Zekaria 3:1-10

  • Maono ya 4: Nguo za kuhani mukubwa zinabadilishwa (1-10)

    • Shetani anamupinga Yoshua Kuhani Mukubwa (1)

    • ‘Nitamuleta ndani mutumishi wangu Chipukizi!’ (8)

3  Na akanionyesha Yoshua+ kuhani mukubwa akiwa amesimama mbele ya malaika wa Yehova, na Shetani+ alikuwa amesimama kwenye mukono wake wa kuume ili kumupinga. 2  Kisha malaika wa Yehova akamuambia Shetani: “Yehova akukemee, Ee Shetani,+ ndiyo, Yehova mwenye amechagua Yerusalemu,+ akukemee! Je, mutu huyu haiko kuni yenye kuwaka yenye imetoshwa katika moto?” 3  Sasa Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu na alikuwa amesimama mbele ya malaika. 4  Malaika akaambia wale wenye walikuwa wamesimama mbele yake, “Mumuvue nguo zake chafu.” Kisha akamuambia, “Ona, nimekuondolea kosa lako,* na utavalishwa nguo za muzuri.”*+ 5  Basi nikasema: “Kilemba safi kiwekwe kwenye kichwa chake.”+ Na wakaweka kilemba safi kwenye kichwa chake na wakamuvalisha nguo; na malaika wa Yehova alikuwa amesimama karibu. 6  Kisha malaika wa Yehova akamuambia Yoshua: 7  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Kama utatembea katika njia zangu na kutimiza mambo yenye unapaswa kutimiza mbele yangu, basi utatumika kama muamuzi katika nyumba yangu+ na utatunza* viwanja vyangu; na nitakupatia uhuru wa kuingia kati ya hawa wenye wamesimama hapa.’ 8  “‘Tafazali, sikia, Ee Kuhani Mukubwa Yoshua, wewe pamoja na wenzako wenye wanakaa mbele yako, kwa maana watu hawa wanatumika kama alama; angalia! ninamuleta ndani mutumishi wangu+ Chipukizi!+ 9  Ona jiwe lenye nimeweka mbele ya Yoshua! Kwenye jiwe hilo moja kuko macho saba (7); na ninachonga maandishi juu yake,’ ni vile Yehova wa majeshi anasema, ‘na nitaondoa hatia ya inchi hiyo kwa siku moja.’+ 10  “‘Katika siku hiyo,’ ni vile Yehova wa majeshi anasema, ‘kila mumoja wenu ataalika jirani yenu akuje chini ya muzabibu wenu na chini ya muti wenu wa tini.’”+

Maelezo ya Chini

Ao “hatia yako.”
Ao “kanzu za heshima.”
Ao “utasimamia; utalinda.”