Mika 3:1-12
3 Nilisema: “Sikieni, tafadhali, enyi viongozi wa YakoboNanyi makamanda wa nyumba ya Israeli.+
Je, hampaswi kujua jambo lililo la haki?
2 Lakini mnachukia mema+ na kupenda maovu;+Mnawachuna ngozi watu wangu na kuondoa nyama kutoka kwenye mifupa yao.+
3 Pia mnakula nyama ya watu wangu+Na kuwachuna ngozi,Mnapasua mifupa yao, na kuivunja vipandevipande,+Kama kitu kinachopikwa ndani ya chungu,* kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.
4 Wakati huo watamlilia Yehova awasaidie,Lakini hatawajibu.
Atauficha uso wake kutoka kwao wakati huo,+Kwa sababu ya matendo yao maovu.+
5 Yehova anasema hivi kuhusu manabii wanaowapotosha watu wake,+Wanaotangaza ‘Amani!’+ huku wakitafuna* kwa meno yao+Lakini wanaotangaza* vita dhidi ya yule asiyeweka kitu vinywani mwao:
6 ‘Mtakuwa na usiku;+ hakutakuwa na maono;+Mtakuwa na giza tu, hakutakuwa na uaguzi.*
Jua litatua kwa manabii,Na mchana utageuka kuwa giza kwao.+
7 Watu wanaoona maono wataaibishwa,+Na wabashiri watakata tamaa.
Wote watalazimika kufunika masharubu,*Kwa maana hakuna jibu kutoka kwa Mungu.’”
8 Lakini mimi, nimejazwa nguvu kwa roho ya Yehova,Nimejazwa haki na uwezo,
Ili nimwambie Yakobo uasi wake na Israeli dhambi yake.
9 Sikieni jambo hili, tafadhali, enyi viongozi wa nyumba ya YakoboNanyi makamanda wa nyumba ya Israeli,+Mnaochukia haki na kupotosha mambo yote yaliyonyooka,+
10 Mnaojenga Sayuni kwa umwagaji wa damu na Yerusalemu kwa ukosefu wa uadilifu.+
11 Viongozi* wake huhukumu ili wapate rushwa,+Makuhani wake hufundisha ili wapate malipo,+Na manabii wake hufanya uaguzi* ili wapate pesa.*+
Na bado wanamwegemea Yehova,* wakisema:
“Je, Yehova hayuko pamoja nasi?+
Hakuna msiba utakaotupata.”+
12 Basi kwa sababu yenu,Sayuni litalimwa kama shamba,Yerusalemu litakuwa marundo ya magofu,+Na mlima wa Nyumba* utakuwa kama vilima msituni.*+
Maelezo ya Chini
^ Au “chungu cha kupikia chenye mdomo mpana.”
^ Au labda, “wanapokuwa na kitu cha kutafuna.”
^ Tnn., “wanaotakasa.”
^ Au “ubashiri.”
^ Au “watafumba vinywa vyao.”
^ Au “wanadai wanamwegemea Yehova.”
^ Au “fedha.”
^ Au “hubashiri.”
^ Tnn., “Vichwa.”
^ Au “mlima wa hekalu.”
^ Au “kilima chenye msitu.”