Hosea 3:1-5

  • Hosea amkomboa mke wake mzinzi (1-3)

  • Waisraeli watamrudia Yehova (4, 5)

3  Kisha Yehova akaniambia: “Nenda tena, mpende mwanamke anayependwa na mwanamume mwingine na ambaye anafanya uzinzi,+ mpende kama Yehova anavyowapenda Waisraeli+ ingawa wanaabudu miungu mingine+ na kupenda keki za zabibu kavu.”*  Basi nikamnunua ili awe wangu kwa vipande 15 vya fedha na homeri moja na nusu* ya shayiri.  Kisha nikamwambia: “Utaendelea kuwa wangu kwa siku nyingi. Usifanye ukahaba,* na usifanye ngono na mwanamume mwingine, nami pia sitafanya ngono nawe.”  Kwa maana Waisraeli watakaa kwa muda mrefu* bila mfalme,+ bila mkuu, bila dhabihu, bila nguzo, na bila efodi+ na sanamu za terafimu.*+  Baadaye Waisraeli watarudi na kumtafuta Yehova Mungu wao+ na Daudi mfalme wao,+ nao watamjia Yehova wakitetemeka na kutafuta wema wake katika kipindi cha mwisho cha zile siku.+

Maelezo ya Chini

Yaani, keki zilizotumiwa katika ibada ya uwongo.
Homeri ni kipimo sawa na lita 220. Angalia Nyongeza B14.
Au “umalaya.”
Tnn., “siku nyingi.”
Au “miungu ya familia; sanamu.”