Zekaria 7:1-14

  • Yehova analaumu wenye wanafunga kwa unafiki (1-14)

    • “Je, kweli mulifunga kwa ajili yangu?” (5)

    • ‘Mutendeane kwa haki, upendo mushikamanifu, na rehema’ (9)

7  Na katika mwaka wa ine (4) wa Mufalme Dario, neno la Yehova likakuja kwa Zekaria+ katika siku ya ine ya mwezi wa kenda (9), ni kusema, mwezi wa Kislevu.* 2  Watu wa Beteli wakatuma Shareza na Regem-meleki na watu wake ili kuomba rehema ya* Yehova, 3  wakaambia makuhani wa nyumba ya* Yehova wa majeshi na manabii: “Je, nilie katika mwezi wa tano (5)+ na kujizuia kula, kama vile nimekuwa nikifanya kwa miaka hii mingi?” 4  Neno la Yehova wa majeshi likakuja tena kwangu, na kusema: 5  “Ambia watu wote wa inchi na makuhani, ‘Wakati mulifunga na kuomboleza katika mwezi wa tano (5) na katika mwezi wa saba (7)+ kwa miaka makumi saba (70),+ je, kweli mulifunga kwa ajili yangu? 6  Na wakati mulikuwa munakula na kunywa, je, hamukukuwa munakula kwa ajili yenu wenyewe na kunywa kwa ajili yenu wenyewe? 7  Je, hamupaswe kutii maneno yenye Yehova alitangaza kupitia manabii wa zamani,+ wakati Yerusalemu na miji yenye kuizunguka ilikuwa na wakaaji na ilikuwa na amani, na wakati Negebu na Shefela zilikuwa na wakaaji?’” 8  Neno la Yehova likakuja tena kwa Zekaria, na kusema: 9  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Muhukumu kwa haki ya kweli,+ na mutendeane kwa upendo mushikamanifu+ na rehema. 10  Musimupunje mujane wala mutoto mwenye hana baba,*+ mugeni+ wala maskini;+ na musipangiane uovu katika mioyo yenu.’+ 11  Lakini waliendelea kukataa kusikiliza,+ na kwa kichwa-nguvu wakageuza migongo yao,+ na wakafunga masikio yao ili wasisikie.+ 12  Wakafanya mioyo yao kuwa kama almasi*+ na hawakutii sheria* na maneno yenye Yehova wa majeshi alituma kwa roho yake kupitia manabii wa zamani.+ Kwa hiyo Yehova wa majeshi akakasirika sana.”+ 13  “‘Kama vile hawakusikiliza wakati niliita,*+ vilevile sikukuwa ninasikiliza wakati waliita,’+ ni vile Yehova wa majeshi anasema. 14  ‘Na niliwatawanya kwa zoruba ya upepo kila mahali katika mataifa yote yenye hawakujua,+ na inchi iliachwa ukiwa nyuma yao, bila mutu wa kupita ndani ao wa kurudia;+ kwa maana waligeuza inchi yenye kutamanika kuwa kitu cha kuogopesha sana.’”

Maelezo ya Chini

Ao “kutuliza uso wa.”
Ao “hekalu la.”
Ao “yatima.”
Ao pengine, “jiwe ngumu, ” kama vile jiwe la musasa.
Ao “agizo.”
Tnn., “aliita.”