Zekaria 10:1-12
10 “Mumuombe Yehova mvua katika kipindi cha mvua ya mwisho.
Yehova ndiye anafanya mawingu ya zoruba,Yeye ndiye anawamwangia mvua,+Na kupatia kila mutu mimea katika shamba.
2 Kwa maana sanamu za terafimu zimesema* udanganyifu;*Na waaguzi wamepata maono ya uongo.
Wanasema juu ya ndoto za bure,Na wanajaribu kutoa faraja lakini wanashindwa.
Ndiyo sababu watatanga-tanga kama kondoo.
Watateseka, kwa maana hakuna muchungaji.
3 Kasirani yangu inawaka juu ya wachungaji,Na nitaomba viongozi wenye kukandamiza* watoe hesabu;Kwa maana Yehova wa majeshi ameelekeza uangalifu wake kwa kundi lake,+ kwa nyumba ya Yuda,Na amewafanya kuwa kama farasi wake mwenye heshima katika mapigano.
4 Kutoka kwake kunakuja mutu wa maana,*Kutoka kwake kunakuja mutawala mwenye kutegemeza,*Kutoka kwake kunakuja upinde wa vita;Kwake kunatoka kila mwangalizi,* wote pamoja.
5 Na watakuwa kama wapiganaji-vita,Wenye wanakanyanga matope ya barabara katika mapigano.
Watapigana vita, kwa maana Yehova iko* pamoja nao;+Na wapanda-farasi watapatishwa haya.+
6 Nitafanya nyumba ya Yuda ikuwe yenye nguvu,Na nitaokoa nyumba ya Yosefu.+
Nitawarudisha,Kwa maana nitawaonyesha rehema;+Na watakuwa kama vile sijawakataa hata siku moja;+Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wao, na nitawajibu.
7 Wale wa Efraimu wanapaswa kuwa kama mupiganaji-vita mwenye nguvu,Na moyo wao utafurahi kama wenye walikunywa divai.+
Wana wao wataona jambo hilo na kufurahi;Moyo wao utakuwa wenye furaha katika Yehova.+
8 ‘Nitawapigia muluzi na kuwakusanya pamoja;Kwa maana nitawakomboa,+ na watakuwa wengi,Na wataendelea kuwa wengi.
9 Hata kama ninawatawanya kama mbegu kati ya vikundi vya watu,Watanikumbuka wakiwa katika maeneo ya mbali;Watarudia kwenye uzima pamoja na wana wao na kurudia.
10 Nitawarudisha kutoka inchi ya MisriNa kuwakusanya kutoka Ashuru;+Nitawaleta kwenye inchi ya Gileadi+ na Lebanoni,Na hakutakuwa tena nafasi kwa ajili yao.+
11 Anapaswa kupita katika bahari kwa taabu;Na ndani ya bahari atapiga mawimbi;+Sehemu zote za chini kabisa za Muto Nile zitakauka.
Kiburi cha Ashuru kitashushwa,Na fimbo ya Misri itaondoka.+
12 Nitawafanya kuwa na nguvu katika Yehova,+Na watatembea huku na huku katika jina lake,’+ ni vile Yehova anasema.”
Maelezo ya Chini
^ Ao “miungu ya familia imesema; sanamu zimesema.”
^ Ao “mambo ya uchawi.”
^ Tnn., “mbuzi-dume.”
^ Tnn., “munara wa pembe,” wenye unafananisha mutu wa maana; mukubwa.
^ Tnn., “kipande kidogo cha muti,” chenye kinafananisha mutu mwenye anatoa musaada; mutawala.”
^ Ao “musimamizi wa kazi.”
^ Ao “eko.”

