Zekaria 10:1-12

  • Mumuombe Yehova awapatie mvua, musiombe miungu ya uongo (1, 2)

  • Yehova anaunganisha watu wake (3-12)

    • Mutu wa maana kutoka katika nyumba ya Yuda (3, 4)

10  “Mumuombe Yehova mvua katika kipindi cha mvua ya mwisho. Yehova ndiye anafanya mawingu ya zoruba,Yeye ndiye anawamwangia mvua,+Na kupatia kila mutu mimea katika shamba.  2  Kwa maana sanamu za terafimu zimesema* udanganyifu;*Na waaguzi wamepata maono ya uongo. Wanasema juu ya ndoto za bure,Na wanajaribu kutoa faraja lakini wanashindwa. Ndiyo sababu watatanga-tanga kama kondoo. Watateseka, kwa maana hakuna muchungaji.  3  Kasirani yangu inawaka juu ya wachungaji,Na nitaomba viongozi wenye kukandamiza* watoe hesabu;Kwa maana Yehova wa majeshi ameelekeza uangalifu wake kwa kundi lake,+ kwa nyumba ya Yuda,Na amewafanya kuwa kama farasi wake mwenye heshima katika mapigano.  4  Kutoka kwake kunakuja mutu wa maana,*Kutoka kwake kunakuja mutawala mwenye kutegemeza,*Kutoka kwake kunakuja upinde wa vita;Kwake kunatoka kila mwangalizi,* wote pamoja.  5  Na watakuwa kama wapiganaji-vita,Wenye wanakanyanga matope ya barabara katika mapigano. Watapigana vita, kwa maana Yehova iko* pamoja nao;+Na wapanda-farasi watapatishwa haya.+  6  Nitafanya nyumba ya Yuda ikuwe yenye nguvu,Na nitaokoa nyumba ya Yosefu.+ Nitawarudisha,Kwa maana nitawaonyesha rehema;+Na watakuwa kama vile sijawakataa hata siku moja;+Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao, na nitawajibu.  7  Wale wa Efraimu wanapaswa kuwa kama mupiganaji-vita mwenye nguvu,Na moyo wao utafurahi kama wenye walikunywa divai.+ Wana wao wataona jambo hilo na kufurahi;Moyo wao utakuwa wenye furaha katika Yehova.+  8  ‘Nitawapigia muluzi na kuwakusanya pamoja;Kwa maana nitawakomboa,+ na watakuwa wengi,Na wataendelea kuwa wengi.  9  Hata kama ninawatawanya kama mbegu kati ya vikundi vya watu,Watanikumbuka wakiwa katika maeneo ya mbali;Watarudia kwenye uzima pamoja na wana wao na kurudia. 10  Nitawarudisha kutoka inchi ya MisriNa kuwakusanya kutoka Ashuru;+Nitawaleta kwenye inchi ya Gileadi+ na Lebanoni,Na hakutakuwa tena nafasi kwa ajili yao.+ 11  Anapaswa kupita katika bahari kwa taabu;Na ndani ya bahari atapiga mawimbi;+Sehemu zote za chini kabisa za Muto Nile zitakauka. Kiburi cha Ashuru kitashushwa,Na fimbo ya Misri itaondoka.+ 12  Nitawafanya kuwa na nguvu katika Yehova,+Na watatembea huku na huku katika jina lake,’+ ni vile Yehova anasema.”

Maelezo ya Chini

Ao “miungu ya familia imesema; sanamu zimesema.”
Ao “mambo ya uchawi.”
Tnn., “mbuzi-dume.”
Tnn., “munara wa pembe,” wenye unafananisha mutu wa maana; mukubwa.
Tnn., “kipande kidogo cha muti,” chenye kinafananisha mutu mwenye anatoa musaada; mutawala.”
Ao “musimamizi wa kazi.”
Ao “eko.”