Zekaria 12:1-14
12 Tangazo:
“Neno la Yehova juu ya Israeli,” ni vile Yehova anasema,Ule mwenye alitandika mbingu,+Mwenye aliweka musingi wa dunia,+Na mwenye alifanyiza roho* ya mwanadamu ndani yake.
2 “Angalia, ninafanya Yerusalemu kuwa kikombe chenye kinafanya* vikundi vyote vya watu vya pembeni-pembeni viyumbe-yumbe; na Yuda itazungukwa kwa ajili ya vita na pia Yerusalemu.+
3 Katika siku hiyo nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe nzito* kwa vikundi vyote vya watu. Wale wote wenye wanalinyangula bila shaka wataumia sana;+ na mataifa yote ya dunia yatakusanyika ili kupigana naye.+
4 Katika siku hiyo,” ni vile Yehova anasema, “nitatia kila farasi woga na mupandaji wake nitamutia wazimu. Nitaendelea kuangalia nyumba ya Yuda, lakini kila farasi wa vikundi vya watu nitamupofusha.
5 Na mashehe* wa Yuda watasema katika moyo wao, ‘Wakaaji wa Yerusalemu ni nguvu kwangu kupitia Yehova wa majeshi Mungu wao.’+
6 Katika siku hiyo nitafanya mashehe wa Yuda wakuwe kama chungu chenye kujaa moto kati ya miti na kama mwenge wenye kuwaka moto katika fungu la nafaka yenye imekatwa,+ na watateketeza kwa moto kwenye upande wa kuume na upande wa kushoto vikundi vyote vya watu vya pembeni-pembeni;+ na Yerusalemu itakuwa tena na wakaaji katika mahali pake,* katika Yerusalemu.+
7 “Na Yehova ataokoa mahema ya Yuda kwanza, ili uzuri* wa nyumba ya Daudi na uzuri* wa wakaaji wa Yerusalemu usikuwe mukubwa sana juu ya Yuda.
8 Katika siku hiyo Yehova atakuwa ulinzi kuzunguka wakaaji wa Yerusalemu;+ katika siku hiyo ule mwenye kujikwaa* kati yao atakuwa kama Daudi, na nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yehova mwenye anaenda mbele yao.+
9 Na katika siku hiyo nitahakikisha kuwa ninaangamiza mataifa yote yenye yanakuja kushambulia Yerusalemu.+
10 “Nitamwanga juu ya nyumba ya Daudi na juu ya wakaaji wa Yerusalemu roho ya wema na ya kumulilia Mungu,* na watamuangalia ule mwenye walitoboa,+ na watamuombolezea kama vile wangeombolezea mwana wa pekee; na watamulia kwa uchungu kama vile wangemulia mwana muzaliwa wa kwanza.
11 Katika siku hiyo maombolezo katika Yerusalemu yatakuwa makubwa, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika Bonde la Megido.+
12 Na inchi itaomboleza, kila familia peke yake; familia ya nyumba ya Daudi peke yake, na wanamuke wao peke yao; familia ya nyumba ya Natani+ peke yake, na wanamuke wao peke yao;
13 familia ya nyumba ya Lawi+ peke yake, na wanamuke wao peke yao; familia ya nyumba ya Shimei+ peke yake, na wanamuke wao peke yao;
14 na kila familia zenye kubakia, kila familia peke yake, na wanamuke wao peke yao.

