Hosea 7:1-16

  • Uovu wa Waefraimu (1-16)

    • Hawataepuka wavu wa Mungu (12)

7  “Ninapotaka kuwaponya Waisraeli,Kosa la Waefraimu hufunuliwa pia,+Na uovu wa Samaria.+ Kwa maana wamezoea udanganyifu;+Wezi huvunja na kuingia ndani na makundi ya wavamizi hushambulia nje.+   Lakini hawasemi moyoni mwao kwamba mimi nitakumbuka uovu wao wote.+ Sasa wamezungukwa kabisa na shughuli zao;Ziko mbele kabisa ya uso wangu.   Wanamfanya mfalme ashangilie kwa uovu wao,Na wakuu kwa udanganyifu wao.   Wote ni wazinzi,Wanawaka kama jiko lililowashwa moto na mwokaji,Ambaye huacha kuchochea moto baada ya kukanda unga na kuuacha uumuke.   Katika siku ya mfalme wetu, wakuu wamekuwa wagonjwa—Wana ghadhabu kwa sababu ya divai.+ Amewanyooshea mkono wadhihaki.   Kwa maana wanakaribia kwa mioyo inayowaka kama jiko.* Mwokaji hulala usiku kucha;Asubuhi jiko huwaka kama miali ya moto.   Wote wanawaka moto kama jiko,Nao wanawanyafua watawala* wao. Wafalme wao wote wameanguka;+Hakuna yeyote kati yao anayenililia.+   Waefraimu huchangamana na mataifa.+ Waefraimu ni kama keki ya mviringo ambayo haijaokwa upande mmoja.   Wageni wamenyonya nguvu zao,+ lakini hawajui. Na mvi zimejaa kichwani, lakini hawana habari. 10  Kiburi cha Waisraeli kimetoa ushahidi dhidi yao,+Lakini hawajamrudia Yehova Mungu wao,+Wala hawajamtafuta licha ya hayo yote. 11  Waefraimu ni kama njiwa mjinga, asiye na akili.*+ Wameomba msaada Misri;+ wameenda Ashuru.+ 12  Popote waendapo, nitatandaza wavu wangu juu yao. Nitawaangusha kama ndege wa angani. Nitawatia nidhamu kulingana na onyo ambalo kusanyiko lao lilipewa.+ 13  Ole wao, kwa sababu wamenikimbia! Wataangamia, kwa maana wameniasi! Nilikuwa tayari kuwakomboa, lakini wamesema uwongo dhidi yangu.+ 14  Hawakuniomba msaada kutoka moyoni mwao,+Ingawa waliendelea kulia kwa sauti kubwa vitandani mwao. Walijikatakata kwa sababu ya nafaka na divai yao mpya;Wananigeuka. 15  Ingawa niliwatia nidhamu na kuimarisha mikono yao,Wananipinga, wakipanga njama ya kutenda uovu. 16  Walibadili njia yao, lakini hawakufuata chochote kilichokwezwa;*Walikuwa wasiotegemeka kama upinde uliolegea.+ Wakuu wao wataangamizwa kwa upanga kwa sababu ya ndimi zao za ukaidi. Kwa sababu hiyo watadhihakiwa katika nchi ya Misri.”+

Maelezo ya Chini

Au labda, “Mioyo yao ni kama jiko wanapokaribia kwa hila.”
Tnn., “waamuzi.”
Tnn., “asiye na moyo.”
Yaani, hawakufuata ibada iliyokwezwa.