Zekaria 1:1-21
1 Katika mwezi wa munane (8) katika mwaka wa pili wa Dario,+ neno la Yehova likakuja kwa nabii Zekaria*+ mwana wa Berekia mwana wa Ido, na kusema:
2 “Yehova alikasirikia sana baba zenu.+
3 “Uwaambie, ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “‘Munirudilie,’ ni vile Yehova wa majeshi anasema, ‘na mimi nitawarudilia,’+ ni vile Yehova wa majeshi anasema.”’
4 “‘Musikuwe kama baba zenu, wenye manabii wa zamani walitangazia hivi: “Yehova wa majeshi anasema, ‘Tafazali, mugeuke* kutoka kwenye njia zenu za uovu na matendo yenu maovu.’”’+
“‘Lakini hawakusikiliza, na hawakunikazia uangalifu,’+ ni vile Yehova anasema.
5 “‘Baba zenu wako wapi sasa? Na je, manabii waliishi milele?
6 Hata hivyo, je, maneno yangu na maagizo yangu yenye nilipatia watumishi wangu, manabii, hayakufikia baba zenu?’+ Basi walirudia kwangu na kusema: ‘Yehova wa majeshi ametutendea kulingana na njia zetu na matendo yetu, kama vile alikuwa amekusudia kufanya.’”+
7 Katika siku ya makumi mbili na ine (24) ya mwezi wa kumi na moja (11), ni kusema, mwezi wa Shebati,* katika mwaka wa pili wa Dario,+ neno la Yehova likakuja kwa nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido, na kusema:
8 “Niliona maono usiku. Kulikuwa mutu fulani mwenye alikuwa amepanda farasi mwekundu, na alisimama bila kutikisika kati ya miti ya mihadasi katika bonde; na nyuma yake kulikuwa farasi wenye rangi nyekundu, wenye rangi nyekundu yenye kungaa, na weupe.”
9 Basi nikasema: “Hawa ni nani, bwana wangu?”
Malaika mwenye alikuwa anasema na mimi akajibu: “Nitakuonyesha hawa ni nani.”
10 Kisha ule mutu mwenye alikuwa amesimama bila kutikisika kati ya miti ya mihadasi akasema: “Hawa ndio wale wenye Yehova ametuma watembee huku na huku katika dunia.”
11 Na wakamuambia malaika wa Yehova mwenye alikuwa amesimama kati ya miti ya mihadasi: “Tumetembea huku na huku katika dunia, na angalia! dunia yote imetulia na haina usumbufu.”+
12 Basi malaika wa Yehova akasema: “Ee Yehova wa majeshi, ni mupaka wakati gani utazuia rehema yako kuelekea Yerusalemu na kuelekea miji ya Yuda,+ yenye umekasirikia kwa miaka hii makumi saba (70)?”+
13 Yehova akamujibu ule malaika mwenye alikuwa anasema na mimi, kwa maneno ya fazili na yenye kufariji.
14 Kisha ule malaika mwenye alikuwa anasema na mimi akaniambia: “Sema kwa sauti kubwa, ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Niko na bidii kwa ajili ya Yerusalemu na kwa ajili ya Sayuni, bidii kubwa.+
15 Kwa kasirani kali nimekasirikia sana mataifa yenye utulivu,+ kwa sababu nilikasirika kidogo tu,+ lakini waliongeza kwenye musiba.”’+
16 “Kwa hiyo Yehova anasema hivi: ‘“Nitarudia Yerusalemu kwa rehema,+ na nyumba yangu mwenyewe itajengwa kule,”+ ni vile Yehova wa majeshi anasema, “na kamba ya kupimia itanyooshwa juu ya Yerusalemu.”’+
17 “Sema tena kwa sauti kubwa, ‘Yehova wa majeshi anasema hivi: “Miji yangu itajaa tena wema mwingi; na Yehova atafariji tena Sayuni+ na atachagua tena Yerusalemu.”’”+
18 Kisha nikaangalia juu na kuona pembe ine (4).+
19 Kwa hiyo nikauliza ule malaika mwenye alikuwa anasema na mimi: “Hizi ni nini?” Akajibu: “Hizi ndizo pembe zenye zilisambaza Yuda,+ Israeli,+ na Yerusalemu.”+
20 Kisha Yehova akanionyesha mafundi ine (4).
21 Nikauliza: “Hawa wanakuja kufanya nini?”
Akasema: “Hizi ndizo pembe zenye zilisambaza Yuda na hivyo hapakukuwa mutu yeyote mwenye aliweza kuinua kichwa chake. Hizi zingine zitakuja kuziogopesha sana, kuangusha chini pembe za mataifa yenye yaliinua pembe zao juu ya inchi ya Yuda, ili kumusambaza.”