Zekaria 9:1-17

  • Hukumu ya Mungu juu ya mataifa jirani (1-8)

  • Kuja kwa mufalme wa Sayuni (9, 10)

    • Mufalme munyenyekevu anapanda juu ya punda (9)

  • Watu wa Yehova watawekwa huru (11-17)

9  Tangazo: “Neno la Yehova liko juu ya inchi ya Hadraki,Na Damasko ndio shabaha yake*+—Kwa maana jicho la Yehova linaangalia wanadamu+Na linaangalia makabila yote ya Israeli—  2  Na juu ya Hamati,+ yenye kuwa kwenye mupaka wakeNa juu ya Tiro+ na Sidoni,+ kwa maana ni wenye hekima sana.+  3  Tiro ilijijengea boma.* Na ilikusanya feza kama mavumbiNa zahabu kama uchafu wenye kuwa katika barabara.+  4  Angalia! Yehova atachukua mali zake,Na atapiga na kuua jeshi lake katika bahari;*+Na itateketezwa ndani ya moto.+  5  Ashkeloni itaona jambo hilo na itaogopa;Gaza itasikia uchungu mukubwa,Ekroni pia, kwa sababu tumaini lake limepatishwa haya. Mufalme ataangamia kutoka Gaza,Na Ashkeloni haitakuwa na wakaaji.+  6  Na mwana-haramu atakaa katika Ashdodi,Na nitamaliza kiburi cha Wafilisti.+  7  Nitaondoa vitu vyenye kuwa na madoa ya damu katika kinywa chakeNa vitu vyenye kuchukiza kutoka katika meno yake,Na atabakia kwa ajili ya Mungu wetu;Na atakuwa kama shehe* katika Yuda,+Na Ekroni kama Muyebusi.+  8  Nitapiga kambi kama mulinzi* kwa ajili ya nyumba yangu,+Na hivyo hakutakuwa mutu mwenye anapita na mwenye anarudia;Na hakuna musimamizi wa kazi* mwenye atapita tena,+Kwa maana sasa nimeiona* kwa macho yangu.  9  Furahi sana, Ee binti ya Sayuni. Piga vigelegele vya ushindi, Ee binti ya Yerusalemu. Angalia! Mufalme wako anakuja kwako.+ Ni mwenye haki, analeta wokovu,*Ni munyenyekevu,+ na amepanda juu ya punda,Juu ya mwana-punda,* mwana wa punda-dike.+ 10  Nitaondoa gari la vita kutoka EfraimuNa farasi kutoka Yerusalemu. Upinde wa mapigano utachukuliwa. Na atatangaza amani kwa mataifa;+Utawala wake utakuwa kutoka bahari mupaka bahariNa kutoka ule Muto* mupaka kwenye miisho ya dunia.+ 11  Sasa wewe, Ee mwanamuke, kwa damu ya agano lako,Nitatosha wafungwa wako ndani ya shimo lenye halina maji.+ 12  Murudie kwenye ngome, ninyi wafungwa wenye tumaini.+ Leo ninakuambia,‘Nitakulipa, Ee mwanamuke, fungu lenye liko mara mbili.+ 13  Kwa maana nitamukunja* Yuda kama upinde wangu. Nitajaza Efraimu katika upinde,*Na nitaamusha wana wako, Ee Sayuni,Wapigane na wana wako, Ee Ugiriki,Na nitakufanya ukuwe kama upanga wa mupiganaji-vita.’ 14  Yehova ataonekana juu yao,Na mushale wake utaenda kama umeme wa radi. Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova atapiga baragumu,+Na ataenda pamoja na zoruba zenye upepo mukali za kusini. 15  Yehova wa majeshi atawalinda,Na watameza na kutiisha majiwe ya kombeo.+ Watakunywa na kufanya makelele, kama wenye walikunywa divai;Na watajazwa kama bakuli,Kama pembe za mazabahu.+ 16  Yehova Mungu wao atawaokoa katika siku hiyoKama kundi la watu wake;+Kwa maana watakuwa kama majiwe yenye samani ya taji, yenye kungaa juu ya udongo wake.+ 17  Kwa maana wema wake ni mukubwa kabisa,+Na uzuri wake ni mukubwa kabisa! Nafaka itafanya vijana wakuwe na nguvu,Na divai mupya itafanya mabikira wakuwe na nguvu.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “ndiko mahali pake pa kupumuzikia.”
Ao “ngome.”
Ao pengine, “juu ya bahari.”
Shehe alikuwa mukubwa wa kabila.
Inaonekana ni taabu ya watu wake.
Ao “mukandamizaji.”
Ao “kambi ya mbele.”
Ao “na ni mwenye ushindi; na ameokolewa.”
Ao “punda-dume.”
Ni kusema, Efrati.
Tnn., “nitamukanyanga.”
Ni kusema, kama mushale.