Zekaria 9:1-17
9 Tangazo:
“Neno la Yehova liko juu ya inchi ya Hadraki,Na Damasko ndio shabaha yake*+—Kwa maana jicho la Yehova linaangalia wanadamu+Na linaangalia makabila yote ya Israeli—
2 Na juu ya Hamati,+ yenye kuwa kwenye mupaka wakeNa juu ya Tiro+ na Sidoni,+ kwa maana ni wenye hekima sana.+
3 Tiro ilijijengea boma.*
Na ilikusanya feza kama mavumbiNa zahabu kama uchafu wenye kuwa katika barabara.+
4 Angalia! Yehova atachukua mali zake,Na atapiga na kuua jeshi lake katika bahari;*+Na itateketezwa ndani ya moto.+
5 Ashkeloni itaona jambo hilo na itaogopa;Gaza itasikia uchungu mukubwa,Ekroni pia, kwa sababu tumaini lake limepatishwa haya.
Mufalme ataangamia kutoka Gaza,Na Ashkeloni haitakuwa na wakaaji.+
6 Na mwana-haramu atakaa katika Ashdodi,Na nitamaliza kiburi cha Wafilisti.+
7 Nitaondoa vitu vyenye kuwa na madoa ya damu katika kinywa chakeNa vitu vyenye kuchukiza kutoka katika meno yake,Na atabakia kwa ajili ya Mungu wetu;Na atakuwa kama shehe* katika Yuda,+Na Ekroni kama Muyebusi.+
8 Nitapiga kambi kama mulinzi* kwa ajili ya nyumba yangu,+Na hivyo hakutakuwa mutu mwenye anapita na mwenye anarudia;Na hakuna musimamizi wa kazi* mwenye atapita tena,+Kwa maana sasa nimeiona* kwa macho yangu.
9 Furahi sana, Ee binti ya Sayuni.
Piga vigelegele vya ushindi, Ee binti ya Yerusalemu.
Angalia! Mufalme wako anakuja kwako.+
Ni mwenye haki, analeta wokovu,*Ni munyenyekevu,+ na amepanda juu ya punda,Juu ya mwana-punda,* mwana wa punda-dike.+
10 Nitaondoa gari la vita kutoka EfraimuNa farasi kutoka Yerusalemu.
Upinde wa mapigano utachukuliwa.
Na atatangaza amani kwa mataifa;+Utawala wake utakuwa kutoka bahari mupaka bahariNa kutoka ule Muto* mupaka kwenye miisho ya dunia.+
11 Sasa wewe, Ee mwanamuke, kwa damu ya agano lako,Nitatosha wafungwa wako ndani ya shimo lenye halina maji.+
12 Murudie kwenye ngome, ninyi wafungwa wenye tumaini.+
Leo ninakuambia,‘Nitakulipa, Ee mwanamuke, fungu lenye liko mara mbili.+
13 Kwa maana nitamukunja* Yuda kama upinde wangu.
Nitajaza Efraimu katika upinde,*Na nitaamusha wana wako, Ee Sayuni,Wapigane na wana wako, Ee Ugiriki,Na nitakufanya ukuwe kama upanga wa mupiganaji-vita.’
14 Yehova ataonekana juu yao,Na mushale wake utaenda kama umeme wa radi.
Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova atapiga baragumu,+Na ataenda pamoja na zoruba zenye upepo mukali za kusini.
15 Yehova wa majeshi atawalinda,Na watameza na kutiisha majiwe ya kombeo.+
Watakunywa na kufanya makelele, kama wenye walikunywa divai;Na watajazwa kama bakuli,Kama pembe za mazabahu.+
16 Yehova Mungu wao atawaokoa katika siku hiyoKama kundi la watu wake;+Kwa maana watakuwa kama majiwe yenye samani ya taji, yenye kungaa juu ya udongo wake.+
17 Kwa maana wema wake ni mukubwa kabisa,+Na uzuri wake ni mukubwa kabisa!
Nafaka itafanya vijana wakuwe na nguvu,Na divai mupya itafanya mabikira wakuwe na nguvu.”+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “ndiko mahali pake pa kupumuzikia.”
^ Ao “ngome.”
^ Ao pengine, “juu ya bahari.”
^ Shehe alikuwa mukubwa wa kabila.
^ Inaonekana ni taabu ya watu wake.
^ Ao “mukandamizaji.”
^ Ao “kambi ya mbele.”
^ Ao “na ni mwenye ushindi; na ameokolewa.”
^ Ao “punda-dume.”
^ Ni kusema, Efrati.
^ Tnn., “nitamukanyanga.”
^ Ni kusema, kama mushale.

