Zekaria 12:1-14

  • Yehova atalinda Yuda na Yerusalemu (1-9)

    • Yerusalemu, “jiwe nzito” (3)

  • Kuomboleza juu ya ule mwenye alitobolewa (10-14)

12  Tangazo: “Neno la Yehova juu ya Israeli,” ni vile Yehova anasema,Ule mwenye alitandika mbingu,+Mwenye aliweka musingi wa dunia,+Na mwenye alifanyiza roho* ya mwanadamu ndani yake. 2  “Angalia, ninafanya Yerusalemu kuwa kikombe chenye kinafanya* vikundi vyote vya watu vya pembeni-pembeni viyumbe-yumbe; na Yuda itazungukwa kwa ajili ya vita na pia Yerusalemu.+ 3  Katika siku hiyo nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe nzito* kwa vikundi vyote vya watu. Wale wote wenye wanalinyangula bila shaka wataumia sana;+ na mataifa yote ya dunia yatakusanyika ili kupigana naye.+ 4  Katika siku hiyo,” ni vile Yehova anasema, “nitatia kila farasi woga na mupandaji wake nitamutia wazimu. Nitaendelea kuangalia nyumba ya Yuda, lakini kila farasi wa vikundi vya watu nitamupofusha. 5  Na mashehe* wa Yuda watasema katika moyo wao, ‘Wakaaji wa Yerusalemu ni nguvu kwangu kupitia Yehova wa majeshi Mungu wao.’+ 6  Katika siku hiyo nitafanya mashehe wa Yuda wakuwe kama chungu chenye kujaa moto kati ya miti na kama mwenge wenye kuwaka moto katika fungu la nafaka yenye imekatwa,+ na watateketeza kwa moto kwenye upande wa kuume na upande wa kushoto vikundi vyote vya watu vya pembeni-pembeni;+ na Yerusalemu itakuwa tena na wakaaji katika mahali pake,* katika Yerusalemu.+ 7  “Na Yehova ataokoa mahema ya Yuda kwanza, ili uzuri* wa nyumba ya Daudi na uzuri* wa wakaaji wa Yerusalemu usikuwe mukubwa sana juu ya Yuda. 8  Katika siku hiyo Yehova atakuwa ulinzi kuzunguka wakaaji wa Yerusalemu;+ katika siku hiyo ule mwenye kujikwaa* kati yao atakuwa kama Daudi, na nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yehova mwenye anaenda mbele yao.+ 9  Na katika siku hiyo nitahakikisha kuwa ninaangamiza mataifa yote yenye yanakuja kushambulia Yerusalemu.+ 10  “Nitamwanga juu ya nyumba ya Daudi na juu ya wakaaji wa Yerusalemu roho ya wema na ya kumulilia Mungu,* na watamuangalia ule mwenye walitoboa,+ na watamuombolezea kama vile wangeombolezea mwana wa pekee; na watamulia kwa uchungu kama vile wangemulia mwana muzaliwa wa kwanza. 11  Katika siku hiyo maombolezo katika Yerusalemu yatakuwa makubwa, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika Bonde la Megido.+ 12  Na inchi itaomboleza, kila familia peke yake; familia ya nyumba ya Daudi peke yake, na wanamuke wao peke yao; familia ya nyumba ya Natani+ peke yake, na wanamuke wao peke yao; 13  familia ya nyumba ya Lawi+ peke yake, na wanamuke wao peke yao; familia ya nyumba ya Shimei+ peke yake, na wanamuke wao peke yao; 14  na kila familia zenye kubakia, kila familia peke yake, na wanamuke wao peke yao.

Maelezo ya Chini

Ao “pumuzi.”
Ao “bakuli lenye linafanya.”
Ao “lenye ni muzigo.”
Shehe alikuwa mukubwa wa kabila.
Ao “katika mahali pake penye kufaa.”
Ao “utukufu.”
Ao “utukufu.”
Ao “mwenye kuwa muzaifu zaidi.”
Ao “dua.”