mawe* Yerusalemu mpaka kwenye Ukuta Mpana.+  Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Refaya mwana wa Huru, mkuu wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu. 10  Kisha Yedaya mwana wa Harumafu akarekebisha sehemu iliyofuata, yaani, mbele ya nyumba yake mwenyewe, na sehemu iliyofuata ikarekebishwa na Hatushi mwana wa Hashabneya. 11  Malkiya mwana wa Harimu+ na Hashubu mwana wa Pahath-moabu+ wakarekebisha sehemu nyingine,* na pia Mnara wa Majiko ya Kuokea.+ 12  Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Shalumu mwana wa Haloheshi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, pamoja na mabinti zake. 13  Hanuni na wakaaji wa Zanoa+ walirekebisha Lango la Bondeni;+ wakalijenga na kuweka milango yake, makomeo yake, na mapingo yake, pia walirekebisha sehemu ya ukuta yenye urefu wa mikono 1,000* mpaka kwenye Lango la Marundo ya Majivu.+ 14  Malkiya mwana wa Rekabu, mkuu wa wilaya ya Beth-hakeremu+ alirekebisha Lango la Marundo ya Majivu; akalijenga na kuweka milango yake, makomeo yake, na mapingo yake. 15  Shaluni mwana wa Kolhoze, mkuu wa wilaya ya Mispa,+ alirekebisha Lango la Chemchemi;+ akalijenga na kuweka paa lake, milango yake, makomeo yake, na mapingo yake, na pia alirekebisha ukuta wa Kidimbwi+ cha Mfereji unaoelekea kwenye Bustani ya Mfalme+ mpaka kwenye Ngazi+ inayoshuka kutoka Jiji la Daudi.+ 16  Baada yake Nehemia mwana wa Azbuki, mkuu wa nusu ya wilaya ya Beth-suri,+ alirekebisha kuanzia mbele ya Makaburi ya Daudi+ mpaka kwenye kidimbwi+ kilichokuwa kimetengenezwa hadi kwenye Nyumba ya Wenye Nguvu. 17  Walawi walirekebisha sehemu iliyofuata: Rehumu mwana wa Bani; na baada yake Hashabia, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila,+ akarekebisha kwa ajili ya wilaya yake. 18  Ndugu zao wakarekebisha sehemu iliyofuata: Bavai mwana wa Henadadi, mkuu wa nusu ya wilaya ya Keila. 19  Sehemu iliyofuata, mbele ya njia inayopanda kuelekea Ghala la Silaha karibu na Nguzo ya Kutegemeza Ukuta,+ ilirekebishwa na Ezeri mwana wa Yeshua,+ mkuu wa Mispa. 20  Baada yake Baruku mwana wa Zabai+ akafanya kazi kwa bidii na kurekebisha sehemu nyingine, kuanzia Nguzo ya Kutegemeza Ukuta mpaka lango la nyumba ya kuhani mkuu Eliashibu.+ 21  Meremothi+ mwana wa Uriya mwana wa Hakozi alirekebisha sehemu nyingine, kuanzia lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu. 22  Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na makuhani, wanaume wa wilaya ya Yordani.*+ 23  Kisha Benjamini na Hashubu wakarekebisha mbele ya nyumba yao wenyewe. Na baada yao Azaria mwana wa Maaseya mwana wa Ananiya akarekebisha karibu na nyumba yake. 24  Baada yake Binui mwana wa Henadadi akarekebisha sehemu nyingine, kuanzia nyumba ya Azaria mpaka kwenye Nguzo ya Kutegemeza Ukuta+ na mpaka pembeni. 25  Baada yake Palali mwana wa Uzai akarekebisha mbele ya Nguzo ya Kutegemeza Ukuta na mnara unaotoka katika Nyumba ya Mfalme,*+ upande wa juu wa Ua wa Walinzi.+ Baada yake kulikuwa na Pedaya mwana wa Paroshi.+ 26  Na watumishi wa hekaluni*+ walioishi Ofeli+ wakafanya marekebisho hadi mbele ya Lango la Maji+ upande wa mashariki na mnara uliochomoza. 27  Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Watekoa,+ kutoka mbele ya ule mnara mkuu uliochomoza mpaka kwenye ukuta wa Ofeli. 28  Makuhani walirekebisha sehemu iliyo juu ya Lango la Farasi,+ kila mmoja mbele ya nyumba yake mwenyewe. 29  Kisha Sadoki+ mwana wa Imeri akarekebisha sehemu iliyokuwa mbele ya nyumba yake. Na sehemu iliyofuata ikarekebishwa na Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki.+ 30  Sehemu iliyofuata ilirekebishwa na Hanania mwana wa Shelemia na Hanuni mwana wa sita wa Zalafu. Naye Meshulamu+ mwana wa Berekia akarekebisha sehemu iliyokuwa mbele ya jumba lake. 31  Malkiya, mshiriki wa chama cha mafundi wa dhahabu, alirekebisha sehemu iliyofuata mpaka kwenye nyumba ya watumishi wa hekaluni*+ na wafanyabiashara, mbele ya Lango la Ukaguzi mpaka kwenye chumba cha dari cha pembeni. 32  Mafundi wa dhahabu na wafanyabiashara walirekebisha sehemu iliyokuwa kati ya chumba cha dari cha pembeni na Lango la Kondoo.+

Maelezo ya Chini

Au “Wakaliweka wakfu.”
Tnn., “hawakutia shingo zao kwenye.”
Au “maeneo yaliyo magharibi ya Mto Efrati.”
Tnn., “walio wa kiti cha ufalme cha.”
Au “wachanganyaji wa manukato.”
Au “wakatandaza mabamba ya mawe.”
Au “sehemu iliyopimwa.”
Mita 445 hivi (futi 1, 460). Angalia Nyongeza B14.
Au labda, “wilaya jirani.”
Au “Jumba la Mfalme.”
Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”
Au “Wanethini.” Tnn., “waliotolewa.”